Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo nitachangia maeneo matatu ambayo Waziri ameyasema kwenye kitabu chake. La kwanza amesema page ya 11 kusimamia Deni la Taifa, la pili kusimamia Taasisi za Mashirika ya Umma na la tatu Kusimamia Sera ya Ubia Kati ya Serikali na Sekta Binafsi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Deni la Taifa ni jambo ambalo lazima tuhangaike nalo vizuri sana, tusipohangaika nalo tunaweza tukajikuta juhudi zote zinazofanywa na TRA kukusanya kodi nyingi zisionekane kwa kiasi kikubwa katika kupeleka maendeleo kwa watu wetu. Katika kuangalia suala la Deni la Taifa, naomba nijikite kwenye suala la interest ambazo tunalipa kwenye madeno haya tunayoyachukua.
Mheshimiwa Naibu Spika, na nitaomba Waziri atakaponijibu aniambie wanampango gani. Interest ni risk management, risk management inahitaji kila siku tuangalie kinachoendelea kwenye uchumi wa dunia. Sisi tunakopa dola, so kitakachotokea kwenye uchumi wa Marekani wale watu woote wanaokopa dola lazima kiwa-affect,sasa tunafanyaje? Ukienda kwenye mikataba yetu yote ya Wizara ya fedha ambayo tumekopa pesa kwa ajili ya kuendesha bajeti jambo jema, interest zetu zote ni liable fractuate ni floating interest, uki-float interest maana yake nini? Unapofanya floating interest maana yake uchumi wa Marekani uki-tilt kwenda juu au kwenda chini utaku-affect kwa sababu kwanza unakopa kwa dola lakini kwa maana nyingi ni kwamba haijawahi kutokea ishuke sana kwamba ile uliyo-float wewe uta-benefit mara nyingi sisi tunapoteza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mfano tumewahi kuchukua kwenye Swiss Credit, ukiangalia interest ya mwezi wa kwanza ni 1.3% lakini ukienda nayo mpaka unamaliza inafika mpaka five percent unafanyaje, ukimuuliza leo Waziri wa fedha mwezi kesho utakapokuwa unalipa ile mshahara, ile first charge ambayo ni interest atuambie ni shilingi ngapi atalipa kama interest Waziri wa Fedha hajui, kwa sababu itategemea situation ya economy ya wakati ule anataka kulipa tunafanyaje sasa kama nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumshauri Waziri wa Fedha umefika wakati watu wa Idara ya Madeni waangalie trend za interest zinaendaje. Wanachofanya wenzetu kuna kitu kinaitwa swapping, una-swap interest rate unazi-swap ili uzi-fix ukifanya fixed rate maana yake unaweza uka-determine cash flow yako.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo wakati unapanga unajua mwezi ujao mshahara kiasi fulani, sijui majeshi kiasi fulani, interest kiasi fulani kwa sababu unajua una uhakika kwa hiyo, ni rahisi katika ku-manage budget ya Serikali, lakini ukiruhusu tukaenda kwenye floating ambayo ukienda kuangalia inavyo fractuate by the end of the year itafika 0.894 maana yake ni nini, Kidata atakusanya pesa nyingi sana, zile fedha zikija nyingi zinakwenda kwenye kulipa madeni mpaka tutaanza kuulizana mbona makusanyo yameongezeka lakini mbona hela haziendi nyingi kwenye Halmashauri, ni kwa sababu hatu-manage interest rate.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Waziri wa Fedha aje ani-critisize hapa kwamba tunafanyaje kwenye suala la ku-budget interest rate ili ku-manage budget ya nchi, ku-manage cash flow zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili nataka kuchangia ni suala la PPP. Waziri wa fedha anasema kwenye kitabu chake page ya 11, kusimamia sera ya ubia kati ya Serikali na sekta binafsi maana yake ni PPP. Ukienda page ya 29, Waziri wa fedha huyo huyo anasema, kwenye suala la kuchukua madeni anasema masharti nafuu ambayo inakopa kwa uangalifu kutumika kwenye miradi yenye vichocheo vya ukuaji wa uchumi ikiwemo ujenzi wa miundombinu, barabara, reli, ujenzi wa mitambo ya kufua umeme, ujenzi wa viwanja vya ndege pamoja na bandari na kadhalika. Maana yake ni nini? Huku unasema unataka ku-embrase PPP, huku unasema nataka nikope kujenga miundombinu, niambieni ni nchi gani Waziri wa Fedha atuambie unaweza ukaleta PPP kama siyo kwenye miundombinu? Tell us? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi kweli kama Serikali kwa nini leo uweke hela kwenda kununua majenereta wakati ukitangaza wako watu wengi sana watanunua majenereta halafu ile fedha ambayo ungenunua majenereta peleka kwenye elimu, peleka kwenye maji, peleka kwenye shule, peleka kwenye kulipa wanajeshi, lipa mapolisi wetu, hii ndiyo management ya economy.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala la PPP naomba tujifunze kwenye aspect moja na Wabunge nataka mnisikilize kwenye suala la simu. Leo vijijini kwetu nani anayeuliza simu hii ni ya nani? Si kila mtu anataka kuwa na simu? Nani anauliza simu hii ni ya Serikali au ni ya nani? Leo tumeweka legal frame work yenye clarity watu wameweka fedha, wamefanya nini leo simu ziko mpaka vijijini, tunapata ajira, tunapata kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bado kwenye mambo mengine tunaona wagumu kweli kuleta watu wa nje ama kuleta PPP na ukiamua ili u-benefit watu wako Waziri wa Fedha, kama nia ni kusaidia private sector ya Tanzania hii ndilo eneo la kusaidia watu. Waambie unataka kujenga bandari, siwezi kukupa kujenga bandari mpaka uwe na Mtanzania, unataka kufungua umeme mpaka uwe na Mtanzania hii ndiyo namna tutaweza kuukuza huu uchumi na ikatusaidia kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukidhani Serikali inaweza ikafanya kila kitu, Serikali hii tutaichosha. Tutashindwa kununua dawa hospitalini, tutashindwa kupeleka hela kwenye education kwa sababu leo hii tunasema elimu bure maana yake ni nini, watoto wengi sana wana-access watakuwa wengi tutahitaji kujenga madarasa, tutajenga kila kitu, hii ni hatari sana kwenye economy. Nikuombe Waziri wa Fedha, tulipitisha sheria ya PPP mwaka 2009, tuanze kuitekeleza sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine nilitaka kulizungumzia ni suala la Mashirika ya Serikali. Taasisi za umma, naombeni Waziri wa Fedha na hii kazi ya Waziri wa fedha pamoja na kukusanya kodi lazima ufanye jukumu la kukuza uchumi wa nchi. Utaukuza uchumi wa nchi kama tuta-embrase biashara. Kama bandari wanafanyabiashara waacheni kuwaingilia, waacheni wafanye kazi za biashara. Kama TANESCO wanafanya biashara waambieni wafanye maamuzi ya kibiashara, ninyi kazi yenu mwisho wa siku muwaulize tu though TR tunaomba dividend mwisho wa mwezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Serikali kuna baadhi ya maeneo tuna-share. Kwa mfano nitasema PUMA Serikali ina asilimia 50 lakini Waziri wa fedha naomba nikwambie kwenye bulk procurement hamjawahi kutumia Kampuni yenu ya PUMA hata siku moja. Kwenye kununua mafuta mnanunua kwa watu wengine hii ni nini? Huku mna-share, mnapata dividend lakini mnapoanza kununua mnanunua kwa watu wengine, hivi nani asiyejipenda? Ukienda South Africa leo hakuna mfanyakazi wa Serikali ambaye hapandi Ndege ya South African Airways. Leo tunaingiza pesa, tunajenga ndege kitakachotokea kwenye ticket mtapanda Emirates, maana tunaulizana maswali hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunataka mashirika haya na taasisi za Serikali yachangie kwenye uchumi wa nchi tuyaache yafanye kazi kibiashara. Naombeni sana bila kufanya hivyo hatutokwenda, naombeni tuanze kazi ya kuamini wafanyabiashara nao ni watu na niombe Waziri wa Fedha, tuache kufikiria wafanyabiashara ni wezi. Tuweke mazingira ya kuzuia wasikwepe kodi lakini tujue ni watu tunaowahitaji kwa maendeleo ya Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ninalotaka kusema ni suala la bei ya mafuta, again narudi kwenye interest pale pale, bei ya mafuta duniani imeshuka weee, imefika mpaka barrel kwa pipa shilingi dola 29, leo imefika dola 50. Maana yake ni nini kwenye uchumi? Sisi tumekaa tunasubiri tu dunia iamue mafuta yakipanda sawa yakishuka sawa. Kazi ya Waziri wa Fedha, Idara yako hiyo ya Sera na ya Madeni ni kuangalia vitu hivi kinachotokea kwenye uchumi kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tulichotakiwa tufanye, tungefanya oil hedging baada ya mafuta tulivyoona yanaanza kurudi, yameanza kufika ishirini na tisa, thelathini tunge-hedge tukasema mafuta yetu ya miezi sita tuta hedge kwa dola 30 per barrel. Na uki-hedge wanafanya watu wote, kama watu binafsi wanafanya, watu binafsi wanapata interest ndogo, kwa nini Serikali tusipate? Ni kwa sababu tunataka kufikirie vilevile tulivyozoea. Uki-hedge Waziri wa Fedha, maana ukiacha, mafuta yakiendelea kupanda maana yake bajeti yako inakuwa tilted, yale uliyoyapanga kununua mafuta haitawezekana, itabidi ubane. Rais amekuja na jambo zuri sana, Rais ameweka austerity measure kubwa, ana-manage economy, anapunguza matumizi, sasa tumsaidie.
Tumsaidie kwa kuangalia trend za market kwenye dunia. Leo mafuta mwaka jana…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.