Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi nataka niseme tu kwamba mpango huu ambao tunauzungumza wa mwaka 2017/2018 suala la mazingira na mabadilio ya tabia ya nchi limezingatiwa vizuri sana katika kipengele cha 6.6 (a), (b), (c). Kwa hiyo, mkisoma pale Waheshimiwa Wabunge mtaona jinsi ambavyo suala la mazingira limezingatiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Mpango huu wa Maendeleo jambo kubwa lilikuwa ni kuanzisha Mfuko wa Mazingira ambao tayari Serikali imekubali na tayari tumeshaanzisha mfuko huo, kwa hiyo tunaamini kabisa kwamba mambo ya mazingira sasa yatakuwa sawasawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ambayo nilitaka pia kuyaweka sawasawa. Moja ni suala hili la Mawaziri kutokumshauri Rais na kusababisha mambo mengine kutokwenda sawa sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya mambo mengi, sasa hivi Serikali tumeweza kuongeza mapato toka tulivyoingia kila mwezi, wastani wa mapato yetu yameenda shilingi bilioni 400; lilikuwa ni jambo la kupongezwa na Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii toka ilivyoiingia madarakani hivi sasa tumeweza kuanzisha kanuni zile ambazo zilikuwa hazijasainiwa muda mrefu, kanuni zinazowalazimisha wamiliki wa madini kusajili katika Soko la Hisa la Dar es Salaam. Sasa hivi kanuni hizo zimeanzishwa na Mawaziri hao hao ambao leo wanaambiwa kwamba hawana uwezo wa kumshauri Mheshimiwa Rais. Vilevile Mawaziri hawa hawa, leo tumeweza kufuta mashamba sita yenye zaidi ya hekta 89,388 ambapo baadhi ya mashamba haya wamepewa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo baadhi ya Wabunge wanasema Mawaziri hawa tumeshindwa kumshauri Mheshimiwa Rais, leo Wabunge wote wanapongeza jitihanda za Serikali upande wa kilimo, leo wakulima wa pamba wanajivunia bei imeenda mpaka shilingi 1,200 kwa mara ya kwanza, korosho imeenda mpaka zaidi ya shilingi 3,000 kwa mara ya kwanza, Wabunge hawa hawa ambao wanaambiwa kwamba hawana uwezo wa kumshauri Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mambo mengine ya kusema serikali imefilisika, haiwezi kumudu majukumu yake kwa sababu haina pesa na kwamba hata fedha unazokusanya ni za arrears, si kweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatakiwa tupongezwe na bunge hili tumeweza kukusanya mapato zaidi ya shilingi bilioni 400 kila mwezi, na kwamba mpaka sasa hivi tumeweza kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni zaidi ya shilingi bilioni 878, tumeweza kulipa miradi mipya ya barabara shilingi bilioni 604, tumeweza kulipia miradi ya umeme shilingi bilioni 305, tumeweza kulipa mikopo ya wanafunzi shilingi bilioni 371, tumeweza kununua ndege kwa shilingi bilioni 103, tumeweza kulipa ndege kubwa advance kwa shilingi bilioni 21 na pointi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haya yote tumeweza kufanya katika muda mfupi, Bunge hili lilikuwa linatakiwa kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano.