Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia Mapendekezo ya Mpango huu unaoendelea. Kwanza kabisa, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha pamoja na timu yake yote kwa kutuletea huu mpango mapema zaidi ili tuweze kuufanyia kazi, uboreshwe na baadaye tuweze ku-achieve yale ambayo tunatarajia kuyafanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kumpongeza sana Mheshimiwa wetu Rais wa Awamu hii ya Tano kwa nia njema kabisa ya kutaka kuleta maendeleo ya nchi hii hasa ukiangalia kwamba anataka keki ya Taifa igawanywe kuanzia kwa mwenye kipato cha chini mpaka mwenye kipato cha juu. Kwa hiyo, jitihada nyingi sana anazifanya na tukizingatia kwamba yeye ndiyo mara yake ya kwanza kushika uongozi ni lazima kutatokea changamoto za hapa na pale. Kwa mfano, anapambana na ufisadi, rushwa, wafanyakazi hewa, matumizi mabaya ya Serikali na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotokea sasa hivi kwa mtazamo wangu, watu wanalaumu wanaona kwamba it is a government failure, kwangu mimi sioni kwamba Serikali imeshindwa, ni muda mchache, hapa tupo kwenye transitional period, kwamba kuna reforms nyingi zinafanyika ili tuweze ku-achieve haya ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayataka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika change ya aina yoyote huwa kuna early adapters, slow adapters na late adapters kwamba wapo wale wanaokubali mabadiliko haraka sana na wapo ambao tayari wanampongeza Mheshimiwa Rais, hawa ni wale wanyonge ambao haki zao hazitolewi. Hata hivyo, wapo wale ambao wanakubali taratibu tunawaita slow adapters, hawa wanaangalia kwanza mazingira wajiweke sawa, lakini kuna wale late ambapo yeye anasubiri kwanza mambo yafanikiwe ndiyo aende.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kinachotokea kutokana na change, wale wanaolaumu inawezekana ni katika kundi la wale watu ambao ni mafisadi, wala rushwa ndio wanamkwamisha Mheshimiwa Rais wetu. Kwa hiyo, hawa kwa vyovyote hawawezi kukubali hizi reforms ambazo zimepangwa ili tuweze ku-achieve kwamba sasa keki ya Taifa wafaidi wananchi kuanzia wa kipato cha chini mpaka kipato cha juu. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi anayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni kwamba sasa tumpe support kwa sababu kila utawala mpya lazima utakuwa na changamoto zake. Yeye ni mara yake ya kwanza. Tukianza hata kihistoria Mwalimu Nyerere wakati amepokea utawala kutoka kwa wakoloni alipambana sana kwenye ujamaa na wapo watu ambao walikuwa ving’ang’anizi ndiyo wakatuletea hata huu ujinga ujinga wa structural adjustment ambayo hailingani. Kwa hiyo, alipambana na watu wengine walikataa kwa sababu ya maslahi yao, tuliwaona kina Kambona walikimbilia nje, ndiyo hiyo hiyo ambayo inatokea sasa hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija upande wa Mheshimiwa Mstaafu Rais Mwinyi, watu walimuita ruksa lakini kutokana na mazingira aliyoyakuta wakati ule, bidhaa hamna akafungulia. Kwa hiyo, ni kama vile tunavyosema kila zama na kitabu chake. Pia ukiangalia wakati wa Mheshimiwa Mkapa watu waliita ukata lakini mwaka wa kwanza aliyumba baadaye mambo yakaenda, vizuri sasa hivi tunamkumbuka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija upande huu wa Mheshimiwa Rais wetu aliyestaafu juzi, Rais Kikwete, wengi wakasema labda mpole lakini alifanya mambo makubwa lakini mwanzoni alivyoanza watu wakaona haendi. Sasa na hii Awamu ya Tano, hizi reforms jamani nani anayetaka ufisadi uendelee au rushwa iendelee, wafanyakazi hewa, tunapoteza fedha bure, ndiyo hiki kinachofanyika. Kwa hiyo, tumpe support Mheshimiwa Rais wetu afanye kazi na sisi Watanzania ndiyo tunaotakiwa tumuunge mkono badala ya kumbeza na kuibeza Serikali. Nafikiri hii siyo vizuri kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande sasa wa mpango, naomba nichangie kuhusu viwanda. Sera ya viwanda ni nzuri lakini tuangalie, je, Tanzania sasa hivi tunataka viwanda vya aina ngani? Kwa sababu sasa hivi tukumbuke tuko kwenye utandawazi, ni free market, tusije tukatengeneza kiwanda ambacho tunategemea labda soko la ndani tuko karibu milioni 50 labda consumers ni milioni 20, kwa hiyo soko la ndani halitoshelezi. Tufanye utafiti na soko la nje, siyo kwamba viwanda ili mradi viwanda. Nia ya viwanda ni kuajiri watu wengi mbali ya production, kwa hiyo, tuhakikishe tunaanzisha viwanda vile ambavyo vitawalenga hawa watu wetu wa chini waweze kupata ajira hasa vijana wetu wanaomaliza vyuo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kuna hili suala la kodi na tozo nyingi. Niungane na wenzangu, jamani sasa wasi-take advantage ya Serikali kukusanya kodi, kufanya mauzauza huko kuiharibia Serikali na ndiyo kinachofanyika sasa hivi. Kwa hiyo, tunaomba sana Waziri aliangalie suala hili, zile kodi na tozo ambazo ni kero kwa wananchi ziondolewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ukienda kwenye mabenki kwa mfano CRDB, jamani ukitaka statement ya karatasi moja ni Sh.11,000/= hivi kweli! Ile si ni ku-print out tu kwa nini wasitoze hela kidogo lakini sasa watu wanatengeneza business. Sasa hivi ukitumia ile mashine ya CRDB labda umeenda kununua kitu wanakata asilimia tano ya value ya kile kitu ulichonunua. Kama ni shilingi milioni tatu asilimia tano ya milioni tatu inakatwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni wizi kwa sababu wewe ni mteja wao lazima wakupe hizo fursa, wachukue hata elfu moja kama vile unavyochukua kwenye ATM, kwa hiyo hizi ni kero. Hata parking fee hizi za magari jamani kwa siku mtu akipaki Sh.1,000x30 ni Sh. 30,000, Sh. 30,000x12 ni Sh. 360,000 hiyo ni mbali na tax nyingine ambazo tunalipa. Kwa hiyo, kodi kama hizi ziangaliwe either zitolewe au zipunguzwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ni emphasize kwenye maendeleo vijijini, hii ni area yangu maendeleo vijijini. Huwezi ukawa na uchumi wa kati bila ya kuwa-empower hawa watu wa vijijini. Kwa hiyo, naomba miradi ya maendeleo ile iliyoachwa 2014/2015, 2015/2016 ipewe kipaumbele ili ile continuity ya kuleta maendeleo na ile Tanzanian vision iweze kuwa achieved. Tukiiruka ile tukaanza na hii mipya hatutaweza kufika kule, programu zetu zitakwama. Kwa hiyo, ni-emphasis tuangalie vitu ambavyo ni mahitaji ya msingi vijijini kama vile maji, elimu, barabara na masoko kwa ajili ya mazao yao. Tuki-promote hivi naamini kabisa huu uchumi wa viwanda na kipato cha kati utafanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme pia kitu kingine, tusi-undermine human capital, ili tuweze kupata maendeleo lazima tuwekeze kwenye capacity building. Kwa hiyo, hizi semina za ndani na nje ni lazima hawa washiriki kwa sababu kwa dunia hii ya utandawazi ya sasa hivi kuna new technologies, new skills, new approaches concept ili tuweze kuingia kwenye hili soko la dunia na sisi tuweze ku-compete. Otherwise tukiangalia tu miradi tukasahau kwenye human capital itakuwa ni shida sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa kweli naipongeza Serikali, napongeza Mapendekezo ya huu Mpango ambao umeletwa ili tuyafanyie kazi, tuboreshe badala ya kubeza na kudharau, hapana, huu ni mwanzo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha azingatie haya maoni ambayo wachangiaji mbalimbali wanatoa, yale ambayo tunaona kweli yanafaa ili kuboresha huu mpango na hatimaye nchi yetu iweze kufikia maendeleo endelevu ifikapo 2030.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na naunga mkono hoja.