Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu ambae ametupa uhai na akatufanya sisi leo kuwa miongoni mwa Wabunge ambao tutachangia maslahi ya nchi hii katika mipango ya kuendesha nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Ni nafasi adhimu ya kuweza kuchangia Mpango wa Maendeleo au Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nizungumze kitu kimoja kidogo ambacho wasemaji wengi sana walikuwa wanakigusagusa ambalo linahusiana na masuala ya bandari.
Kwanza nakwenda huko moja kwa moja masuala ya bandari, ni kweli tumeona kwamba mzigo katika bandari umepungua lakini tunaposhauri tujaribu kuangalia katika maeneo ambayo mzigo maeneo gani yamepungua. Ukitizama katika hizi transit goods ambazo zinakwenda katika nchi jirani basi utagundua kwamba nchi ya Zambia na DRC Congo ndipo mzigo ulikopungua, lakini ukiangalia Uganda na Malawi mzigo haujapungua. Sababu zimeleezwa na wengi pengine labda VAT na pengine labda hiyo single custom territory ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kufanya mizigo katika bandari ipungue.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika hili nilikuwa naomba Serikali ijaribu kuangalia hivyo vitu ambavyo vimetajwa hapo kwamba ni sababu na tujielekeze na tubaini kwamba hiyo kweli ni sababu; kwa sababu kuna baadhi ya mambo yalianza kabla ya hapo. Tukija katika hiyo single custom territory kwamba ilikuwa iko toka mwaka 2013 ikaanza kuwa implemented Disemba, 2014 sasa tutizame kitu gani kilichotuathiri. Na ukija kutazama katika mizigo mingine hususani ya mafuta mpaka katika nchi za Rwanda na Burundi kwa mujibu wa takwimu ambazo zimo katika kitabu cha bandari kwamba nayo pia ilipungua. Lakini ukiangalia katika nchi nyingine zimeongezeka sasa hili nilikuwa naomba tutafute sababu hasa ili tunapotibu basi tujue tunatibu kitu gani ambacho mahususi moja kwa moja kitakuwa kinatusaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ninataka kulizungumzia amelizungumzia Mheshimiwa Kingu pale kwamba kuhusiana na fedha ambazo zimo katika uchumi wetu. Tunafahamu Serikali imepanga kukopa ndani, lakini moja katika changamoto ambayo Serikali yenyewe ilieleza kwamba kutoshiriki kwa sekta binafsi katika uchumi imefanya kwamba uchumi kutokukua vizuri au mambo kutokwenda sawa.
Sasa tunapoamua kukopa ndani vilevile tutasababisha hali hiyo hiyo ya kwamba fedha zitakuwa hazipatikani kwa wananchi na baadaye hawa watu binafsi hawataweza kukopa, kwa hiyo na sekta binafsi nayo itarudi katika changamoto yake ile ile ya kwamba itaanguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naishauri Serikali iharakishe suala la kupata ile dhamana ya Kimataifa kukopa kuweza kufanya sovereign rating kwa haraka ili tuweze kupata mikopo ya nje. Lakini pia si vibaya kwakuwa soko letu la hisa la Dar es Salaam Stock Exchange linakubali kualika foreign investors ambao labda Serikali nayo ijielekeze katika kukopa kwa foreign investors ingawaje changamoto zake zinajulikana kwamba ufanisi katika soko lile pamoja na vitendea kazi siyo vizuri kwa muda huu, lakini tutakapotumia njia hiyo, kwa hiyo, tutaweza kupunguza kukopa ndani na baadaye tutajielekeza katika masuala mengine ambayo ya mikopo mizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ni muhimu sana ambalo wengi walilizungumzia, Serikali ingeweka utaratibu uliowazi kufahamu shughuli zinazofanyika. Wengi wanaozungumza hapa wanalalamikia utaratibu wa Serikali kutofikisha fedha katika masuala ya dawa, katika Halmashauri na sehemu nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa mujibu wa report ya BOT ambayo wameleeza kwamba katika mwezi wa Agost, Serikali ililipa zaidi ya shilingi bilioni 900 ili kulipia Deni la Taifa. Katika mwezi wa nyuma yake Serikali iliipa hizo report zimo katika mawasilisho ambayo yalifanywa na Gavana wa Benki Kuu tarehe 25 Agosti. Kwa hiyo, hii ndiyo imepelekea kwamba Serikali kutopata fedha za kutosha katika kuhudumia masuala mengine sasa hapa ikafikia kipindi ambacho watu wakaanza kuisema Serikali vibaya na hapa na mimi ninaomba kidogo niongee neno moja ingawa kwamba kwa wengine itakuwa siyo zuri lakini neno lenyewe ni muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu ambaye yupo hai akatafuta kurehemewa na maiti. Narudia tena, mtu ambaye yupo hai hawezi kutafuta rehema kwa aliyefariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu hapa alizungumza kwamba hii Serikali imefilisika lakini akasahau Serikali hii ndiyo iliyompa yeye majengo bila kulipa akawa anafanya biashara. Sasa kama mfu ndiyo wewe unamtegemea akurehemu, sasa wewe mwenyewe ni mfu zaidi ikiwa aliyekufadhili amefilisika ina maana kwamba wewe uliyefadhiliwa umefilisika zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna msemo wa kiswahili ambao una lafudhi ya Kiarabu ambao unasema wafadhilaka wasajidaka, man-fadhilaka wasajidaka, aliyekufadhili ni bwana wako na sio pundaka; sio punda wako. Kwa hiyo, Serikali bado atabakia bwana wake huyo ambaye amefadhiliwa na Serikali hii, kwa hiyo, Serikali haijafilisika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ni muhimu nazungumza masuala ya retention ambayo pia yameshazungumzwa. Nakumbuka moja ya hoja ambayo Serikali ikaamua kufuta retention kwa taasisi zile ambazo zimefutiwa retention kwa sababu Serikali ilikuwa ikikopa pesa zake wenyewe. Zile taasisi zilikuwa zikiweka pesa benki baadaye Serikali inapopeleka dhamana zake kuuza katika masoko ya hisa, mabenki haya yananunua ambayo ni fedha za taasisi za hii Serikali, kwa hiyo ikaamua kuzitoa kuziweka huku. Sasa ufanyike utaratibu ambao uko mzuri na muafaka ili iweze kupatikana urahisi zaidi kwa fedha hizi kuingia katika mzunguko au Serikali yenyewe kama iliona taabu kukopeshwa na mabenki katika retention ambayo ziko BOT sasa je, Serikali ina mpango gani kuzitumia hizi? Labda pengine nazo zinaweza zikasaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na suala moja ambalo ni muhimu sana ni lazima tuangalie balance ya monetary policy na fiscal policy tunajua Wizara ya Fedha inashughulikia masuala ya fiscal policy, lakini Benki Kuu inashughulikia monetary policy.
Kwa hiyo, vitu hivi viwili ni lazima viwe balanced ili mambo yaweze kwenda sawa na tuweze kuepukana na mambo ambayo hayaendi vizuri. Kuna watu walisifu hapa kwamba Serikali iliyopita ya Mheshimiwa Mwinyi ilikuwa nzuri, ya Mheshimiwa Mkapa ilikuwa nzuri, ya Mheshimiwa Jakaya ilikuwa nzuri na hii pia ninaamini wataisifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mshairi mmoja anasema mpende bado yuko hai, pendo lako alipokee, ukimpenda yuko kaburini umelitupa pendo lako hewani, hayo mapenzi yenu mliyoyataja hapa mmeyatupa hewani lakini tunaamini kwamba na huyu mtampenda. (Makofi)
Sasa jambo lingine ambalo ni muhimu na kama tutalifanyia kazi itakuwa vizuri. Mheshimiwa Khatib pale alizungumza jana kitu kizuri kidogo hata kile kitu nimekipenda. Anasema kwamba alikiombea dua chama chake na akasema kwamba kuna watu wanakiombea kife, hawakiombei kife, mfano wa mtu ambaye ananyeshewa na mvua, tuseme unanyeshewa na mvua baadaye akatokezea mtu akakwambia njoo ujifiche kwenye jeneza unakufa, unajiua? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo,niongee masuala mawili ambayo muhimu. Katika…
MWENYEKITI: Ahsante.