Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia Mpango huu muhimu wa leo. Kwanza kabisa nichukue fursa hii kuwashukuru Wabunge wenzangu wa CHADEMA kwa kuniamini na kunichagua kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na nawaahidi sitawaangusha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukisaidiana hapa Bungeni na nimepata taarifa kuna karatasi zinatembea hapa upande mwingine wa kumchangia mpiga kura wangu Mzee Wassira na mimi Mbunge wake naombeni pia nishiriki kumchangia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, sasa naomba niende kuzungumzia Mpango…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Tunapopanga mipango kama Taifa lazima tupange maeneo yanayogusa watu wengi na katika Taifa letu maeneo yanayogusa watu wengi ni sekta ya kilimo, takribani asilimia 80 ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda wa miaka mitatu mfululizo tumekuwa tukipanga trilioni 2.7 kwenda katika sekta ya kilimo, lakini zikatengwa bilioni 371, zilizotoka milioni 250 sawa na asilimia tisa, sasa kama tunapanga kutoka trilioni 2.7 kwenye sekta inayoajiri watu wengi tunatoa asilimia tisa tuna dhamira ya dhati ya kumkomboa Mtanzania! Haya ndiyo mambo ya msingi Wabunge wenzangu tujiulize na hasa sisi tunaotoka Majimbo ya Vijijini ambayo yanaitwa Mjini leo hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipanga hapa huko kwenye sekta ya kilimo tufikie asilimia 10 hatukufika, tukapunguza asilimia sita hatukufika, ikawa asilimia 3.2, leo kwenye sekta ya kilimo iko asilimia 2.3, tunaenda mbele tunarudi nyuma. Tuna mpango kweli wa kuhakikisha hii sekta inaondoa umaskini katika Taifa letu! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka mitatu mfululizo asilimia tisa kwenye sekta inayowaajiri watu wengi, halafu tukija kuongea hapa watu tunapiga bla bla! Please Mheshimiwa Mpango naomba apange na atekeleze kama kazi yake ni kupanga ajifunze na kutekeleza ili haya mambo yaende katika hii sekta nyeti, Watanzania wanufaike nayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimeangalia katika mipango mbalimbali, Serikali kupitia Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, hapa naongea kama Waziri Kivuli, inadaiwa trilioni saba, kwenye hii mipango sijaona mkilipa. Trilioni sita ziko PSPF, Mfuko ambao hali ni hohehahe, tukisema Serikali mtachangia kwenda kufilisi Mfuko huu, mtajibu nini? Miongoni mwa fedha hizo ni fedha za mikopo takribani miaka 10 hamjalipa, lakini hamna mpango wa kulipa. Serikali inadaiwa mbele, inadaiwa nyuma, inadaiwa kushoto, inadaiwa kulia, lini sasa haya mambo yatakwisha? Hakuna humu katika mpango, jamani hii Mifuko tunatambua kuna mambo ya msingi ambayo inachangia, lakini tunahitaji hii Mifuko isaidie wanachama wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inadaiwa trilioni sita katika Mfuko mmoja ambao tumeambiwa unakaribia kufilisika, huna mpango wa kuonesha unaanza kulipa lini na ni deni la muda mrefu, tunajua deni lingine mlilirithi kwa watu ambao walikuwa hawajaanza kuchangia. Sasa haya mambo lazima tuoneshe kuna mikakati dhahiri ya kulipa, ndiyo kwanza mnapanga kukopa tena, tena ndani trilioni 6.8 wakati tunajua mkiendelea kukopa ndani mzunguko wa fedha unakuwa finyu. Hali ya umaskini ni kubwa wananchi ni hohehahe, uchumi umeshuka, huko kitaa hali ngumu, Wabunge hali ngumu, kila mtu kapauka tu, pesa hakuna. Haya lazima tuyaseme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha hili naomba nimwambie ukweli, duniani kote kama Waziri wa Fedha hakuwa stable nchi inayumba, hatuhitaji Taifa letu liyumbe. Tunaomba mipango inayopangwa itekelezwe kwa maslahi ya Taifa letu, ni jambo la msingi sana. Leo hii tunazungumzia masuala ya viwanda lakini ukiangalia huku hakuna connection yoyote kati ya sekta ya kilimo, sekta ya viwanda pamoja na Wizara ya Elimu na Wizara ya Mafunzo na Ufundi, hivi vitu vinakwenda sambamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwaambia kwenye bajeti tulijua basi leo mngeleta katika Mpango, hakuna. Tukitoka mnasema, tukibaki tukiwashauri mnasema, mnataka nini sasa? Chukueni basi hata haya mazuri maana unajiuliza haya hatukuwepo uchumi umekua! Mikutano ya hadhara mmezuia uchumi umekua! Mmetufukuza Bungeni uchumi umekua! Kwenye mipango mmeshindwa kupanga sawasawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Bunge, kama Taifa tunaomba tuweke maslahi ya Taifa mbele tusijiwekee sisi kulinda nafsi zetu wenyewe, tumshauri Mheshimiwa Rais vizuri. Hali ya uchumi haiko vizuri, bandarini kumekauka kila sehemu kumekauka. Tuliongea katika briefing hapa, leo hii Bunge ni aibu ukiangalia kule majani ile green yote imekauka sasa hivi shida kila kona, wananchi wana njaa, Wabunge wana njaa, kila sehemu kuna njaa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunamwambia Mheshimiwa Mpango apange na kutekeleza, huko kwenye Halmashauri ndiyo kabisa, yeye asipopanga vizuri, asipotekeleza Wizara zingine na zenyewe hali yake ni ngumu. Kwenye Halmashauri zetu mpaka leo fedha hazijafika, kwangu pale Bunda Mjini kwa sababu nimeamua kuongoza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunda Mjini hata photocopy tu wanakuja kutoa kwenye ofisi ya Mbunge kwa sababu nimeamua kuongoza. Ahsante.