Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Huu ni Mpango mzuri. Waheshimiwa Wabunge mawazo yenu tumeyapata na tutayafanyia kazi na mengine tunayafanyia kazi tayari. Cha maana cha kujua ni kwamba maana ya uchumi ambao unafanyiwa mapinduzi makubwa huwa mara nyingi haukubaliki kiurahisi, ndio historia ya mapinduzi ya kiuchumi duniani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa mafuta na gesi, nataka niwaeleze Watanzania ukweli, wengine wamesema hakuna wataalam siyo kweli na wala hatuhitaji kumleta kama alivyosema mwingine mzungu mmoja aje kutufundisha, haiwezekani hiyo. Kwa sababu huku kuna watalaam kweli kweli. TPDC penyewe kuna Ph.D nne, kuna Masters 62, kuna shahada za kwanza zaidi ya 200. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kina degree programmes zaidi ya tano, UDOM wapo tano, lengo ni kwamba kwa miaka michache inayokuja Tanzania ndiyo itakuwa na wataalam wengi wa madini na mafuta nchini hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunasomesha watu, mwaka huu Norway tumemaliza scholarship ya watu 40 na wengine 40 tutaziomba tena. Kwa hiyo, maana ya mageuzi haya tunayoyaongelea ndugu zangu Wabunge yataendana na uchumi wa gesi, ndiyo roho ya mapinduzi ya uchumi wetu na niwahakikishie tuko kwenye njia nzuri. Wanaosema hawaoni faida, umeme utatoka huko, viwanda vya mbolea tutajenga, majumbani tutatumia na gesi tutaisindika.
Mheshimwa Mwenyekiti, niongelee kingine ambacho ni injini ya mageuzi yote haya, ni mambo ya umeme. Ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote ni kwamba, umeme wa uhakika na umeme wa bei ndogo lazima utapatikana kwenye Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kwa mahesabu, sio kwa hisia, sio kwa matusi, sio kwa kumkejeli mtu. Ni lazima tutoke kwenye power per capita, yaani mtu mmoja mmoja, mwenye umeme wa units 108 kwenda units 3000. Ndio kazi ambayo Wizara ya Nishati inaifanya. Hiyo inaendana na ukuaji wa uchumi, utoke sasa hivi asilimia saba mpaka asilimia 10 kwa mwaka ili ifikapo mwaka 2025, tukiwa nchi ambayo ni ya kipato cha kati, yenye Pato la Taifa GDP ya bilioni 240, tunahitaji umeme wa uhakika na Wizara ya Nishati na Madini na Serikali kwa ujumla ndiyo kazi inayoifanya hiyo.
Sasa Waheshimiwa Wabunge kingine ambacho ni cha kufahamu, tumeongelea sana fedha za wafadhili, Watanzania wote naomba tuelewane, fedha za wafadhili ni tofauti na fedha za uwekezaji. Mimi huku Wizara ya Nishati na Madini, hata wakinipatia fedha zote za wafadhili, ni fedha kidogo. Fedha za wafadhili, wasiojua siyo zaidi ya dola milioni 500 kwa mwaka, dola za Marekani hazivuki milioni 500. Halafu upatikanaji wake, kwa ndani ya miaka 10 hesabu zimepigwa ni wachache wamevuka asilimia 50 ya ahadi walizozitoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kinyerezi I, megawati 150, uwekezaji ni dola milioni 183. Kinyerezi II ambayo tutaweka jiwe la msingi mwezi huu, inahitaji dola za Marekani, milioni 344. Hizo ni zaidi ya fedha za wafadhili. Kwa hiyo, tunachokitafuta sisi, ni fedha za uwekezaji, kwa hiyo, Watanzania msiwe na wasiwasi, fedha za wawekezaji zitapatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wengine wamesema Exim Bank ya China imekataa, siyo kweli. President Jinping alivyokuwa Afrika ya Kusini ametoa dola bilioni 60, kwa uhusiano wa China na Afrika. Tanzania ni kati ya nchi tatu ambazo zitafaidika. Nawaambia Wizara yangu yenyewe, mimi nataka…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji