Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. DKT. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia jioni ya leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mambo mengi yameshazungumzwa kuhusu suala hili, lakini lazima tuwe wazi tunavyozungumza Halmashauri na tunavyozizungumzia Halmashauri ninaomba tuweze kujiuliza maswali kadhaa. Tatizo tunalolipata katika Halmashauri zetu ni tatizo la kutopelekwa kwa fedha kwa wakati au kutopelekwa fedha kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaweza tukawasema Wakurugenzi, tunaweza tukasema Halmashauri hazifanyi kazi, lakini tatizo tunalolipata ni kwamba Wizara haipeleki pesa katika Halmashauri kwa muda. Sasa tatizo kama hili linapotokea kule kwenye Halmashauri kunakuwa hakuna namna nyingine ya kuweza kufanya kazi katika utaratibu ambao Serikali ilikuwa inataka na ndiyo maana tunakuta kwamba miradi mbalimbali haikamiliki. Kwa mfano, miradi ya maji inashindwa kukamilika, miradi ya barabara inashindwa kukamilika, lawama zinaenda kwa Wakurugenzi, lakini tatizo hili lazima tujiulize je, Wizara ya Fedha inasema nini kuhusu suala hili? Halmashauri ngapi ambazo tayari zimepata zaidi ya asilimia 70 ya bajeti? Ni nani ambaye anaweza akasimama na kusema Halmashauri yake imepata pesa za kutisha za miradi katika mwaka? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tatizo hili kubwa tunalolipata lazima Wizara ya Fedha iweze kusimama na kusema pesa zinakwenda wapi au pesa zinapelekwa namna gani katika Halmashauri mbalimbali. Tunavyosema makusanyo yanaongezeka lazima tuangalie upande wa pili, unavyokusanya basi tujue tunavyopeleka katika Halmashauri twende kwa uwiano, hatuwezi kusema tunakusanya kiasi hiki, lakini kwenye Halmashauri hatupeleki pesa zozote. Kuna Halmashauri zimepata asilimia 30 ya bajeti, kuna Halmashauri zimepata asilimia 20, asilimia 30, asilimia 40; lakini kuna miradi mbalimbali na Halmashauri nyingi zina madeni makubwa. Wengine wameshazungumza hapa na wamesema kwa undani zaidi, kuna Halmashauri zinadaiwa mabilioni ya fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi lazima niwe wazi na niseme kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati ya LAAC, nimeona mambo mengi na tumejadili na tumeziita Halmashauri mbalimbali kwenye Kamati. Tatizo tunalolipata si tatizo la Wakurugenzi peke yake. Ndiyo kuna Wakurugenzi wapya, ndiyo kuna watumishi wapya, lakini tunachokisema tunaomba sasa Wizara husika iweze kuchukua nafasi ya kuweza kuwaelimisha hawa Wakurugenzi wapya na watumishi wapya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mchangiaji aliyepita alizungumza akasema tuna chuo pale Hombolo, sasa kwa nini tunashinwa kukitumia chuo hiki ili watu hawa waweze kufanya kazi katika hali ambayo tunadhani itaweza kuleta tija katika Halmashauri zetu? Kuna mambo mengi ambayo wanashindwa kuyafahamu, wanakuja kwenye Kamati wanashindwa kujieleza. Ile competitiveness haipo! Unashindwa kujua kwamba huyu mtu ame-qualify katika sekta gani, katika eneo gani? Unapomuuliza kwa nini uli-realocate fedha hizi anashindwa kueleza. Kwa hiyo, lazima tuweze kujua Wizara inayohusika imefanya kazi gani kuhakikisha kwamba watu hawa wanaweza wakatumika inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo kadhaa ambayo tumeweza kuyatizama, lakini jambo la msingi kuna asilimia 10 na kuna asilimia 20; asilimia 10 za vijana na akinamama na asilimia 20 zinazotakiwa kupelekwa kwenye vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni masikitiko makubwa kuona Halmashauri zote tulizozihoji katika Kamati yetu hakuna Halmashauri ambayo ilifanikiwa kupeleka asilimia 10 kwa uzito wake au kwa ujumla wake. Sasa tunafanye ili kuhakikisha kwamba Halmashauri hizi zinawaangalia vijana? Halmashauri hizi zinawaangalia akinamama? Halmashauri hizi zinaangalia wananchi kule vijijini?
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunavyoshindwa kupeleka hizi asilimia tano kwa vijana, na mimi kama kijana lazima niwe na masikitiko makubwa. Vijana wenzangu kule wanataka kuendesha miradi yao, lazima waone hizi hela zinakwenda. Sasa ni maajabu ambapo utaweza kusimama hapa na kutetea kwamba Halmashauri zinapeleka asilimia 20 jambo ambalo sio sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi nilikuwa naomba kwamba Wizara iweze kuangalia kwa undani zaidi halmashauri zinafanyaje kazi, hizi asilimia 10 za vijana na akinamama ni fedha ambazo zinatoka kwenye mapato ya ndani ya Halmashauri, lakini kwa bahati mbaya ukiangalia hata hizi Halmashauri zetu ukusanyaji wa mapato ya ndani bado unasuasua. Hatuna makusanyo ya kutosha, vyanzo vya mapato hatuna vya kutosha kwenye Halmashauri kuweza kuhakikisha kwamba, hizi asilimia 10 zinakwenda kwa wahusika na walengwa. Sasa tutakaa na tutajiuliza muda wote namna gani tunavyoweza kusonga mbele, lakini tatizo linabaki palepale kwamba kama Wizara haipeleki fedha kwenye Halmashauri na tunazituma Halmashauri ziweze kufanya makusanyo ya ndani kupitia miradi yake mbalimbali, tutaweza kupata matatizo makubwa huko mbele kwa sababu tunashindwa kuzihudumia hizi Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine baya zaidi, afadhali useme kijana, lakini unavyomnyanyasa mwanamke kwa kumnyima ile asilimia yake tano ni kitu kibaya kuliko vyote. Unakuta Mkurugenzi yuko pale kwenye Kamati anashindwa kujieleza kwa nini kashindwa kupeleka zile asilimia tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jana nilikuwa nikiangalia katika chombo kimoja cha habari watu wanalalamika sehemu fulani wanasema akinamama na ndoa zao zinaenda kuvunjika kwa sababu ya kwenda mbali kutafuta maji, wanatumia masaa matatu, manne, matano. Sasa fedha hizi ambazo tunazisema ndizo ambazo tunataka watu wa kutoka halmashauri waweze kuhakikisha kwamba zinaenda kwa akinamama. Na akirudi nyumbani anapata kichapo vilevile kutoka kwa mume wake. Sasa hili sio jambo la kuweza kulifumbia macho, ni jambo la msingi sana kwa sababu, misingi ya jamii yetu nayo itaenda kuporomoka kwa sababu ya kukosa mambo ya namna hii ambayo tunayazungumza, na ni mambo ambayo yanajirudia mara kwa mara.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyozungumza kuhusu upelekwaji wa miradi mbalimbali katika maeneo yetu na tukiangalia hasa sisi tunaotoka katika maeneo ya vijijini kule tunajua changamoto ya maji, kwamba unavyoshindwa kuwa na maji hilo ni tatizo kubwa. Lakini vilevile tunavyoshindwa kuwaeleza wananchi wetu kwamba kuna asilimia tano, kwa sababu haya ni mambo ambayo aidha Wakurugenzi au wanasiasa tunashindwa kuwaeleza wananchi wetu kwamba kuna asilimia tano na mambo yanakuwa kimya kimya watu wanapiga ile pesa na ndiyo maana watu wanatumia maneno wanasema wanapiga-deal kwa sababu wamekula fedha ambazo zilitakiwa ziende kwa wahusika, sasa sijajua tunaweza kuwachukulia hatua gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ukiangalia katika miaka mitatu, mine, mitano ambayo tumekuwa tukikagua hizi Halmashauri, hakuna Halmashauri ambayo imetekeleza hilo, lakini bado tunakuta hakuna namna ambavyo hawa watu wa Halmashauri wanachukuliwa hatua za kisheria. Kwa hiyo, mimi ningependa kushauri kwamba, sheria iweze kuchukua mkondo wake wakati mwingine kwamba, tunavyoshindwa kuwapelekea hawa vijana, akinamama na hizi fedha za asilimia 20 kule vijijini basi tuweze kujua namna gani tunaweza kuwaadabisha hawa, nitumie hilo neno.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ningependa kuzungumza kwamba kuna matatizo ya watumishi ambao wamekaimishwa kwa muda mrefu, hili kwa sasa ni tatizo kubwa. Mtu amekaimishwa miaka mitatu, mtu amekaimishwa miezi zaidi ya sita, lakini unashindwa kujua kwa nini Serikali au TAMISEMI inashindwa kufanya huyu mtu sasa apewe nafasi yake kwa sababu kama anaweza kufanya kazi basi mpeni nafasi, lakini kama anashindwa basi mmuondoe. Unamkaimisha mtu kwa zaidi ya miezi sita, zaidi ya mwaka mmoja, zaidi ya miaka miwili, halafu unategemea kutakuwa kuna utendaji pale katika Halmashauri? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, haya ni mambo ambayo yapo, si mambo ambayo tunayatoa kwenye hadithi ni mambo ambayo yapo kwenye Halmashauri zetu, na ndiyo maana hata utekelezaji wa baadhi ya majukumu katika Halmashauri yetu watu wanakuwa wanshindwa kuwa na uhakika, je, kesho watakuwepo au hawatakuwepo. Kwa hiyo, mimi nilikuwa napenda kushauri kwamba sasa umefika wakati kwa wale wanaokaimishwa waweze kupata nafasi zao au waweze kuondolewa katika nafasi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo mbalimbali tumeyaona. Kuna mikataba mibovu imeingiwa katika maeneo mbalimbali, mikataba ambayo huwezi hata ukaamini kwamba hivi kwa nini mwanasheria aliweza kusaini mkataba kama huu?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni masuala hayo hayo kwamba watu wamekaimishwa kwa muda mrefu, wanashindwa kupata majibu ya ajira zao, wanaona tu wasaini mikataba wapate vijisentisenti wakimbie. Na kuna maeneo ambayo tumeyaangalia kwa undani tukajua kabisa hapa kuna tatizo la kimkataba. Kwa hiyo, mimi ningependa kuangalia hili kwa undani na kuiomba Serikali iweze kutizama kwa umakini masuala ya watumishi ili kwamba TAMISEMI sasa ichukue jukumu hili kuweza kuwapa nafasi hawa watu ambao wanakaimishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la CAG. Ni kweli kwamba wengine wengi wamezungumza wamesema CAG anashindwa kuwezeshwa. Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ilikuja kwenye Kamati ikarudishwa kwa sababu kulikuwa hakuna tathmini iliyofanywa na CAG. Sasa hii ni aibu kubwa kwamba unavyoirudisha Halmashauri je, hizi fedha ambazo wamekujanazo kwenye Kamati, kama ilikuwa Dar es Salaam au Dodoma? Lakini kumbe tatizo linakuwa ni CAG ameshindwa kuwezeshwa. Kwa hiyo, mimi ningependa kuishauri Serikali kwamba sasa kama tunasema CAG ndio jicho letu basi tumuwezeshe CAG, tatizo liko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakuwa tunalalamika kila siku kwamba, hatuna fedha huku hatuna fedha kule, lakini ninachokisema ni kwamba lazima tuwe tuna mikakati. Tuweke mikakati yetu sawa ili kwamba kama CAG tutamtumia na tunaendelea kumtumia basi tumuwezeshe.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati yetu sisi tunashindwa kwenda kukagua miradi mbalimbali katika maeneo mbalimbali, tunakaa tunawaita Wakurugenzi waje na mavitabu makubwa namna hii. Mtu ukiliangalia lile likitabu unashindwa hata kuanza useme nianzie wapi. Lakini kumbe ile miradi ambayo ipo kule majimboni, iko kule vijijini, tunashindwa sisi kwenda kuiangalia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanakuja wana-manipulate tu zile figures wanasema hivi sawa sawa na vile, hivi sawa sawa na vile, mradi hujauona, na tupokuja huku kutoa ripoti na tunavyosema kwamba kitu hiki hakijakaa vizuri, ile value for money, lakini ni mambo ya kusikitisha sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ningependa kuishauri Serikali, najua Bunge lilikuwa lina mfuko sasa sijui ule mfuko uko wapi? Kwamba watuwezeshe basi twendeni tukafanye kazi, tuko tayari kufanya kazi. Lakini sasa tunavyoshindwa kwenda kufanya kazi kule na tunakaa tu kama ni Dodoma au kama ni Dar es Salaam haisaidii. Twende kule tukafanye kazi tukaangalie miradi, fedha ambazo Serikali ilipeleka tukaangalie kwamba huu mradi upo au haupo. Sasa utaambaiwa kuna mradi umepelekwa kule umekamilika una milioni 300; milioni 500, lakini ukienda kule ule mradi haupo, mnazungushwa tu kwenye magari kule mpaka unachoka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba niishie hapo, lakini ninaunga mkono hoja. Ahsante sana.