Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ninakushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia katika mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita moja kwa moja katika ushauri kwa Serikali. Jambo la kwanza ambalo ninafikiri nitumie nafasi yangu ya uwakilishi kuishauri Serikali ni katika ongezeko la mahitaji ya matumizi katika fedha tunazozipata kutokana na deni la ndani na nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, itakumbukwa kwamba katika kipindi cha mwaka ulioisha 2015/2016 matumizi makubwa ya deni la nje na ndani la Taifa yalielekezwa katika sekta za nishati, barabara, madaraja na viwanja vya ndege. Nataka nimshauri kwa dhati kabisa Waziri wa Fedha, tunakopa fedha kutoka nje na ndani kwa lengo la kwenda kuwekeza kwenye sekta ambazo kimsingi hazina uhusiano wa moja kwa moja katika ku-stimulate ukuaji wa uchumi, kuna tatizo. Ninatoa mfano, tunakopa fedha kutoka katika taasisi za kifedha za ndani na za nje ya nchi, tunajua sote kwa pamoja asilimia 80 ya Watanzania ni wakulima. Hivi ndugu zangu katika fikra tu za kawaida, nimeshawahi kuwa Mkuu wa Wilaya pale Igunga, katika vitu ambavyo lazima Waziri wa Kilimo na Waziri wa Fedha mfanye kazi kwa coordination. Ndugu zangu ukiangalia miradi tuliyonayo kama nchi, miradi mikubwa ya schemes of irrigation ni miradi ambayo ilijengwa na muasisi wa hili Taifa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema kwamba nchi tunataka tuwasaidie wakulima ambao ni asilimia 80 ya Watanzania, hivi tunaachaje kwenda kukopa fedha na kwenda kuwekeza kwenye miradi ya kuwasaidia wakulima kufunga irrigation schemes? Nina mfano mmoja na Mheshimiwa Dalaly Kafumu utaniunga mkono.
Nilipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga, tuna mto unaitwa Mto wa Mbutu kipindi cha mvua mto huu kuna maji ambayo ukienda kuyaangalia yanayotiririka na kupotea na chini ya Igunga kuna eneo la karibu mpakani mwa Singida na Igunga eneo ambalo ni fertile kwa ajili ya shughuli za kilimo. Tumepiga kelele tukiwa pale kwamba utengenezwe mkakati ifunguliwe irrigation scheme kubwa ajili ya kuongeza tija katika uzalishaji wa kilimo cha mpunga Igunga mpaka leo imekuwa hadithi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nataka nitoe ushauri, tunapokopa fedha kutoka katika Taasisi za ndani na nje, pelekeni fedha hizi kwenye miradi ambayo itakwenda ku-stimulate ukuaji wa uchumi na kumgusa mwananchi moja kwa moja kilimo kikiwa cha kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya pili, tunazungumzia habari ya ku-industrialise nchi, how do we industrialise nchi wakati vocational education hakuna mipango yoyote ya kusaidia kwenye vocational education hapa? Nilitarajia Waziri wa Elimu kwa kushirikiana na Waziri wa Fedha kuwepo na coordination ya kuhakikisha ya kwamba tunapojiandaa nchi kui-industrialise lazima tuwaandae watoto wa Kitanzania kuwa na uwezo na ujuzi wa kufanya kazi kwenye viwanda tunavyotaka kuvijenga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano, ninawapongeza watu wa NSSF nimeona wameifungua National Milling, ninaona wanaelekea kujenga Kiwanda cha Sukari ambacho wanasema kinakwenda kuajiri watu zaidi ya laki moja, nani tumeshaanza kuwaandaa watoto wa Kitanzania ndani ya miaka tatu kitakwenda kusimama, tumefanya mikakati gani kuwandaa watoto wa Kitanzania kuwa na vocational skills ya kwenda kifanya kazi kwenye viwanda hivi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu niwashauri Mawaziri kwa nia njema Mawaziri wa Serikali yangu, Mawaziri wa Serikali inayotokana na chama changu, niwashauri. Ninawaomba ndugu zangu, mambo mengine hebu tuwe na creative sisi wenyewe tuwe na creativity, kwa mfano, hata suala hili la kumaliza tatizo la madawati tulisubiri mpaka Rais atoe tamko, lakini hivi leo tunaposema nchi tunataka iwe nchi ya viwanda hivi tunajua kwamba tuna walimu wetu mpaka leo hawana nyumba za kuishi? Hivi kwa nini asitokee Waziri mmoja aseme ninaweka mikakati ndani ya kipindi cha miaka mitatu hakuna mwalimu atalala nje, hakuna mwalimu atakwenda kukaa kwenye nyumba ya kupanga linashindikana hilo? Mambo haya tukiweza kuyafanya ndugu zangu tutajenga base ya kuhakikisha kwamba elimu inayotolewa itakuwa ni elimu itakayoendana na zama hizi tunazozungumza, zama za viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wa pili, kudorora kwa uchumi. Ninaishauri Serikali yangu kwa nia njema, hakuna shaka kwamba kuna viashiria na dalili kwamba uchumi wa nchi yetu to some extent kuna mdororo. Ninatoa ushauri kwa kaka yangu Mheshimiwa Mpango, Mheshimiwa Mpango ninakujua nimefanyakazi na wewe nikiwa Serikalini, ninakujua uzalendo wako haya mambo ya kuteleza hapa na pale tutasaidiana kwa lengo la kulijenga Taifa letu.
Ninakupa ushauri, Mheshimiwa Waziri wa fedha fanyeni kila mnaloweza punguzeni base ya kodi kwa wananchi, kodi zimekuwa nyingi sana. Tume-tax kila maeneo na unapoongeza tax kila eneo definitely lazima utapunguza circulation ya fedha kwenye uchumi. Na ukishapunguza circulation ya fedha kwenye uchumi utakwenda kuathiri masuala mazima ya huduma na uzalishaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri ninaotoa kwa Serikali yangu, kuna fedha mlizichukua za mashirika na taasisi mkazipeleka kuziweka kwenye deposit ya Benki Kuu. Watu wa mashirika ya umma, NSSF na mashirika mengine walikuwa wakipata riba kutoka kwenye mabenki kwa hizo deposit. Ninawashauri Waziri wangu rudisheni fedha hizi kwenye mabenki, yaiteni mabenki myape maelekezo yapunguze riba ya mikopo kutoka asilimia 18 mpaka 13 mtakuwa mmeongeza wigo wa Watanzania kukopa na mtakuwa mmesaidia middle class katika business hapo tutakuwa tunajenga uchumi wa nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna theory inasema kwamba kiuchumi, mahali popote unapotaka ku-stimulate uchumi wa nchi kwa lengo la kukuza wafanyabiashara wa kati, ukifanya kitu kinaitwa kupunguza pesa kutoa pesa kwenye mzunguko katika uchumi maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba watu wanapokuwa hawana fedha kwenye uchumi inakwenda kuathiri hata shughuli za uzalishaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninatoa ushauri tusi-ignore suala la kusema kwamba pesa hakuna mtaani tukaishia kusema kwamba watu wanapiga dili, hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuende extra miles na tutumie wachumi wa Taifa hili tulionao wafanye tafiti, watuambie Tanzania kwa uchumi tulionao ni fedha kiasi gani zinahitajika ziwepo kwenye circulation na watupe majibu ni fedha kiasi gani sasa hivi kwenye circulation hazipo, ziko wapi ili kusudi tuweze kuwa na remedy katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nizungumzie suala zima la sera za kifedha (monetary and fiscal policy). Ukiamua kujenga uchumi ambao utaleta ushirikishwaji wa wananchi lazima tuhakikishe ya kwamba uwepo wa fedha nyingi kwenye mzunguko. Inawezekana labda Waziri wa Fedha waliamua kubana fedha kwenye mzunguko kwa lengo la ku-control inflation kwenye nchi kwa maana ya kwamba bei zinakuwa juu na fedha inakisa thamani. Lakini nataka nikwambie kitu kimoja, bado tunaweza kulifanya hili kwa kuziagiza commercial banks zikaweka riba kubwa kwa watu wanaweka deposit. Watu watapeleka fedha kwenye mabenki lakini pia tukaziambia benki zikashusha riba ya mikopo kwa wafanyabisahara wa kati na wakubwa tuta-encourage private sector kuchukua mikopo na ku-invest. Tunaposema tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda tukiacha hali iendelee namna hii kuna hatari kubwa ya Serikali kukwama na kuna hatari kubwa ya nchi kukwama kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia jambo lingine ninalotaka kushauri kwa nia njema kabisa kuna mambo tumekuwa tukiyazungumza hapa kwa muda mrefu. Ninawashauri Mawaziri wangu wanaotokana na chama changu kilichoko madarakani kwa nia njema tunaomba sana Mawaziri wasiwe wanasubiri mpaka matukio ndiyo waweze kuchukua hatua kwa mfano, mwaka jana kipindi tunafungua Bunge la mwezi wa 11, nilikuja na kilio juu ya usumbufu wa ndege wanaokula mazao ya wakulima maskini watu wasio na kipato. Tunazungumza hapa Mheshimiwa Waziri, leo ninapozungumza Singida ndiyo Mkoa tuna-lead katika production ya sunflower lakini leo ninavyozungumza asilimia 70 ya sunflower iliyolimwa kwenye jimbo langu ililiwa na ndege wanaitwa silingwa na mpaka sasa hivi tunavyozungumza nina imani hata Waziri usikute wanasubiri msimu ufike tuanze kupiga kelele tena Bungeni hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba mtimize majukumu yenu kwa lengo la kumsaidia Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Sina mashaka na uzalendo wa Dkt. Magufuli, sina mashaka na uzalendo wa huyu Rais katika kutetea na kupigania maslahi ya Taifa hili lakini inawezekana kabisa kuna baadhi ya wasaidizi kwa makusudi yao wameamua kumkwamisha Rais wetu whether kwa kuogopa kumshauri vizuri. (Makofi/vigelele)
Kwa hiyo, ninatoa ushauri tusisubiri mpaka mambo yaharibike ndiyo tuje kwa ajili ya kuanza kupiga kelele. Wakulima wetu wanahitaji kuiona Serikali yetu iko proactive na kushughulikia matatizo na changamoto zao kabla athari hazijaonekana. (Makofi/vigelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sekta ya elimu, ni wazi kwamba Mheshimiwa Rais Dkt. John pombe Magufuli alipokuja na sera ya elimu bure, niitumie fursa hii kuipongeza sana Wizara ya elimu na kumpongeza Rais japokuwa changamoto ni nyingi lakini ninauona moyo wa kizalendo wa Rais wetu katika kulitetea suala zima la sekta ya elimu. Changamoto tuliyonayo na alizungumza kaka yangu Mheshimiwa Heche, alizungumza leo asubuhi, tumeongeza idadi ya enrolment. Mimi kwenye jimbo langu peke yake asilimia ya wanafunzi walioongezeka kwenye udahili ni asilimia 17.8 kwenye jimbo langu lakini ndugu zangu tunauhaba wa vyumba vya madarasa, hivi ndugu zangu hili nalo tunasubiri mpaka Rais atoke atoe declaration kwamba muanze vyumba vya madarasa? Kwa nini tusiweke mipango mikakati tuseme ndani ya kipindi cha miaka miwili tatizo la changamoto la uhaba wa vyumba vya madarasa litakuwa limetatuliwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatoa changamoto kwa Mawaziri, ninatoa changamoto kwa Baraza langu la Mawaziri, nendeni mkakae mjifungie pelekeni proposal Dkt. Magufuli ni Rais msikivu suala la madawati nililizungumza mimi hapa Bunge la kwanza ndiyo nilikuwa Mbunge wa kwanza kulizungumza na alipokuja Singida sisi tulionyesha mfano na chama…(Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante.