Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii kuchangia kwenye hoja ya Wizara muhimu, Wizara ya fedha. Nianze kwanza kwa kuipongeza Wizara, Waziri pamoja na timu yake kwa kufanya kazi zao vizuri sana na kwa hotuba nzuri na pia kwa kutupa muelekeo ni kwa namna gani wamejipanga kuhakikisha kuwa yale malengo ambayo walikuwa wametupa mwanzoni yatatimia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo nilitaka na mimi nijaribu kushauri mambo machache. La kwanza ni suala zima la ukusanyaji wa mapato. Naona kwa muda mrefu sana tumetegemea mapato yetu kupitia TRA. Sidhani kama tukiendelea namna hiyo itakuwa sustainable ili tuweze kufikia hayo malengo na kukiangalia ni namna gani kipindi chote kilichopita tulikuwa tunazungumzia kuhusu miradi mbalimbali na Wabunge wengi tumezungumzia kuhusu namna ya kutumia pesa, hatukupata muda namna gani hizo pesa tutakazotumia zitatoka wapi na zitakusanywa wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kiasi kikubwa naona nchi yetu ina uwezo mkubwa wa kujitegemea na bila hata kutegemea misaada kutoka nje. Tukiweza kujipanga vizuri, tukaangalia zile fursa tulizonazo ambazo ni nje ya zile za kodi ambazo tulikuwa tumezizoea nafikiri malengo yetu yanaweza kutimia kwa haraka sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, angalia ofisi ya TR, tunashukuru kwanza imeimarishwa sasa hivi kuna timu nzuri. Nafikiri tukiendelea kuimarisha hii timu, kuna nafasi ya kukusanya pesa nyingi kutoka kwenye mashirika yetu. Tuangalie ni kiasi gani ambacho Serikali imewekeza mitaji kwenye hayo mashirika. Je, haya mashirika yamepewa malengo ya kurudisha kiasi gani Serikalini? Mabilioni na mabilioni yapo huko lakini ukisoma kwenye report ya Waziri anaangalia ni namna gani ya kuyasaidia haya mashirika yalipe madeni, nafikiri hilo Waziri jaribu kuangalia, dunia ya leo ni dunia ambayo inaangalia zaidi tuende Kibiashara zaidi. Tuongeze capacity kwenye mashirika yetu, tuwe na management zinazoeleweka, tuangalie mifano ya mashirika yanayofanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, angalia Shirika kama NMB, benki kama NMB ilivyokuwa? Ilikuwa imefilisika lakini leo inafanya kazi vizuri sana. Sababu yake kubwa ni nini? Ni kwa sababu Serikali ilihakikisha kuwa inaweka management nzuri na leo hii ukilinganisha NMB na NBC ninaimani NMB inafanya vizuri zaidi. Angalia Shirika la Nyumba lilivyokuwa hoi lakini baada ya kuweka management nzuri, Shirika la Nyumba sasa hivi linafanya vizuri sana. Kwa hiyo, na haya mashirika mengine naomba mpe uwezo mkubwa sana TR aweze kuangalia hata vilevile management zitakazokuwepo pale na bodi zitakazokuwepo pale, hilo lizingatiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine nilichokuwa namuomba Waziri aangalie ni Benki ya Wakulima. Naona kwenye repoti ya Kamati wametoa mawazo mazuri sana ya milioni 59 zile ambazo zililengwa kwenda kwa ajili ya Mfuko wa Vijiji zipelekwe kwenye Benki ya Wakulima na mimi hilo naungana nao. Hizi zitasaidia sana ili zilete chachu huko vijijini, wakulima waweze kupata mikopo kirahisi lakini pia na zile pesa ziweze kusimamiwa kitaalamu. Lakini vilevile milioni 59 ni kidogo mno, naomba ziongezwe zifikie hiyo bilioni 196 ambayo ni asilimia 20 ya bilioni 980.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo ningependa zaidi Wizara iliangalie; ushiriki wa mabenki kwenye uchumi wa nchi yetu. Riba za mabenki ni kubwa sana ukilinganisha tofauti ya riba anayolipwa anayeweka pesa (depositor) na anayekopa ni kubwa kupita kiasi na tumeona kwa muda mrefu haya mabenki yanatengeneza pesa nyingi sana, lakini ni namna gani hizi pesa wanazozitengeneza ambazo zimetokana wakati mwingine na amana za walalahoi zimeweza kurudisha kwa wale watu ambao ni depositors. Nafikiri hili nilijaribu kuliangalia, hizi riba za asilimia 20, asilimia 18 ni kubwa mno. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine; unapoangalia amana nafikiri Mheshimiwa Waziri aangalie pesa zinazozunguka kwenye miamala ya M-pesa or mobile money, ni kubwa mno. Hizi tumeziangalia vipi ya kwamba nazo zinawezakusaidia kwenye uchumi wa nchi hii? Zinasimamiwa vipi? Nafikiri hilo tuendelee kuliangalia vizuri. Ukiangalia katika hotuba ya Wizara hapa, hajaiona hiyo kama ni sehemu mojawapo ya amana tulizonazo nchi hii ambazo zinaweza kusaidia katika uchumi wa nchi yetu. Amana inayozunguka kwa mwezi mmoja ni zaidi ya trilioni 4.5, hizo ni nyingi mno. Chukulia kidogo tu, ya kwamba unaweza kuchukuklia hata 0.5 zirudi kwenye uchumi wetu, utapata bilioni zaidi ya 270. Naomba na hilo liangaliwe kwa karibu, tuweke mfumo vilevile wa kuzilinda.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ningependekeza tuangalie vilevile ni namna gani tuweke usimamizi wa hizi pesa ambazo Wizara zinakwenda kwenye miradi yetu. Nafikiri hapa kuna tatizo kubwa kwa sababu kama Wizara itapeleka pesa kwenye Halmashauri au kwenye miradi asilimia yote ile ikaliwa hiyo mojawapo ni kwamba yale mapato tunakuwa tumeyapoteza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunakuwa hatuna sababu ya kuzungumzia kutafuta mapato wakati tunashindwa kusimamia vizuri matumizi ya hayo mapato. Ukichukulia mfano, kwenye Halmashauri ya kwangu kuna bilioni zaidi ya two point five zimepelekwa kwa ajili ya miradi ya maji lakini mpaka leo unashindwa kuuliza ni nani ambaye anasimamia zile pesa. Maji hayatoki, miradi huioni! Makandarasi huwaoni!
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hizo ni pesa za wananchi, ni pesa za kodi, nani anazisimamia? Zimetoka Wizara ya Fedha labda zimekwenda Wizara ya Maji na zimekwenda Halmashauri, msimamizi ni nani hapo katikati? Na hili nafikiri ni tatizo kubwa, nafikiri tuweke coordination kati ya hizi Wizara zinazohusika ili tuweze kusimamia hii miradi yetu vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Sika, baada ya kusema hayo ningependa kwa kumalizia kuipongeza hii Wizara na pia suala zima la commodity exchange ingawa nimeongelea kwa kiasi kidogo sana lakini nafikiri hiki ni chombo muhimu sana hasa kwa wakulima. Tuiangalie kianzishwe haraka ili kiweze na wakulima wakafaidika na mazao hayo ambayo kwa sasa hivi tunapovuna, mahindi bei inakuwa kidogo sana lakini baada ya muda mfupi bei zinapanda. Kwa hiyo, kama kukiwa na chombo kama hiki kinaweza kusaidia ili wakulima waweze kufaidika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja.