Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Awali ya yote napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia siku ya leo, na hasa katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani ambapo waislamu wote kote nchini wanatimiza miongoni mwa nguzo tano zile ni pamoja na kufunga Ramadhani. Namshukuru Mungu, nawatakia kila la heri wale wote ambao wamewajaliwa kutimiza nguzo hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa dhati ya moyo wangu na kama sikusema haya hakika sitaietendea haki nafsi yangu, naomba binafsi nikupongeze sana kwa kazi nzuri unayoifanya. Kuna usemi wanasema usimdharau usiyemjua. Awali wakati unaingia kwenye nafasi hii nilipata shida sana kuona kweli Naibu Spika utamudu nafasi hii! Kwa kweli, umeitendea haki nafsi zetu, lakini umetufurahisha akinamama wenzako, hakika unatuwakilisha vizuri endelea kuchapa kazi tuko pamoja na wewe na Inshallah tunakuombea uendelee kuwa salama mpaka tarehe Mosi tunapomaliza kufunga Bunge hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana niwapongeze, Waziri wa Fedha na Naibu Waziri, wamewasilisha mpango mzuri na wametupa nafasi hata sisi Wabunge ya kuona nini kimeandaliwa katika bajeti hii. Naomba niwapongeze sana kwa kazi nzuri wanayoifanya, lakini yako mambo mengi yamezungumzwa mazuri. Miongoni mwa mambo mazuri lazima kuwe na changamoto. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie upande wa afya. Waheshimiwa Wabunge, wenzangu wengi wamezungumzia kuhusu ujenzi wa vituo vya afya na zahanati, niwapongeze sana na mimi nakubaliana nao moja kwa moja, lakini mimi naomba sana nizungumzie suala la ikama ya watumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, utakuwa shahidi na Mheshimiwa Waziri anayehusika atakuwa shahidi kwamba tunalo tatizo la watumishi wachache katika Idara hii ya afya. Mimi niombe sana tuliangalie jambo hilo, kwa kuwa tunalo tatizo la hawa watumishi ni vizuri kupitia vile vijiji vyetu wako kule vijana ambao wamejifunza uhudumu wa afya, ni vizuri tukawaangalia wale kuwapa mafunzo, ili wawe wanasaidia kutoa huduma za afya kwenye zahanati na vituo vya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiofichika, hata tukienda sasa hivi kwenye vijiji vyetu unaweza ukakuta mhudumu mmoja, huyo huyo ataandika cheti, huyo huyo atachoma sindano, huyo huyo ataenda kuhudumia kusafisha vidonda, kazi zote anatakiwa azifanye. Kwa hiyo, mimi binafsi niliona sana kulingana na muda huu mfupi nijikite sana kwenye eneo hili katika kuhimiza kupata watumishi wa afya kwenye vituo vya afya na zahanati zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo naomba nilizungumzie ni suala la miradi ya maji. Tumekuwa tukizungumza sana kuhusiana na suala la miradi ya maji, siyo siri iko miradi ambayo tayari wananchi wetu wamekabidhiwa, lakini upo ukweli usiofichika kwamba, miradi ile mpaka sasa iko miradi mingine haifanyi vizuri, haitoi maji ipasavyo. Mimi naomba sana, kupitia Wizara husika, ufanyike uhakiki wa kuona ni miradi gani ambayo imekabidhiwa kwa wananchi, lakini haitoi maji ipasavyo kuona sasa hatua zichukuliwe katika kuhakikisha tunaifanyia ukarabati na wananchi wetu wanapata maji ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, yamezungumzwa mambo mengi, lakini naomba pia nizungumzie suala la kupunguza tozo kwa wakulima. Kwenye taarifa yao wamezungumza na hasa kwenye suala la wakulima wa korosho. Kama alivyoeleza Mheshimiwa Dkt. Mpango katika mpango wake kwamba watahakikisha wanapunguza tozo mbalimbali kwa wakulima na mimi nakubaliana nao kwa sababu, zipo tozo ambazo zilikuwa zinawakandamiza sana wananchi wetu. kwa kuwa wameanza kupunguza baadhi ya tozo nasisitiza sana waendelee kuziangalia hizo tozo ambazo hazina maslahi kwa wananachi wetu, ni vizuri kuziondoa ili wakulima waone waone tija ya kile wanachokifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala zima la bajeti. Hapa tunazungumzia bajeti tumeweka mipango mingi ambayo tunakusudia tupige hatua, lakini kama hatujasimamia ukusanyaji mzuri wa mapato, mimi naamini haya yote tunayozungumza hayawezi kuzaa matunda. Mimi nasisitiza sana kwenye haya mambo ambayo tumekusudia kwenye hivi vyanzo vya mapato ni vizuri tuvisimamie ili hii miradi ambayo tunaikusudia ifanyike, ifanyike kwa jitihada na itafanyika vizuri kama kile ambacho tumekusudia kukikusanya kitakusanywa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala zima la bajeti. Hapa tunazungumzia bajeti tumeweka mipango mingi ambayo tunakusudia tupige hatua, kama hatujasimamia ukusanyaji mzuri wa mapato naamini haya yote tunayozungumza hayawezi kuzaa matunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninasisitiza sana katika haya mambo ambayo tumekusudia katika vyanzo vya mapato ni vizuri tuvisimamie ili hii miradi ambayo tunaikusudia ifanyike, ifanyike kwa jitihada na itafanyika vizuri kama kile ambacho tumekusudia kukikusanya kitakusanywa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie jambo…..

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na ninaunga mkono hoja.