Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ili nami niweze kuchangia kidogo kwenye mkataba ambao upo mbele yetu. Kwa sababu mengi yameshazungumzwa na wenzangu, nitazungumza machache sana.
Mheshimiwa Spika, kwanza linapokuja suala la maslahi ya Taifa lazima tusimame kama Taifa. Japokuwa tuna Umoja wa East Africa, lakini kila nchi ina levels zake za maendeleo ambayo ime-move. Kwa hiyo, tunapoenda kuangalia suala la maslahi ya Tanzania tuasianze kusema kwa nini fulani kasaini, kwa nini Uganda kasaini, kwa nini Kenya kasaini? Yapo mambo ambayo yamemvutia yeye kusaini huo mkataba. Kwa hiyo, kwenye masuala ya maslahi ya Taifa tusimame kama Taifa kuangalia maslahi ya Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, ni jambo la kusikitisha kwamba mkataba ambao upo mbele yetu ukiusoma vizuri unaturudisha nyuma karibu miaka 50 tuliyotoka. Unakwenda kutupangia masharti wakati tumepigana angalau miaka 50 tunaanza kuweka sera za uchumi, sera za mapato na sera mbalimbali nzuri, inatuambia sasa kwamba tuache sera zote pembeni tufuate masharti ya EU, hatukubaliani na hilo.
Mheshimiwa Spika, leo tunazo sera ambazo sahihi jinsi ya kukusanya mapato. Mkataba unachambua, zipo changamoto na hasara ambazo tutazipata kutokana na kuingia mkataba huu.
Mheshimiwa Spika, nasema ili muweze kuondokana na hasara hizo, lazima mkae mrekebishe sera za mapato ndani ya nchi zenu, hivi kweli tupo sawa sawa? Cha kusikitisha sana, pia wanatuambia ili muweze kufidia hasara zitakazotokana na kuruhusu biashara free kuingia nchi yetu bila ushuru muweze kukaa muongeze VAT kwenye bidhaa ndani ya nchi yenu ili muweze kufidia hasara.
Mheshimiwa Spika, tukiongeza VAT kwenye bidhaa zetu, tunamuumiza nani? Tunawaumiza wananchi wetu, kwa sababu vyote wanaenda kulipa wananchi wetu. Kwa hiyo, tunalazimishwa sasa kwenda kuwabana zaidi Watanzania kwa sababu tu ya kukidhi matakwa ya Mkataba nchi za Ulaya.
Mheshimiwa Spika, kwenye suala kama hili kiukweli ni lazima tuwe makini, tuwe makini sana jamani. Juzi tulikuwa na bajeti mwezi wa sita, tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda; ni nchi gani duniani ambayo imeweza ku-move kwenda kwenye industrialization bila kulinda viwanda vya ndani? Hakuna. Hata hao Ulaya ambao leo tunaona wame-move, walilinda viwanda vya ndani.
Mheshimiwa Spika, kwanza sisi mpaka hapa tulipo bado ni soko la bidhaa za wenzetu, ni soko la pamba-stick, ni soko la Wachina, ni soko la Wakenya, ni soko la wengine. Haitoshi tu tukafungue wazi, sisi tuwe kazi ni kuzalisha na kupeleka.
Mheshimiwa Spika, kama tunataka ku-move na mikataba kama hii na mikataba mingine naomba, kama Taifa lazima tuje tuwe na watu ambao tunapokuwa na mikataba kama hii waende ku-negotiate; negotiators wenye uwezo mkubwa. Kwa sababu mkataba kama huu haukutakiwa hata sisi kuja kuujadili; ulitakiwa uishie huko huko! Baada ya kuona kwamba hatuna maslahi nao, wanapiga pembeni, tunasonga mbele kwenda na mambo mengine ambayo yana maslahi kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, lazima sisi Wabunge tuisimamie Serikali vizuri, tuje tuwe na watu wenye uwezo, capacity thinking nzuri ya kuweza kuwa negotiators kwenye mikataba kama hii hasa ya kitaifa ambayo tusipoiangalia vizuri, kipengele kimoja tu kinaweza kutu-switch tunajikuta kwamba tunaenda kuwa watumwa wa nchi nyingine badala ya ku-move kwenda mbele kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, naungana na wenzangu Wabunge wengine wote kwamba mkataba kama huu hautufai na hata kama utatufaa, ni huko mbeleni. Pengine miaka 50 ijayo tuwe tume-move kidogo tumekuta wenzetu. Kama Wakenya, leo Kenya ni nchi ndogo, lakini kila nchi pia ina factors zake. Leo Tanzania tupo karibu milioni 50. Wakenya wenyewe ni wachache, lakini pia sera zinatofautiana. Kwa hiyo, lazima tuangalie factors nyingi nyingi kuhakikisha kwamba mikataba ya Kimataifa kama hii tunaipitisha. Kila mkataba unaopitishwa, tuangalie maslahi yetu, tusiangalie East Africa kwa sababu kila mmoja anapambana kwenye uwanja wake.
Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Ahsante sana.