Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, naomba nikushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili pia niweze kuendelea kutoa michango yangu katika Bunge lako Tukufu. Pia naendelea kumshukuru Mungu kwa sababu ameendelea kunipigania na kuendelea kutoa michango yangu katika Bunge hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoanza kuchangia Mpango huu wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2017/2018 nitapenda sana niwapitishe katika kitabu hiki kwa kutumia pages. Kwanza kabisa, naomba tuangalie ukurasa wa pili wa Mpango huu wa Maendeleo ya Taifa, kifungu cha 1.4 kinazungumzia utaratibu wa kuandaa Mapendekezo ya Mpango. Katika utaratibu wa kuandaa Mapendekezo ya Mpango umeangalia mambo mbalimbali ikiwemo hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa wakati anafungua Bunge la Kumi na Moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Rais anafungua Bunge hili la Kumi na Moja wote tulimsikiliza kwa makini. Mheshimiwa Rais aliongea vizuri sana na hotuba yake ilikuwa inalenga katika kuwakomboa wananchi wa Tanzania. Mheshimiwa Rais aliongea mambo mengi sana na moja ya jambo ambalo alisisitiza ni viwanda. Mheshimiwa Rais alisisitiza kwamba anataka Tanzania iwe ya viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimepitia mpango huu vizuri sana, ukiangalia viwanda vimeongelewa kwa kuguswaguswa, nasikitika sana kusema hilo. Kwa maana kwamba mpango haujajikita katika kusema waziwazi kwamba ni viwanda gani ambavyo sasa vinaenda kuangaliwa na mpango huu. Hivyo basi, napata wasiwasi kama kweli sisi tuko tayari kufuata ushauri ambao Mheshimiwa Rais alikuwa akiuongea? Aliongea katika kampeni zake, aliongea katika kulifungua Bunge hili na mpaka sasa bado Mheshimiwa Rais anaendelea kuongea na kusisitiza kuhusiana na suala zima la viwanda, napata wasiwasi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, kwamba anapotuletea mpango mwezi Mei nadhani baada ya kuchukua mapendekezo yetu Waheshimiwa Wabunge, namsihi sana katika mpango wake atuelezee ni viwanda gani hasa ambavyo anaenda kuviweka katika mpango wake. Vivyo hivyo atakapokuja kutenga bajeti atenge bajeti ambayo kweli ita-reflect kwamba sasa Tanzania inaenda kuwa Tanzania ya viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la maji. Hatutaweza kuwa na viwanda nchini Tanzania na hatutaweza kamwe kufikia malengo ya Mheshimiwa Rais ambayo ni malengo mazuri sana kama haitakuwa Tanzania ambayo wananchi wa kawaida, mwananchi aliyeko kijijini anaweza akapata maji wakati wowote atakapoyahitaji. Nasema hivi kwa sababu gani? Maji ni kiungo kikubwa sana kwani yanaweza yakasaidia katika kilimo. Ukiangalia sasa hivi naweza nikasema nchi hii inaelekea kwenye jangwa kwa sababu hakuna maji kabisa. Nchi imekuwa na ukame na hata watu wa Idara ya Hali ya Hewa pia wametabiri kwamba sasa hivi hakutakuwa na mvua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kule kwetu Mwanza kuna kilimo cha pamba na mazao mengine mbalimbali lakini wananchi wanashindwa kulima kwa sababu ya ukosefu wa maji. Hata hivyo, ukiangalia katika mpango huu, kama ninavyosema na nitarudia kusema maji yanatajwa tu kwamba maji, maji yanafanya nini? Tuna mikakati gani kwamba maji sasa yanaenda kupatikana Tanzania? Namwomba sana Mheshimiwa Waziri wa Mipango atakapoleta mpango atuletee mpango mkakati kwamba anaenda kufanya nini ili kuhakikisha kwamba Tanzania inaenda kuwa na maji? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo kuna suala pia la irrigation scheme, nimeliona limetajwa humu katika mpango lakini halioneshi dhamira kwamba kweli tunataka kufanya irrigation scheme hapa nchini Tanzania ili kuwezesha kilimo ambacho ndicho kitakachotupeleka kwenye viwanda. Kwa sababu tutakapoanzisha viwanda tunatarajia kuwa na raw materials, tunaenda kupata wapi hizi raw materials kama hatutaweza kuimarisha kilimo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena niongelee suala kubwa sana ambalo Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, ameliongelea wakati wa kampeni zake. Wakati wa kampeni zake akifanya ufunguzi pale Jangwani aliongea kwa ari kubwa sana na alikuwa anamaanisha. Najua anamaanisha kwa sababu niliona jinsi alivyoongea. Hakuna mtu aliyemtuma kuongea, alijituma mwenyewe kwa sababu anao uchungu na anayo nia ya kuwasaidia Watanzania ili waondokane na umaskini. Mheshimiwa Rais alisema kwamba atahakikisha Serikali yake inatoa milioni 50 katika kila kijiji, hii ni katika kuwawezesha Watanzania kuondokana na umaskini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunapitisha bajeti hapa niliongea kwa uchungu sana kuhusiana na suala la milioni 50. Nashukuru kwamba Serikali ilisikiliza na ikaongeza pesa kidogo hadi kufikia kutenga bajeti ya shilingi bilioni 49. Hata hivyo wakati nikichangia katika bajeti iliyopita nilisema kwamba shilingi bilioni 49 ambazo zimetengwa bado hazitoshi. Tuna vijiji 13,000 hizi hela ambazo zimetengwa bado ni ndogo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, natambua juhudi za Serikali, natambua juhudi ambazo Mheshimiwa Waziri wa Fedha anazifanya kuhusiana na suala la kutimiza ahadi ya Rais ya milioni 50, ili kuweza kuwakomboa Watanzania kutokana na umaskini, namwomba na ninamsihi sana katika mpango wake ajaribu kuelezea ni vijiji vingapi ambavyo vitaweza kupata hii shilingi milioni 50. Atuoneshe na atuelezee wazi kwa sababu tunapata kigugumizi tunapozunguka kwenye Majimbo yetu, wananchi wameandaa vikundi mbalimbali wamevi-register, wako kamili wanasubiri milioni 50 ya Mheshimiwa Rais, lakini sasa kama hatutataja kwenye mpango wananchi tutawaambia nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha atakapoleta mpango uwe umejumuisha ni vijiji vingapi, vitapata shilingi ngapi, ni mkoa gani kwa Tanzania nzima? Hivyo vijiji avitaje ili tuweze kufahamu kwamba sasa mimi Mkoa wangu wa Mwanza vijiji kadhaa vitapata na Mkoa wa Tanga vijiji kadhaa vitapata. Naomba sana kuishauri Serikali kuhusu hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongelea suala la afya. Juzi nilisimama hapa kwa uchungu mkubwa sana na nikasema kuhusiana na suala la dawa. Kumekuwa na upungufu wa dawa na hata Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu alikiri kuwepo kwa upungufu wa dawa. Tumekuwa tukiilaumu Wizara ya Afya ambapo sasa hivi naomba kabisa niombe radhi kwa Wizara ya Afya kwa sababu naamini kabisa nimewakosea kuwaonea nilitakiwa nimlaumu Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kwa sababu yeye ndiye ambaye anahusika na suala zima la kutenga fedha kwa ajili ya dawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri wa Mipango atakapoleta Mpango katika Bunge hili, atuoneshe wazi kwamba sasa ni fedha kiasi gani au ni mikakati gani aliyonayo ya kuhakikisha dawa zinapatikana Tanzania nzima ili akinamama wasiteseke. Akinamama ambao wanateseka ni wajawazito wanakwenda kwenye hospitali wanaishia kupimwa ujauzito tu basi, kuangalia vipimo kwamba mimba imefikia katika hatua gani lakini dawa hakuna! Inapotokea anapata tatizo lolote mama huyu anaandikiwa dawa anaambiwa nenda kanunue kwenye pharmacy, pesa hana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunayo nia ya kuwasaidia Watanzania namsihi sana…
Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wangu nadhani bado upo, dakika 15?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana