Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Labda kwanza nianze kwa kumpongeza Waziri wa Viwanda na Biashara na Serikali kwa ujumla kwa kuleta mjadala ndani ya Bunge wa kujadili mkataba ambao Taifa letu lingeingia. Naiomba Serikali, spirit ya kuleta mikataba Bungeni na uangalie namna gani unaweza kutusaidia kupitia ofisi yako, mikataba ikawa inaletwa ili kupata mandate ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, labda nianze kujenga hoja yangu; kwa nini Watanzania tunahoji juu ya mkataba wa EPA? From the business perspective, mahali ambapo mnaenda kushindana hakuna kuaminiana, ndiyo maana tunayoosheana vidole. Tatizo la mkataba huu, hali-recognize state as an individual lina-define parties as a group. Hili ni tatizo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi ningesema na ushauri wangu kwa Serikali, kwa sababu section 143 ya Mkataba wa EPA, kama hawa wazungu wana nia njema na uchumi wa nchi yetu, tupeleke amendment; kwa sababu section 143 inaruhusu kupeleka amendment. Tupeleke amendment ku-redefine parties, kila nchi iingie mkataba na EPA kivyake kwa kuangalia maslahi yake. Bila hivyo, hatuna sababu ya kusaini mkataba huu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa nini nasema hivyo? Ukiusoma mkataba huu unanikumbusha wakati nasoma form three historia; triangular trade. This is another triangular trade in a different way. Ni mkataba ambao unatujenga sisi kuwa producers wa raw material and become a market for them. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sababu ya pili, mkataba huu unapingana na dream ambayo Tanzania imekuwa nayo toka tulivyopata Uhuru. Mwaka 1964 tuli-develop thinking ya kuwa na industries, tuka-fail. Vilevile mistrust kati yetu na Kenya jamani tusisahau. Mwaka 2015 kabla ya Bunge, Mawaziri wetu walienda kukaa kwenye East Africa, wakakubaliana mambo ya msingi kama block.
Moja, walikubaliana kuweka kodi kwenye transit goods; sisi tumekuja kuweka, Wakenya wamefuta. Kwa hiyo, how can we trust them? We will never trust them kwa sababu ya historia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, yapo mambo ambayo tumekubaliana na wao toka tuna Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kwanza, Jumuiya ya Afrika Mashariki ya pili, wenzetu wameshindwa ku-honour kwa kuangalia maslahi yao. Kwa hiyo, hili ni jambo la msingi sana ambalo tunatakiwa tulione. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo lingine ukisoma Article 20 kwenye mkataba huu, unazungumzia issues za tax; import duties, kutoa uhuru na kufungua borders without restriction. Wanakuwekea conditions kabisa kwamba ukitaka kufanya protection on your internal market or internal development, lazima upate approval kutoka kwao. Who are they? Are we not free country?
Mheshimiwa Spika, ili ujue mkataba huu ni shida, wanazungumzia compensation framework ambapo hawatoi commitment. They know we are going to lose money; we are going to lose our development truck, lakini hawaweki commitment, this is the problem. Kwa hiyo, ndiyo maana nasema, tusiseme kwamba tuko kisiwani, tuko kwenye dunia; lakini mkataba lazima uwe win win situation. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nami nataka kumshauri Waziri wa Viwanda, kwa kuwa section 143 inatoa ruhusa ya kufanya amendment; proposal ya kwanza, redefinition of parties, “this has to be a country between EU and Tanzania, not EU with East Africa, that is number one. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, number two, tukubaliane, we have raw material, they have capital, they have technology; tukubaliane kwamba chochote wanachotaka kuuza kwenye soko lao, viwanda vyao wahamishie kwetu, tu-produce ndani. If they want, they sing our song, not their song. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tusipokuwa protective; tusipokubali kama nchi ku-protect interest zetu za ndani, nataka niwahakikishie, tunaletewa; amesema mama yangu Mheshimiwa Hawa Ghasia this is a second scramble of Africa, tunageuka wazalishaji wa raw materials kama wakati ule tulipokuwa wazalishaji wa watumwa.
Mheshimiwa Spika, ukisoma Article 75 kwenye huu mkataba, unazungumzia issue za economic development. Vilevile, wameorodhesha items, wame-avoid kitu kimoja, they know, there is no development, without industrialization. There is no anywhere kwenye huu mkataba mimi nimeusoma page by page. Wanako-require na kukubali kwamba katika transfer of knowledge we will transfer teknolojia za viwanda kwenye nchi ambazo tunaingia nazo kwenye mikataba, lakini EPA Agreement wametugawa kama Afrika. EPA Agreement content zake kwenye West Afrika, hazifanani na East Africa. Kwa hiyo, wametugawagawa kwa maslahi yao.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niishauri Serikali, hamjakosea kutokusaini na niipongeze Serikali, nimpongeze Mheshimiwa Rais kutokusaini mkataba huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba huu uende uwe ni mkataba kati ya Tanzania...
Taarifa..
Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa yake.
Mheshimiwa Spika, namalizia kwa kusema kitu kimoja, East African Community ni historical. Ilikufa kwa sababu ya mistrust na kwa sababu ya economic interest ya individual state members. There is no shame kwa nchi kuingia kwenye block na kujitoa. There is no shame kwa nchi kuingia kwenye block na kulinda maslahi ya watu wake na kuachana na wenzake. Watu huachana na wake zao, huachana na wazazi wao, kwa kuangalia maslahi na yale wanayoamini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nataka niwatie moyo Serikali, EPA Agreement, if they will not follow our interest we can‟t, kuna Far East, kuna Middle East; kwanza leo tumbaku inadhalilishwa na wazungu; leo hii mazao yetu yanadhalilishwa na wazungu, we should think of another way. Ahsante.