Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimpongeze Waziri wa Fedha na Naibu Waziri wa Fedha kwa mipango na bajeti nzuri ya kwanza wa Serikali ya Awamu ya Tano ambayo kusema ukweli ni bajeti ambayo ni realistic.
Mimi nimesimama ili nizungumze pamoja na mambo mengi ambayo yamechangiwa na Waheshimiwa Wabunge, yanayohusu Wizara ya TAMISEMI ambayo ndiyo Wizara ya wananchi, lakini ndiyo Wizara inayokwenda kubadili maisha kwa maana ya huduma za Jamii ambazo wananchi wanazitarajia kutoka kwenye Serikali yao, pia waheshimiwa Wabunge mliahidi sana kule kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, yako mambo megi ambayo mmesema juu yamaji, juu ya miundombinu, lakini mimi nimesimama hapa kwa sababu ya muda nizungumzie eneo moja ambalo limeonekana kuchangiwa na Wabunge wengi sana takribani Wabunge 27 wamezungumzia suala la huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitoe takwimu ya hali tuliyonayo kwa sasa kwenye zahanati na vituo vya afya. Tunavyo vijiji 12,545 na sera yetu inasema kila kijiji lazima kiwe na zahanati, zahanati tulizonazo ni 4,700 tu.
Kwa hiyo, tuna upungufu wa zahanati takribani 7,845 kwa sababu tulizonazo ni asilimia 38 tu, utauona upungufu huu ni mkubwa. Lakini sera yetu pia inasema tutakuwa na kituo cha afya kila kata, tunazo kata 3,963 na tuna vituo vya afya 497 tu ni asilimia 13 ya mahitaji. Kwa hiyo upungufu wetu ni vituo vya afya 3,466.
Mheshimiwa Naibu Spika, mamlaka ya Serikali za Mitaa zimejitahidi sana, kuna ujenzi mbalimbali ya majengo ambayo sasa tunayaita maboma, tunayo jumla ya maboma ya zahanati 1,443; tunayo jumla ya maboma ya vituo vya afya 244 na tunayo jumla ya maboma ya hospitali za Wilaya 51, kazi hii imefanywa vizuri sana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa nchini. Mpango wetu sasa wa kushirikiana kwa Serikali nzima tumejaribu kuongea na Waziri wa Fedha na Waziri wa Afya ambaye yeye anasimamia utoaji wa huduma na Wizara ya TAMISEMI ndiyo inayojenga, inamiliki na kuendesha utoaji huu wa huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumejaribu kuzungumza, jambo la kwanza tulilokubaliana ni kwamba tupitie upya ramani ile ili iwe ramani ambayo inamudu kwa uchumi wetu lakini itatoa huduma zinazostahili zote. Kwa sababu ramani iliyopo Waheshimiwa Wabunge kama mnavyofahamu ni kubwa kiasi kwamba inakatisha tamaa kwa vituo vya afya kuwa na ramani kubwa kiasi kile. tulipoipunguza ramani ile tunahitaji kiasi kama cha bilioni 2.5 kwa kila kituo cha afya kilichokamilika na huduma zake zote kutolewa ikiwa ni pamoja na upasuaji, fedha hizi bilioni 2.5 Waziri wa Fedha ananiambia tunaweza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa bajeti hii ya sasa niombe mambo mawili, la kwanza tuendelee na mpango wetu ule ule wa Halmashauri kuwa na mpango wa kuwa na zahanati kila kijiji waendelee na mpango wa wananchi na Halmashauri kuendelea, isipokuwa sisi Serikali kuu tuone namna ambavyo tutakuja na mpango wetu sasa wa ujenzi wa vituo vya afya, hapa tunaweza tukafanya vizuri kwa sababu kwa upungufu tulionayo, tukiwa tunajenga kila Halmashauri kituo cha afya kimoja kila mwaka wa fedha nina hakika kwa miaka mitatu iliyobakia tutakuwa tumejenga vituo vitatu vitatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tutakuwa na vituo vya afya vingi tu kuliko hata tulivyojenga toka tulivyopata uhuru. Kwa hiyo, mimi nasema kwa bajeti hii ambayo tunakwenda nayo yakwanza hii ambayo imetenga takribani bilioni 32 kwa ajili ya umaliziaji wa maboma haya niliyoyataja, itatufikisha mahali fulani. Lakini bado niwaombe na niombe sana kwamba tuhakikishe tunasimamia own source hii ambayo tulipanga kukusanya ili maboma haya ya vituo vya afya yakamilike kwa sababu ndiyo tuliyopitisha kwenye bajeti hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo yakikamilika haya maboma tutakuwa tumekamilisha zahanati 1.443, vituo vya afya 244 itakuwa ni hatua moja mbele ili tukija kwenye bajeti inayokuja ya mwaka 2017/2018 tutakuja na mpango huu sasa ambao tutakuja na bajeti mahususi kwa ajili ya vituo vya afya kama nilivyosema ambayo kama tutakwenda hivyo kila mwaka, kila Halmashauri ikajenga kimoja ambacho kinakamilika nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tunaweza tukajenga vituo vya afya vingi kwa miaka mitano, na hata tukimaliza miaka yetu mitano tukaweza kusema tumefanya kitu gani kila mmoja kwenye jimbo lake.
Waheshimiwa Wabunge, niwasihi na niwaombe sana, muunge mkono bajeti hii ya Serikali ili iweze kutekelezwa kama ambayo tumepitisha kwa shilingi bilioni 32 katika sekta ya afya lakini tusimamie tu michango yetu kwa makusanya ya Halmashauri yaweze kukusanywa kwa sababu utoaji wa huduma siyo ujenzi tu wa haya majengo, pia kuna suala la watumishi kwa idadi inayotakiwa ya watumishi. Lakini pia ni jambo ambalo linahitaji katika ukamilifu wake ili iweze kutoa huduma ile tunayostahili, kwa hiyo lazima haya yote yaende yakiwa yanaandaliwa kwa pamoja, tusikurupuke tukawa na majengo lakini vitu vingine vikawa haviendi sawa sawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mnafahamu tuna upungufu wa wataalamu wa afya, lazima tuwe na huo uwezo na wenyewe pia ujengwe sambamba na ujenzi wa haya maboma.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilidhani haya ndio machache ambayo yamesemwa,na mimi nimeona nizungumzie kwenye jambo hili la afya, nirudie tena kutoa wito Waheshimiwa Wabunge tukashirikiane kule; tuhimize makusanyo ya Halmashauri ili mipango tuliyoipanga hii maana imepangwa na sisi iweze kutekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.