Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha jioni ya leo kuchangia mapendekezo ya mpango yaliyowasilishwa na Waziri wa Fedha.
Awali ya yote nampongeza Waziri wa Fedha, sisi kama Kamati ya Bajeti tulishirikiana nae vizuri katika kujadili mapendekezo haya. Na naenda moja kwa moja kwenye mchango wangu katika suala zima la kufungamanisha maendeleo ya uchumi na rasilimali watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa naomba niipongeze Serikali ya Awamu ya Tano kwa uamuzi wake wa kutoa elimu bure, nikiwaona mamia ya wanafunzi walioongezeka kwenye shule za msingi, sekondari, waliokuwa wanapoteza fursa kutokana na ada na michango mbalimbali na nikiona utayari wa wazazi kuchangia huduma ambazo pengine Serikali haijachangia kwenye ule mchango wa kila mwezi kwa kweli nafarijika. Ndio maana baadhi ya maeneo sisi tumejipanga tunafyatua matofali kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya shule, ujenzi wa madarasa mapya na ndio maana baadhi ya maeneo tumejipanga, tumetengeneza wenyewe madawati pamoja na Waheshimiwa Wabunge acha yale ya kupewa na Bunge. Lakini yapo maeneo tumechangia madawati, tumejenga nyumba za kuhifadhi hayo madawati. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwenye masuala ya kufungamanisha maendeleo ya viwanda na afya. Nichukue fursa hii kuipongeza Serikali pia kwa jitihada mbalimbali za uboreshaji wa afya husasan katika tukio la mkutano wa wafadhili wa Kimataifa juu ya afya ya mama na mtoto. Nampongeza sana Mheshimiwa Ummy pamoja na Wizara yake kwa kufanikishwa kufanikisha kupatikana kwa zaidi ya dola milioni 30 kwa ukarabati wa vituo vya afya mia moja. Ukarabati huo utahusu ujenzi wa theatre, maabara ya kuhifadhi damu, wodi ya wazazi, nyumba moja ya mtumishi. Ninaamini itakuwa ni ukombozi mkubwa na Serikali ya Awamu ya Tano itakuwa imeaanza vizuri. Kwa kuwa tuna vituo 489, vituo 113 ndiyo vyenye fursa hizo ukivijumlisha na vituo hivi mia moja vinabaki vituo 376. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali, natarajia mapendekezo ya mpango huu utakapokuja kuwa kamili na tutakapo kaa Kamati ya Mipango mwezi wa pili, nadhani watakuja na mapango utakaoainisha vituo vilivyosalia namna ya ukarabati na uboreshaji, lakini pia ujenzi wa zahanati mpya kwa ajili ya kupunguza vifo vya akina mama, wajawazito na watoto. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, zimewasilishwa taarifa mbalimbali; mpango nimeuchangia kwenye Kamati, taarifa zilizowasilishwa kuna taarifa ya Waziri, lakini kuna taarifa ya Waziri Kivuli. Naomba kwa kuwa taarifa zote ni za Bunge na zinajadiliwa na ninapojadili hapa, kambi nyingine huwa wakiona Wabunge wanachingia wanasema anataka Uwaziri. Najua Wizara ile imejaa, Mawaziri wapo wanatosha lakini nachangia ili kuweka sahihi kumbukumbu na kuuacha upotoshaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo ukurasa wa 19, tumeambiwa tulipitisha bajeti hewa na katika ukurasa wa 19, katika maelezo ya Waziri Kivuli anaeleza kwamba, sisi tulipitisha shilingi trilioni 23 kama matumizi. Nataka nimfahamishe kwa kuwa Waziri wetu Kivuli ni mgeni katika Wizara hiyo, alikuwa anahudumu Wizara ya Ardhi, mambo bado hajayajua. Lakini nataka nimfahamishe kuna vitabu Volume III, aliruka fedha za maendeleo kwa Mikoa bilioni 4.3. Pia aliruka fedha za maendeleo kwa ajili ya Halmashauri trilioni 1.3 na trilioni nne, hakuna, hakuna! Kwa kuwa hotuba hii ilichapwa kwenye magazeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mwongozo wako endapo zinawasilishwa hotuba zenye nia ya kupotosha na watu waliondoka wenyewe ndani ya Bunge. Napenda niwataarifu Watanzania hatukupitisha bajeti hewa na hili nimelisemea kwa sababu Mheshimiwa Waziri Kivuli huyu hawezi kuendana sawa na Dkt. Mpango wala Dkt. Ashatu na watendaji wa Wizara ya Fedha waliopoteza muda mwingi kuandaa makaburasha haya, kila kitu kiko sawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka niweke record sawa na kwa kuwa iligusa pia Kamati; anapozunguza masuala ya bajeti wa kuwasilisha pia maoni ni Kamati. Sasa nashangaa mwenzetu, lakini ninaomba pia wakati mwingine upangaji wa Wizara ziangalie na taaluma pia, nilishangaa Mwanasheria kuwa Waziri wa Fedha, nilishangaa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika mapendekezo ya mpango walifanya tathimini ya sekta ya fedha na hapa naomba nijielekeze ni kweli katika taarifa aliyowasilishwa Waziri kunaonyesha mikopo ya kibiashara na shughuli za uchumi kwa quarter iliyoanza Julai zimeshuka na sababu zinazopelekea ni kupungua kwa shughuli za kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali ikae na mabenki, ikae na sekta za fedha kwa sababu sekta hii inachangia kwenye ukuaji wa uchumi kwa mwaka ambao miezi sita imechangia zaidi ya asilimia 13 inawezekana kupungua kwa fedha katika mabenki hayo inasababishwa na shughuli mbalimbali au maendeleo ya teknolojia ya simu ambazo watu wengi wanatumia miamala ya fedha au masuala ya microfinance. Kwa kuwa inachangia ningeomba sana Serikali isikilizane na sekta hii ya fedha, lakini sekta ya fedha nayo iweke mazingira wezeshi itafute wateja katika maeneo mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la mwisho, muda umeisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la mwisho lilizungumzwa, ukiangalia umbile la…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Subira, muda umekwisha.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Eeh! Ahsante!