Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kama walivyosema watangulizi wangu, nianze kwanza kwa kuzipongeza hizi Kamati mbili za PAC na LAAC kwa kazi nzuri walizofanya na ripoti zao ni nzuri sana na pia recommendation zao nazo ni nzuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, labda nianzie pale alipoishia msemaji wa mwisho. Ukiangalia masuala yote haya inaonekana udhibiti wa haya mashirika yetu na hata taasisi zetu kuna mahali pana legalega. Ukijaribu kuangalia kwa mfano mdogo tu kwa ripoti kama ya NSSF achilia mbali hiyo ya Mradi wa Dege lakini wamekopesha mikopo kwa SACCOS mabilioni mengi na wao sio benki, hawana utaalam wa taasisi za kibenki. Kawaida ya SACCOS unategemea kwamba hawa wanafanya savings and credit unakuta SACCOS ndiyo zinaanza kukopa, ni kitu cha hatari sana katika uchumi wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tungetegemea SACCOS zikusanye savings huko na zikopeshe wale members wao. Sasa unakuta shirika kama NSSF ambapo siyo kazi yake inakwenda kukopesha SACCOS na hizo SACCOS kama ripoti inavyosema zingine ni hewa, zaidi ya shilingi bilioni 70 imetolewa kama ilivyoelezwa kwenye ripoti humu. Hizo pesa zote ni za umma na zimekwenda sehemu ambayo siyo. Kama ripoti ya PAC ilivyosema ufanyike uchunguzi kuangalia namna hiyo mikopo ilivyotolewa na ilikwenda kwa nani na kwa jinsi gani. Sidhani kama wana kitengo maalum kwa ajili ya kukopesha na sidhani kama wana software ya kibenki ambayo inaweza kufanya tracking ya mikopo hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni la usimamizi wa mashirika yetu. Kuna mifano imetolewa ya EWURA na SUMATRA kuwa yale makusanyo yao yote wameyatumia katika matumizi ya mishahara na matumizi ya kawaida. Ukiangalia EWURA wametumia zaidi ya 71% na SUMATRA wametumia 82% ya pesa walizokusanya. Sasa unajaribu kuangalia hawa SUMATRA na EWURA ni vyanzo vya mapato ya Serikali, badala ya kutumia hizo pesa kutunisha Mfuko wa Hazina wenyewe wamezitumia kwa matumizi ya kama kujilipa mishahara, posho na matumizi mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naungana na PAC kushauri kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina iweze kuimarishwa ili iweze kuyasimamia mashirika haya kwa ukaribu zaidi. La sivyo tutaendelea kutegemea tax revenue na tukaacha hili eneo ambalo Serikali yetu kama ikilisimamia vizuri litaondoa kabisa kutegemea kodi ambazo zinaongezeka kila siku. Tukisimamia hizi investments, haya mashirika tuna uwezo hata wa kupunguza kodi kwa wafanyabiashara wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wenzangu waliongelea kuhusu Internal Auditor (Mkaguzi wa Ndani). Nafikiri huu mfumo uliopo sasa hivi kwa Wakaguzi wa Ndani kwenye Halmashauri zetu kuwa chini ya Wakurugenzi siyo sahihi. Internal Auditor kama alivyo External Auditor wanatakiwa wawe na uhuru wa aina fulani kwa watu wanaowakagua. Sitegemei Internal Auditor anayeripoti kwa Mkurugenzi amkague Mkurugenzi atatoa ripoti nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikawaida hata code of ethics za Internal Auditors zinasema Internal Auditor awe independent anatakiwa aripoti kwa mtu ambaye ni tofauti. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile nilivyokuwa naangalia governance za hizi Halmashauri zetu nafikiri kuna vitengo ambavyo vinahitaji kuimarishwa kama Audit Committee na Risk Committee. Ukiangalia composition za hivi vitengo nafikiri haziko sawasawa. Kama tungekuwa na Internal Audit Committee na Risk Committee ambazo zinajitegemea tungeweza vilevile tukaagiza hawa Internal Auditor waripoti kwenye hizi committee ambazo ziko nje ya utawala wa DED. Mimi naona kwa vile kuna Director of Internal Audit ambaye yuko chini ya Wizara ya Fedha labda angejaribu kuwa karibu zaidi kuwaangalia na kuwasimamia hawa Internal Auditors ili waweze kulinda maslahi ya pesa zetu na kusiwe na ufujaji mkubwa wa hizi pesa zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.