Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa niseme tu kwamba na mimi naunga hoja kuhusiana na mpango huu. Lakini pili, nichukue nafasi hii kutoa pongezi za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Rais wetu mpendwa kwa kufikisha mwaka mmoja tangu alipoingia madarakani. Lakini zaidi pia mwaka mmoja ambao umejaa mafanikio makubwa katika kuiongoza nchi yetu. Utendaji wake kwa hakika umetukuka, umeiletea sifa kubwa nchi yetu ndani na nje ya mipaka yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa niweze kujibu hoja chache kwa haraka. Hoja ya kwanza nisuala zima la usitishaji au ucheleweshwaji wa ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba sababu kubwa ambazo zilipelekea au zimepelekea kutotoa ajira mpaka hivi sasa; ya kwanza ni suala zima la uwepo wa watumishi hewa kama ambavyo tulikuwa tukisema, na idadi imekuwa ikiendelea kupanda, mpaka sasa hivi tumeshaondoa watumishi 19,629 hewa ambao kwa kweli wangeendelea kubaki katika orodha ya malipo wangeendelea kusababisha hasara kubwa takribani shilingi bilioni 19.7 kwa kila mwezi.
Mheshimiwa mwenyekiti, sababu ya pili, baada ya kuwa tunaendelea kuhakiki watumishi hewa tulibaini pia uwepo wa vyeti vingi vya kughushi, tukaona hapana ni lazima tuhakikishe kwamba tunakuwa na ajira mpya baada ya kuwa tumehakikisha kwamba katika mfumo wetu wa ajira basi wale walioko katika ajira ni wale tu wenye sifa zinazostahiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu kubwa ya tatu ni uwepo wa miundo mkubwa katika Serikali na taasisi zetu. Tulipopunguza Wizara bado katika taasisi mbalimbali miundo ilikuwa haijafanyiwa tathmini, tumeshaanza huo mchakato na mchakato unaendelea vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba kwa sasa tumeanza kuimarisha mifumo ya utambulisho na ninawapongeza sana NIDA pamoja na wote walioshiriki katia zoezi, tumeongeza alama za utambulisho. Mwanzoni ilikuwa tu ni jina na check number, lakini hivi sasa walau tunaweza tukapata picha ya mtumishi wa umma, tunaweza tukapata alama za vidole pamoja na namba ya utambulisho wa Taifa katika kuhakikisha kwamba hakuna alama ambayo inaweza ikagushiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana pia na suala la muundo tumekuwa tukiangalia pia kuhakikisha kwamba tunakuwa na muundo wenye tija na muundo ambao unahimilika. Lakini vilevile tutaendelea kuhakikisha tunafanya uhakiki ili kuhakikisha kwamba tunakuwa na watumishi wale tu ambao wana sifa. Lakini niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na wananchi wanaotusikiliza wakati wowote sasa hivi hatua tumefika pazuri tutatangaza ajira muda sio mrefu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, kulikuwa kuna hoja ilitolewa na Mheshimiwa Zitto Kabwe kwamba ni nani anasema ukweli kati yangu na Waziri wa Fedha. Nimwambie tu kwamba Serikali ni moja, Waziri wa Fedha anasema ukweli na mimi pia ninasema ukweli. Kigezo cha kusema kwamba watumishi hewa; naomba tusikilizane ili muweze kuipata hoja vizuri halafu mtakuja kupinga mnavyotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watumishi hewa wameondoka 19,629, Mheshimiwa Waziri wa Fedha ataeleza kwa kina sana. Lakini ipo michakato mingine wage bill maana yake ni nini, ni lazima Mheshimiwa Zitto Kabwe afahamu. Bajeti ya mishahara ina include vitu vingi sana, kuna masuala mazima ya upandishwaji vyeo, kuna masuala mazima ya upandishwaji wa madaraja, huwezi kuwa kuna mtu anastaafu usimrekebishie mshahara wake akajikuta anaathirika katika malipo ya pensheni.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Zitto Kabwe, mimi na Mheshimiwa Mpango wote tupo sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili alisema pia kwamba tumesema tunaokoa shilingi bilioni 17 kila mwezi, hatujasema hivyo, tunachokisema kwamba endapo watumishi hewa 19,000 kwa mfululizo kuanzia mwezi Machi mpaka sasa hivi wasingeondolewa kwa mkupuo (cummulative), basi katika mwezi husika wa mshahara wangeisababishia Serikali hasara ya shilingi bilioni 19.7. Lakini hakuna popote tuliposema kwamba kila mwezi Serikali inaokoa shilingi bilioni 17. Lakini maelezo ya kina Mheshimiwa Waziri wa Fedha ataeleza vizuri sana na nini kimefanyika na niliomba rekodi hiyo iweze kuwekwa sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaunga mkono hoja.