Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kutoa mchango wangu jioni ya leo. Vilevile nimshukuru Mwenyezi Mungu, muweza wa yote aliyeniwezesha kusimama kuweza kuzungumza jioni ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana sana wananchi wa Tanzania kwa kujua mchele ni upi na pumba ni zipi na kuchagua Chama cha Mapinduzi kwa ushindi wa kishindo kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa upande wa Wabunge 73% na kwa upande wa Madiwani 74% na kwa upande wa Viti Maalum 80%, kwa kweli wananchi Mwenyezi Mungu awajalie sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachoweza kusema hapa, tunawaahidi kwamba imani huzaa imani, tutaendelea kuwatumikia kwa moyo wetu wote na hata pale ambako Chama cha Mapinduzi hakikupata kura tutawahudumia bila ubaguzi likiwemo Jimbo la Arusha na Majimbo mengine ambako CCM haikushinda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nichukue nafasi hii kumpongeza sana, mpendwa wetu Rais wetu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa jinsi alivyoanza kutekeleza kazi. Ameanza vizuri, anafanya kazi nzuri na kama kura zingepigwa leo ushindi wa CCM ungekuwa ni 69.999%. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya utangulizi huo, napenda sasa kujielekeza kwa mambo machache ambayo nimeyapanga kuyatilia mkazo katika hoja iliyo mbele yetu. Kwanza kabisa, naomba kuunga mkono hoja iliyo mbele yetu kwa sababu zifuatazo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu yangu ya kwanza ni kwamba, Waziri wa Fedha na timu yake yote wameandaa vizuri Mwelekeo wa Mpango wa mwaka 2016/2017. Ni Mpango unaoeleweka, wenye matumaini na ambao umelenga kuwakomboa Watanzania katika suala zima la kuwakomboa kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa sababu endapo Mpango huu utapangwa na ukatekelezwa, nina imani yale ambayo tumeyaandika kwenye Ilani ya CCM yataweza kufikiwa. Naomba sasa nitoe ushauri kwa mambo machache yafuatayo na nitaanza suala zima la ukusanyaji wa kodi. Ili mpango utakaotengenezwa usiendelee kubaki kwenye makaratasi, nilikuwa naishauri Serikali yetu hii ya CCM ijielekeze katika kuhakikisha inakusanya mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kupongeza kazi nzuri ambayo imeanza kufanywa ya kukusanya mapato, lakini bado kuna baadhi ya mapato yanaishia mifukoni mwa watu, pia bado kuna mashine za kukusanyia mapato ni feki na bado kuna taasisi ambazo zinatumia vitabu ambavyo havieleweki katika mfumo wa Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba niishauri Serikali ili Mpango wa Maendeleo uweze kutekelezwa katika mwaka 2016/2017, lazima pia tuweke mkakati namna ambavyo Serikali itakusanya mapato. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nishauri Serikali yetu na Mawaziri wetu kwamba, katika kutekeleza Mpango huu, hauwezi kutekelezeka kama hawajadhibiti upotevu wa mapato na matumizi yasiyokuwa ya lazima. Naiomba sana Serikali yetu, ijielekeze katika kuhakikisha Mpango unaokuja 2016/2017 unalenga kwenda kuwakomboa Watanzania na hasa wanawake. Naomba Mpango unaokuja 2016, tujielekeze katika kuhakikisha suala zima la maji na hasa vijijini linapatiwa ufumbuzi ili wanawake wetu wanaotembea umbali mrefu waweze kupata maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu, mwaka jana tulipanga mpango mzuri, lakini kwa bahati mbaya sana, hivi ninavyozungumza, sekta ya maji imepata asilimia nane tu ya bajeti. Sasa kama tutatengeneza mpango mzuri kama utakavyokuja na kama fedha hazikutafutwa na zikatengwa, Mpango wetu utabaki kwenye makaratasi na matokeo yake lengo ambalo limekusudiwa halitafikiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba katika kuhakikisha Mpango unatekelezwa ni lazima tujielekeze sasa kuweka vipaumbele katika sekta ambazo zitaongeza mapato na napongeza mpango wa Serikali wa kuhakikisha tunafufua viwanda, tunaanzisha viwanda vipya na kukaribisha wawekezaji waje kuwekeza, lakini hapa naomba nitoe ushauri.
Naomba niishauri Serikali kwamba isijitoe katika suala zima la uwekezaji wa viwanda na naomba Serikali isitegemee wawekezaji kutoka nje peke yao. Ni lazima Serikali ijipange kuhakikisha tunawawezesha Watanzania wa kati, wafanyabishara wadogo na wafanyabiashara wakubwa ili wawe na uwezo wa kujenga viwanda hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo viwanda peke yake, ni pamoja na kilimo na hasa Mwenyekiti hapa ninaposisitiza, uchumi wetu hauwezi kukua kama kilimo chetu bado ni cha kutegemea mvua. Nahimiza twende na kilimo cha umwagiliaji na tuongeze wigo, badala ya kutegemea mikoa ya Nyanda za Kaskazini ndiyo zilishe nchi nzima, hebu tuangalie na Kanda ya Ziwa iliyozungukwa na mito na maziwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuangalie mikoa ya Kanda ya Kati ambayo bahati mbaya ni mikoa kame, kuna Mkoa wa Tabora, Singida, Dodoma ambapo sasa hivi mvua zinanyesha mpaka tunakosa pa kupita, lakini Mkoa wa Dodoma kila siku wanalia njaa na tunategemea Mkoa wa Ruvuma na Rukwa. Naiomba Serikali iipe sekta ya kilimo fursa ya pekee na katika bajeti inayokuja tuipe nafasi inayostahili, tuipe fedha ya kutosha ili sekta ya kilimo iweze kuleta tija. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri ili tuweze kufikia malengo tunayokusudia, ni lazima tujielekeze katika suala la uvuvi na tujielekeze katika kuvua katika kina cha bahari kuu. Tujenge Bandari na hasa hiyo ya Bagamoyo na Bandari zingine. Kama hatutaweza kwenda kuvua kwenye kina cha maji marefu, tukaifanya sekta ya uvuvi kama ni sekta ya uzalishaji ya kiuchumi, Mpango wetu utabaki kuwa kwenye makaratasi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri pia, hebu watumie ushauri aliotoa Mwenyekiti Chenge na timu yake wakati ule wa bajeti, Waziri wa Fedha, achukue ushauri ule, ni ushauri mzuri sana, kuna mambo mengi sana yapo mle, hebu angalieni vyanzo vipya ili uchumi wa nchi yetu uweze kukua na tuweze kupiga hatua mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe sana Serikali yetu, pamoja na mipango mizuri iliyowekwa hapa, lakini tujielekeze katika kuwawezesha wanawake kiuchumi. Nimefurahishwa na Mpango uliopo wa kupeleka milioni 50 katika kila kijiji na mtaa, naomba katika mpango unaokuja, lazima tuweke mfumo, hizi milioni 50 zitafikaje katika kila kijijiā€¦
MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Mwenyekiti naunga mkono hoja.