Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii na mimi niweze kuchangia. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya ili na mimi niweze kuchangia taarifa hizi za Kamati mbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa. Naomba nianze kuchangia moja kwa moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016, Sehemu ya Nne fasili ya (16) inasema Kamati yetu ya LAAC itafanya kazi kwa kutumia taarifa zilizokaguliwa na Mkaguzi wa Nje. Kamati ilikumbana na changamoto nyingi wakati wa utekelezaji wa majukumu haya ikiwemo Ofisi ya CAG kukosa fedha kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tukichangia bajeti ya mwaka 2016/2017 tuliongelea sana suala hili. Pamoja na bajeti iliyopitishwa upelekaji wa fedha umekuwa ni wa shida. Tunafahamu kwamba kazi za CAG zinafanyika kwa msimu kwa hiyo, kufikia ile Julai, 2016, CAG alikuwa hajapelekewa fedha za kutosha kumuwezesha kutekeleza majukumu yake ili Kamati iweze kutumia taarifa zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto hiyo ilipelekea Halmashauri ya Korogwe ambayo walikuwa wametumia fedha kwa ajili ya kujiandaa kuja kukaguliwa na Kamati mfano usafiri, posho za kujikimu, stationery tuliwarudisha kwa sababu hoja zao zilikuwa hazijafanyiwa verification. Hivyo, nashauri Wizara ya Fedha ipeleke fedha kulingana na plan of action ya Ofisi ya CAG. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee kipengele cha mishahara isiyolipwa. Serikali ilianza utaratibu wa kulipa mishahara ya watumishi wa Halmashauri moja kwa moja kupitia akaunti zao. Changamoto iliyopo, Mkurugenzi wa Halmashauri anatoa zuio la mishahara kulipwa kwa Meneja wa Benki. Mishahara inapozuiliwa Meneja wa Benki anairudisha moja kwa moja Hazina Kuu, Hazina Kuu inakiri kupokea fedha hizo kutoka kwa Meneja wa Benki. Changamoto inayotokea ni kwamba kunakuwa na gap kati ya Meneja wa Benki na Mkurugenzi na Mkurugenzi na Wizara ya Fedha. Meneja wa Benki hana document ya kuweza kumrudishia Mkurugenzi kuonyesha mishahara iliyozuiliwa kwa sababu hawezi kuirudisha kwenye akaunti ya Halmashauri. Hazina hawawezi kutoa risiti tena kwa Mkurugenzi itakuwa ni double accounting ya revenue. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Wizara ya Fedha haijatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ni nini wafanye ili kuweza ku-reconcile mishahara ambayo haijalipwa. Wasipofanya hivyo kutatokea loophole kwa watumishi wa benki wasio waaminifu, wakiona hakuna ufuatiliaji wa karibu mishahara mingine inaweza ikalipwa tu kwa watumishi wasiostahili.
Naishauri Wizara ya Fedha ifanye mawasiliano na Wakurugenzi Watendaji. Kwa mfano, Jiji la Tanga lilikuwa lina hoja ya mishahara isiyolipwa ya shilingi milioni 168.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie katika kipengele cha mfumo wa kihasibu wa EPICOR. Halmashauri nyingi zilikuwa zina hoja…
Mheshimiwa Mwenyekiti,…
Ninyi mbona mnanichanganya bwana.
Haya sawa. Mheshimiwa Naibu Spika,…
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunilinda.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri nyingi zilikuwa zina hoja ya matumizi mabaya ya mfumo wa EPICOR. Tunavyofahamu Serikali ilitumia fedha nyingi kwa ajili ya kupeleka mfumo huu kwa lengo la kudhibiti matumizi mabaya na kudhibiti mapato. Changamoto iliyopo kuna baadhi ya package bado hazijaingizwa katika mfumo wa EPICOR, kwa mfano asset management. Hii inapelekea Halmashauri nyingi kutoa taarifa au kukamilisha kazi zao nje ya mfumo kwa sababu mfumo haupo wakati Serikali ilitumia fedha nyingi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la mfumo huu pia ilikuwa ni ku-control matumizi mabaya ya vifungu. Tukiangalia kuna hoja nyingi za wrong accounting coding. Hii inapelekea hata taarifa zinazotolewa kwenye Halmashauri katika vikao mbalimbali kuwa siyo zenyewe kwa sababu zinafanywa nje ya mfumo. Nashauri Serikali ifanye ufuatiliaji kuhusu matatizo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie kuhusu matumizi ya fedha nje ya bajeti katika fedha za miradi. Kwanza, napenda nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa maagizo anayotoa kwa ajili ya Halmashauri. Mheshimiwa Rais ana lengo zuri lakini changamoto inakuja maagizo yanapotolewa zipo Halmashauri nyingine zina uwezo wa kutumia wadau waliopo katika Manispaa au Majiji kazi hiyo ikafanyika. Halmashauri nyingine hazina uwezo wa kupata wadau hao inawalazimu watumie fedha kwa kutozingatia bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunapitia taarifa Halmashauri nyingi zilionekana miradi mingi haijatekelezwa kwa mfano miradi ya maji, miradi ya …
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati fedha hizo zimetumika katika maabara. Je, Serikali inafahamu ni miradi kiasi gani iliyoathirika na ina mkakati gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache naunga mkono hoja.