Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza kabisa nianze kwa pongezi. Naomba kwanza nimpongeze Rais wetu JPM maarufu sana Mzee wa hapa kazi tu, maana hili jina la J J mara nyingi linanitatiza sana lakini kwa kweli kwanini nampongeza Rais wetu? Ameonesha namna nzuri na mwelekeo wa Awamu ya Tano ya hapa kazi tu kwa kukusanya kodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu muda wangu ni mdogo, nataka niende haraka na nitaongea mambo mengi, nakwenda moja kwa moja kwenye suala la maji. Wananchi wametutuma huku kwa sababu wanahitaji kuishi, na maji ni uhai. Kwa kuwa maji ni uhai nimwombe ndugu yangu Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa Wabunge wengi tunahitaji kuleta mawazo ya wananchi wapate maji, mimi nakuwa wa kwanza ku-declare kwamba, tufanye namna yoeyote watu wapate maji kule vijijini na mbinu ya kufanya hayo ni kuongeza kale katozo kadogo tu, ka sh. 50 tu kwenye tozo ya mafuta ya petrol na diesel. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia sasa hivi petrol imeshuka thamani yaani bei imeshuka, lakini ukiangalia kwenye bidhaa zote hakuna mahali ambako inaonekana kabisa bei ya chochote imeshuka, nauli ziko pale pale, kila kitu kiko hapo hapo. Kwa hiyo, naomba niungane na Wabunge wenzangu waliojaribu kuweka mawazo yao kwamba, tuweke sh. 50 ili basi watu wetu wapate maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri anakumbuka, nilitamani kutoa Shilingi siku ile ya Wizara ya Maji wakati wana-present hapa kitu kinachoitwa bajeti yao. Kwa kuwa maji kwenye Wilaya yangu ya Mbulu Vijijini wanahitaji bilioni tatu, nikiangalia kwenye bajeti humu haimo, tunaipata wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Waziri, niombe basi, nimetumwa na Wanambulu kutafuta maji humu, tumetumwa na ndoo. Slogan ya kwamba, tunamwondolea mama ndoo kichwani tutapata wapi kama tusipokuwa makini hapa kuhakikisha kwamba, tunayapata maji? Ndugu zangu Wabunge, hebu tuongelee kwa kilio chetu eti, tunahitaji kupata maji, hatuna namna nyingine zaidi jamani, zaidi ya kutafuta mwanya wa kupeleka maji vijijini. Kwenye Mji wangu wa Hydom kuna miradi 10 ile ambayo imeshafanywa, yani Serikali imepeleka pesa pale, lakini haikamiliki kutokana na nini? Hakuna pesa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niombe, kwa kweli Serikali mkikubali kuweka mpenyezo tu huu mdogo wa Sh. 50 kwenye kila lita, naamini tukahakikisha kwamba pesa hii inakwenda kule mahali ambako tumeamua hapa Bungeni na ikasimamiwa; na sasa hivi tunajua Mheshimiwa Rais ameweka mipango mizuri, Mawaziri wote mmesoma. Mama yangu! Serikali hii ya JPM iki-fail mimi sipeleki mtoto shule.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivi? Watu wameenda shule, ni Madaktari, ni Maprofesa, sisi tulioingia humu tumekuja tu kuwawakilisha tu wananchi wetu kwa kuomba haya na tunaposema haya tunamaanisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine kwa sababu muda ni mfupi niende kwenye suala la afya, afya tunalo tatizo kubwa mno. Leo hii ukimwambia mwananchi achague kati ya kujenga kiwanda na kujenga zahanati au kituo cha afya, atakwambia ni kituo cha afya kwa sababu anahitaji kuona afya yake inaboreka. Kwa hiyo, nina masikitiko makubwa sana. Ukiangalia kwenye Wizara ya Afya kwenye pamflet letu hapa, inaonesha kabisa Mbulu Vijijini hata kituo kimoja cha afya hakijaingia huku wala zahanati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niombe, naamini inawezekana ni typing error, kwa sababu tuna hata own source ya Halmashauri yetu tumeweka na tumetuma huko, lakini kutokana na ukomo wa bajeti natambua kwamba kuna tatizo hilo, kwa hiyo, naomba kabisa Mheshimiwa Waziri aangalie sehemu hii hasa suala la afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna sababu ya kuzianzisha hospitali au zahanati mpya. Akifanya research vijijini kuna zahanati na hospitali ambazo zimekaa muda mrefu hazijamaliziwa. Kwa mfano kule Dongobeshi Mbulu; wananchi wamechanga wamejenga hospitali yao, wamejenga theatre, wanasubiri sasa hivi kuezeka tu. Kwa hiyo, Serikali wakiweka kitu kidogo hapa kwa bajeti hii tunamalizia, tunaanza kazi, naomba niseme haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine nataka nijielekeze kwenye hii milioni 50 ambayo kimsingi ni ilani ya Chama cha Mapinduzi, tumewaahidi watu kwamba, milioni 50 zitakwenda vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kitu kimoja; ukisema leo milioni 50 iende vijiji; nimeamini kwamba, bajeti inasema wataanza kutekeleza baada ya mwezi Juni, lakini naomba ni-question, ukipeleka fedha hizi kabla ya mwezi Juni hakuna financial institutions ambazo ziko kule zitakazosaidia watu hawa kupata pesa zao as equal katika vijiji vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipendekeze tu kitu kimoja; kwa sababu ukiangalia kwenye maendeleo ya jamii hapa au kwa hawa watu wanaojiita Maafisa Maendeleo, Maafisa Ushirika, nchi nzima wako 400 na hawa hawawezi kusimamia zile fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuangalie namna ya kuunda hizi benki za vijijini ili angalau watu wetu waweze kusaidiwa namna nzuri ya kupeleka na kuweza kukopa na kukopeshwa. Ziende kwa mtiririko kulikoni kwenda moja kwa moja kwa namna ya kisiasa, vinginevyo tutapoteza kama tulivyopoteza zile fedha za Mheshimiwa JK au maarufu sana kama mabilioni ya JK.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala hili ambalo kidogo linakula vichwa vya wananchi, wameanza kutupigia simu huku; suala la transaction money kwenye hizi finance institution. Mimi sina tatizo sana na ukusanyaji wa kodi, lakini naomba niielekeze Serikali iangalie sana. Hizi transaction charges ambazo zimewekewa VAT kwenye Sheria ya Kodi, niombe kabisa Serikali iwe makini isije ikawa sasa wakayatoza mabenki, haya mabenki haya baadaye yakaamua kupeleka au kuweka VAT kwenye transaction za mtoaji wa mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano sasa hivi wanafunzi wengi wana pesa ndogo wanazopewa kwenye boom. Akienda kutoa pesa zake kuweka kwenye simu kutoka benki anachajiwa, akiangalia salio anachajiwa ikiwemo VAT ndani, akituma anachajiwa, sasa mtu wa kawaida atakuwa amechajiwa mara nne kabla ya kutumia fedha hizo. Kwa hiyo, naomba Serikali iwe makini sana kuangalia hali hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine niangalie eneo moja la watalii. Kuna jambo hili la watalii tuliangalie vizuri, nimesoma bajeti ya Kenya, ukiangalia wao wamekuwa wajanja wameondoa ile VAT katika kuwaingiza watalii kwenye mbuga zao. Sasa nashauri hebu angalieni namna ya kuweka kodi hii, aidha iwekwe kwenye vitanda au kwenye mahoteli, lakini ukimwekea hapa inakuwa ni tatizo. Kenya ukiangalia wameweka pesa zao nyingi katika kuwa- accommodates watalii na pia wametangaza utalii wao; angalia bajeti ya Kenya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimsihi sana ndugu yangu Mheshimiwa Philip Mpango, najua ana mipango mingi na yeye ni rafiki yangu sana na ni baba ambaye nimeendelea kumpenda. Basi aangalie eneo hili namna ya kuweza kuwaingiza hawa watu wetu wasitutoroke. Sisi tuna utalii kule Mbulu, asituone hivi watu wanataka kwenda kuangalia Wahadzabe, wale click language ambao wamekaa interior kule, wanafikaje ukiweka kodi kwenye hili eneo? Itakuwa ngumu, watakatia Kenya wapotelee huko huko. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, East Afrika sasa hivi kila mtu anataka kuvutia kamba kwake. Nimsihi ndugu yangu aangalie eneo hili vizuri, wataalam wa kodi walimshauri vizuri hapa ili anapo-charge kodi asimshtue mtu anayeitwa mtalii kabla hajaingia kwetu. Bahati mbaya sana ukiangalia kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii hakuna fedha nyingi aliyoweka kwa ajili ya advertisement ya utalii wa Tanzania. Kwa hiyo, niombe sana hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua muda wangu umekwisha, lakini naunga mkono hoja. Ahsante sana.