Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi jioni ya leo ili kuchangia. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wataalam kwa ujumla, mengi nimechangia kupitia Kamati ya Bajeti. Kwa leo kuna machache ambayo nadhani iko haja ya kuongezea ili kumtengeneza ng‟ombe vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimewasikiliza wachangiaji wengi ni kama vile dhana haieleweki kwamba Serikali inataka na sisi tujazie ya kwetu, badala yake watu wanakuja wanalalamika kama vile essence ya kuwepo wao kuchangia haina maana. Tungewasikia wapi kama fursa hii isingepatikana, kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge ni fursa ya kuchangia ili tuwe na mpango mzuri kwa ajili ya kulivusha Taifa hili, Taifa ni la kwetu sote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma maoni ya Kambi ya Upinzani wanachokisema ni kama vile wana nchi ya kwao kiasi kwamba hata boti hili likienda vibaya wao wana option ya pili, haitujengi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo ambayo nimeyatoa kwa utangulizi naomba nichangie kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirejee ukurasa wa saba wa kitabu cha Mheshimiwa Waziri ambayo katika matazamio yake anatarajia kwamba bei ya mafuta itaendelea kuwa nzuri. Naomba tukumbushane OPEC walishakubaliana kwamba watapunguza uzalishaji wa mafuta, tafsiri yake ni nini? Kama uzalishaji wa mafuta utapungua maana yake bei itapanda, sasa katika mipango yetu lazima tulijue hili na tukishalijua sasa tujiandae tunafanyaje kama Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwombe Mheshimiwa Waziri, ni manufaa yapi ambayo tulipata kama Taifa baada ya bei kushuka? Kwa sababu haiwezekani tuache liende kama linavyoenda bei ikishuka hakuna ambacho Serikali inafanya, bei ikipanda hakuna ambacho Serikali inafanya. Ni vizuri tukawa na mkakati maalum kwamba pale ambapo inatokea bei kushuka tuone faida moja kwa moja ambayo inapatikana kutokana na anguko la bei ya mafuta. Lakini ingependeza sana kama ungeanzishwa Mfuko Maalum ili kuweza ku-stabilize pale ambapo bei zikipanda sana basi kuwe na namna ya kuweza ku-absolve shock ambazo zinajitokeza wakati bei za mafuta zimepanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi sote ni mashuhuda kwamba pale ambapo bei ikipanda hata siku moja tayari siku inayofuata tunaambiwa nauli zinapanda na kila kitu kinapanda. Sasa ni vizuri katika mipango yetu tukajiandaa tunaitumiaje fursa kama hiyo pale inapotokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika mpango wa maandalizi ya bajeti kuna prediction kwamba hali ya chakula itakuwa nzuri. Naomba nipingane na hili kwasababu kwa taarifa tulizonazo ni kwamba kuna ukame unatarajiwa kuwepo. Kwahiyo, hatuwezi tukasema hali ya chakula itakuwa nzuri, sio sahihi. Kwa hiyo, kwenye mipango yetu lazima factor hiyo tuiweke na tuseme sasa hiki kinachotokea tunafanyaje ili hali ya uchumi wetu isije ikaharibika kwa kiasi kikubwa. Ni vizuri katika mipango ambayo inawekwa tukaweka hiyo factor kwa sababu ipo; kama jambo una uhakika litatokea ukajifanya kwamba hulijui utakuwa husaidii Taifa. Ni vizuri tukalijua, tukajiandaa kwamba tunafanyaje kama Taifa ili tusije tukapata tabu kutokana na upungufu wa chakula.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimewasikiliza wenzangu kuhusiana na kupungua kwa mizigo bandarini. Ni kweli, lakini ambacho ningeomba kiingie na kionekane vizuri kwenye mipango yetu, sisi sote ni mashuhuda kwamba bandari ya Dar es Salaam haina uwezo wa kupokea meli kubwa za kuanzia 3G, 4G uwezo huo hatuna, nini kifanyike? Tumekuwa tukisikia muda mrefu kwamba bandari ambayo itajengwa Bagamoyo itakuwa na uwezo mkubwa wa kuweza kupokea meli za ukubwa wa fourth generation.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukipata fursa ya kutembelea bandari ya Mombasa ukaona uwekezaji uliofanywa na wenzetu na hawakuishia kwenye Bandari ya Mombasa wameenda sasa Bandari ya kule Lamu, kiasi kwamba tusitarajie. Hata kama tutafanya upanuzi wa geti namba 13, 14 bila kuanza seriously ujenzi wa bandari ya Bagamoyo hakika tunajiandaa kwenda kushindwa kama Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni vizuri katika mipango yetu tukajielekeza katika hilo kwamba hata ungepanua vipi Bandari ya Dar es Salaam imeshafika mwisho. Kwahiyo, ni vizuri katika mipango yetu tukajielekeza katika kuanza kujenga bandari ya kisasa ambayo itakuwa na uwezo wa kupokea meli za kisasa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa napitia taarifa na hii pia tulikutana nayo hata wakati tumekutana na Wizara ya Fedha. Kuna fikra ndani ya Serikali kwamba mpango unaokuja sasa hivi juu ya currency yetu ni kuhama kutoka utaratibu wa fluctuation floating twende kwenye fixed na fikra iliyopo Serikalini ni kwamba tu-peg shilingi yetu kuibadilisha na dola kwa shilingi 2,193 kama sijakosea, ni jambo jema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili tafsiri yake ni nini? Ni kwamba tayari tunajiandaa kwamba shilingi yetu inakwenda kuanguka, faida ya ku-devalue shilingi inakuwa ni rahisi kwa mtu ambaye anakuja kuwekeza kwetu kwa ile direct foreign investment lakini disadvantage ambayo tunakuwa nayo ni kwamba itakuwa ni gharama sana kwa mtu ambaye anataka kupeleka mizigo nje kutoka Tanzania akija kubadilisha na pesa yetu atakuta anapata hasara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri hii hali ya kuacha soko ndio liamue na tutafute namna nzuri ambayo itahakikisha kwamba shilingi yetu haiyumbi sana, ndiyo namna iliyokuwa nzuri kulikoni habari ya kwamba unasema fixed, ukishafanya fixed ikija kutokea kipindi uchumi umeanguka maana yake tutalazimika ku-devalue shilingi yetu kwa kiasi kikubwa sana. Ni vizuri ikafanyika tathmini na utafiti wa kutosha kabla hatujafikia hatua hiyo, tujue madhara ambayo tumekuwa nayo kwa kuachia bei ya soko ni yapi na hicho ambacho tunatarajia kukifanya faida yake ni ipi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inapendeza sana tukiwa na makampuni ya Kitaifa kwa ajili ya Watanzania, sioni katika mpango unaokuja nia thabiti ya kuhakikisha kwamba TPDC inawezeshwa kwa niaba ya Watanzania ili kuweza kushiriki katika upstream na downstream katika suala zima la mafuta na gesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mikataba iliyopo mizuri kabisa inaonesha kwamba, wakiweka mtaji basi ushiriki wao na share ambayo watakuwa wanapata ni kubwa, lakini pale ambapo hawezeshwi kwa maana ya capital, kitabaki kugawanywa kile kidogo ambacho kimebaki. Sasa kwa Taifa ambalo tungependa kampuni ya Taifa kama zilivyo State Oil, Petrolbras ni kwamba Serikali zao ziliwekeza ndiyo maana makampuni haya yakawa na uwezo mkubwa. Ni vizuri na sisi tukahakikisha kwamba TPDC inawezeshwa kwa ajili ya Watanzania walio wengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la uvuvi wa bahari kuu. Silioni hili likijitokeza dhahiri lakini limekuwa likisemwa siku nyingi. Nakumbuka katika bajeti iliyotangulia ya 2015/2016 ilikuja Wizara ya Uvuvi wakisema kwamba wanahitaji pesa kwa ajili ya kununua meli ya doria. Ikatengwa nadhani kama shilingi milioni 500 wakapewa, hadithi ya hiyo pesa imetumikaje mpaka leo haijulikani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe, haiwezekani kile ambacho tunapata kwenye bahari kinazidiwa na maziwa ya Victoria na Tanganyika. Maana yake kuna tatizo kubwa ambalo hatujafanya kiasi kwamba wanakuja Wakorea kuvua samaki wengi sana wanatajirika kutoka katika maji ya kwetu lakini sisi kama Taifa tunapata nini? Ni vizuri sasa likajitokeza waziwazi kwamba kama Taifa tunafaidika vipi na bahari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo kuhusiana na General Tyre; sisi sote ni mashahidi, Wabunge wote tunatumia magari, kwa hiyo hatuna jinsi lazima tununue matairi kwa ajili ya magari, kwa hiyo soko lipo wazi hata kama mngekuwa na uhakika wa ku-service gari za Wabunge tu una uhakika wa kupata tairi ambazo zina ubora lakini soko lipo la kutosha nchi zote hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kasi ya kufufua General Tyre ni vizuri ikaonekana dhahiri; haipendezi tukaendelea kutazama tu kwenye makaratasi, inatosha tunataka utekelezaji. Kama imeshindikana tuambizane kwamba idea hii imeshindikana, labda tuanze thinking nyingine, lakini ukirejea kama miaka minne, mitano General Tyre inatajwa, Mchuchuma na Liganga inatajwa, kule Natron inatajwa, itoshe kutajwa tunataka kwenda kutenda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini katika Serikali hii ya Awamu ya Tano ambayo tunataka maneno kidogo vitendo viwe vingi, vitendo vikiwa vingi huna haja ya kusema sana wenzako watakuwa wanatafuta namna gani ya kukosoa. Lakini pale unapotenda kama ambavyo tumetenda kuhusiana na suala zima la ndege, kuna wengi walibeza wengine wakasema ni ndege chakavu, lakini ukija hata asiyekuwa na macho atapapasa, atajua kwamba hii siyo ndege chakavu, ni ndege mpya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana na naunga mkono hoja.