Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Na mimi kwa sababu ya muda mfupi nikubaliane na kumuunga mkono dada yangu Mheshimiwa Halima kwa hapo alipofika. Nikuhakikishie kwamba na sisi tunajua kama kuna utapeli umefanyika wa kulisadikisha Bunge hili kwamba Lugumi walichokuja nacho mara ya pili ni cha ukweli wakati ukweli halisi unajulikana. Kama alivyosema ni maajabu katika muda wa mwezi mmoja kutoka vituo 14 vikaja 153. Huo ni uongo, ni uongo, ni uongo kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nataka nianze kuchangia kwa kusema kwamba nasikitika sana kwa taarifa hizi nzuri ambazo tumeletewa hapa na wenzetu wa PAC na LAAC lakini kuna upungufu na nataka nianze na hii ripoti ya LAAC.
Kamati hizi ni za Bunge na ni Kamati za mahesabu. Umuhimu wa Kamati hizi hakuna ambaye hawezi kuuona kwa vyovyote vile iwe kwa jicho la karibu au kwa mbali. Hata hivyo, malalamiko makubwa yaliyopo hapa, nataka nisome katika ukurasa wa nne wa taarifa hii ya LAAC, anasema, nanukuu:-
“Zipo namna kuu tatu za kutekeleza majukumu ya Kamati ambazo ni:-
3. Kamati kuzuru na kufanya ukaguzi wa matumizi ya fedha katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika baadhi ya Halmashauri ili kujiridhisha na thamani ya fedha katika miradi hiyo (value for money).”
Mheshimiwa Naibu Spika, cha kusikitisha sana ni kwamba tunaletewa taarifa hizi, siyo LAAC wala PAC, wote wanasema hakuna aliyepata fungu la kwenda kujiridhisha na taarifa hizi tulizoletewa hapa. Kwa maana nyingine ni kwamba wao wamepelekewa taarifa kwenye meza na wametuletea sisi hapa bila kuthibitisha chochote, hili ni kosa moja kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ni mambo ya kimahakama kosa hili linafanana na utakatishaji fedha, uhaini, ugaidi, makosa ambayo hayana dhamana, ndiyo! Kwa sababu tunakotoka tunajua mambo yaliyokuwa yanaletwa kwenye makaratasi na wanapokwenda field kwenye ukaguzi kulikuwa kunakuja manyago makubwa sana. Kulikuwa kunakuja mambo ya hatari, mtu anaoneshwa hapa imejengwa shule wakifika hata kiwanja hakuna. Leo Bunge mmeridhia tuletewe haya kwenye makaratasi badala yake tunakuja kulishwa humu na tunapiga makofi tunakubaliana nayo. Hili ni kosa moja kubwa sana ambalo Serikali haihitaji kupewa dhamana juu ya kosa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa najua tunabana na kubana mimi najua kuna utamu wake, lakini na kubanua kuna raha zake. Huwezi kubana moja kwa moja ukadhani mambo yataenda, haiwezekani. Lazima sehemu nyingine ubanue kidogo ndiyo raha ipatikane. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka ninukuu usemi…
Mheshimiwa Naibu Spika, hicho ni Kiswahili cha mwambao. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka ninukuu usemi wa hekima aliosema Rais Mstaafu kipenzi cha nyoyo, Jakaya Mrisho Kikwete. Hivi karibuni alisema hivi, unapokuwa mpya watu wanataka mambo mapya, lakini yawe mapya ya kimaendeleo siyo mapya ya kuharibu kule tulikotoka. Huu ni usemi mmoja wenye hekima sana kwa Rais wetu yule mpendwa mstaafu, Mungu amjalie akae kwa amani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hizi taarifa za CAG ndizo zilizosaidia kuonesha madudu makubwa sana yaliyofanyika ndani ya nchi hii lakini leo hata CAG amelalamika kushindwa kwenda kufanya verification kwa sababu hakupewa bajeti ya kutosha. Mnataka kuficha nini ikiwa CAG sasa hapewi uwezo wa kwenda field kuangalia uhalisia wa mambo yanayofanyika? Mmeanza kubana Bunge lisionekane live, mmeanza kubana mikutano ya vyama vya siasa, mmeanza kumbana mpaka CAG asiende kwenye kazi zake? Tunawatendeaje haki Watanzania? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hatari na kama huko tunakokwenda mwendo wenyewe ndiyo huu jiangalieni upya. Mliwaambia Watanzania mnaleta ajira, mnaleta maisha mazuri, mnaleta afya, Watanzania wakawaamini na kuwapa kura zao sasa fanyeni yale mliyowaahidi Watanzania msiende kinyume chake. Siku ya hukumu inakuja na haiko mbali, siku zinakwenda kweli kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshangazwa na jambo lingine na mimi nataka niliseme kwamba Kamati ya PAC wamelalamika hapa na mchangiaji mmoja amelalamika anasema wametaka taarifa ya madeni ya TIB wamenyimwa. Hili ni kosa lingine la uhaini kabisa kwa Kamati ya Bunge kunyimwa taarifa ili wafanye kazi zao. Hili Bunge linaonekanaje sasa? Hili siyo Bunge tulilotokanalo sasa tunataka kuchezewa na sisi tumekubali kuweka videvu vichezewe, haiwezekani! Ni lazima tuoneshe wajibu wetu kama wawakilishi wa wananchi ni vipi tumeisimamia Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Kamati yangu hatukukubaliana na hili na TIB walileta orodha yote ya waliokopa Community Import Support tukawa nayo. Kwa hiyo, haiwezekani ni lazima wakubaliane na matakwa ya Kamati za Bunge, hakuna namna nyingine, ahsante sana.