Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nashukuru kupata nafasi hii na namshukuru sana Mheshimiwa Paresso kwa kunipa muda wake nitumie kuchangia.
Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi niseme mambo machache na niseme pale Wabunge wenzangu walipoishia. Tatizo kubwa ninaloliona mimi hasa kwenye uendeshaji wa Serikali za Mitaa ambazo kimsingi ni Serikali kamili, zimepewa mamlaka yake Kikatiba. Leo kila mtu aliyesimama hapa analalamika, aidha, kwa Wakuu wa Wilaya au Wakuu wa Mikoa kuingilia mamlaka za Halmashauri. Hii inafanyika kwa sababu kila mtu anafukuzia kumfurahisha bosi, Mtukufu Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, yaani watu wanafanya madudu pale na imekuwa utaratibu kwamba watu waliofanya madudu wanapandishwa cheo. Sasa na wengine kule Wilayani anatafuta na yeye nitoke vipi. Mkuu wa Wilaya anatembea nyuma kuna kamera utafikiri anaenda sijui kufanya shooting? Mkuu wa Mkoa naye akitembea nyuma kuna kamera, nionekane huko, Mtukufu anione jioni kwenye taarifa, matokeo yake ni kwamba tunaua Serikali za Mitaa. Tunaendesha nchi hii kama duka. Unajua ukiwa na duka asubuhi unasema ile paketi ya sigara iliyokuwa hapa iko wapi, inatafutwa. Ndiyo hayo yanayotuletea matatizo. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilikuwa Diwani, leo Madiwani wote wazuri wanakataa kugombea na hili Mheshimiwa Simbachawene unalijua, watu wazuri wanakataa kugombea kwa sababu hawalipwi mshahara, wanalipwa posho. Leo hata ile posho ambayo wanalipwa, Mkuu wa Mkoa anaona ni shida anaenda kuwaondolea posho Madiwani wakati yeye mwisho wa mwezi analipwa mshahara. Kama yeye ni mzalendo kiasi hicho kwa nini asiache mshahara wake? Sasa hii ndiyo level ya unafiki ambayo tunaiwea hapa kwamba Mkuu wa Mkoa anataka kuondoa posho ya Madiwani wakati yeye analipwa mshahara, wao hawana mshahara na mnataka wasimamie fedha ambazo mnapeleka Halmashauri, haitawezekana. Ni lazima tuweke heshima kwa Madiwani, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili fedha zote zinazopelekwa Halmashauri zinakwenda kwenye vijiji, vitongoji, kule ndiyo kuna watu. Serikali hii ya CCM tumeimba miaka yote kwa nini hamtaki kuwalipa Wenyeviti wa Vijiji fedha kama malipo? Hakuna anayetoa majibu. Wenyeviti hawa wa Vijiji ambao wanafanya kazi kwa hisani kila siku utasikia Mkuu wa Mkoa nimekufukuza kazi, nimewaweka ndani, unawekaje mtu ndani kwa vitisho ambaye humlipi hata senti tano? Kwa hiyo, mimi nafikiri tuliangalie hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za CAG kufanya ukaguzi. Nyie wenyewe mnasema mnataka kutumbua majipu, kumbe ni unafiki mnataka kujificha madudu yenu myafichie ndani humo. Kheri Mheshimiwa Kikwete aliyeweka wazi watu wakajua, ninyi mnaficha hamtaki kujulikana maovu yanayofanywa, mnamnyima CAG fedha. Wananchi wa nchi hii wajue kwamba Serikali hii ni Serikali isiyotaka kukosolewa ndiyo maana haimpi hata CAG fedha ili aende akakague aone hawa Wakuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya mliyopeleka, walioshindwa kura za maoni za CCM madudu watakayofanya kwa miaka hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, wote mliopeleka ni wale walioshindwa kura za maoni za CCM yaani bora wangewachukua ninyi mlioshinda wakawapeleka kuwa Wakurugenzi kuliko kuchukua mtu aliyeshindwa, amekataliwa na wanachama wenzake kwamba wewe huwezi kuongoza, halafu unamchukua unampeleka eti kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri matokeo yake hajui chochote anayochotakiwa kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, sitatumia muda wangu kuharibu kwa kumjibu yule najua anachofukuzia nitaharibu sana. Naomba niendelee. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mifuko ya Hifadhi za Jamii watu wameweka fedha zao, wewe unakatwa mshahara wako unaenda pale. Leo inasemekana fedha hizi zilipopelekwa Benki Kuu mmechukua mmeenda kununulia Bombardier, mnawakataza watu kuchukua fedha zao ambazo wamehifadhi. Yaani kijana amefanya kazi mgodini, ameteseka maisha yake amehifadhi kule, anataka kujitoa au amefukuzwa kazi achukue fedha ajengee watoto wake, mnamwambia mpaka miaka 60. Mnamkataba na maisha? Akifia hapa katikati huko mtampa nani?
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa matokeo haya ya kuchukua fedha ambapo tunaendesha nchi kama duka, kila kitu mnataka kiwe centralized, Halmashauri mnaua, Mifuko ya Hifadhi za Jamii mnaingilia, kila kitu na fedha mpaka za wananchi wa kawaida mnataka muwe mnachukua kwenye mifuko yao, ni lazima ikome.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakusukuru kwa sababu hata nikianza hii hoja hautanivulimia, ahsante.