Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru wa kupata nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia machache ambayo ninayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nianze kwa kuzipongeza Kamati zote mbili kwa taarifa nzuri ambazo zimetolewa. Kwa kweli ni nzuri sana na naamini kama Serikali itazifanyia kazi basi hali itakuwa ni nzuri. (Makofi)
Mheshimwa Naibu Spika, suala la pili ambalo napenda kuchangia ni kuhusu taarifa za Mkaguzi Mkuu (CAG). Kwanza CAG ndiyo mwakilishi wa Bunge hili, ndiyo jicho la kwenda kuangalia kukoje huko katika taasisi zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaenda haraka haraka kwa sababu ya muda, chukulia ripoti ya Serikali Kuu ya mwaka huu. Katika ripoti ya mwaka 2014/2015, katika Serikali Kuu taasisi 18 zilipata hati yenye mashaka na taasisi moja ilipata hati isiyoridhisha kwenye Serikali za Mitaa ndiyo inatisha. Ukiangalia kwenye Serikali za Mitaa mwaka 2011/2012 hati zenye mashaka zilikuwa 29, hati isiyoridhisha ilikuwa moja na hati chafu ilikuwa moja. Mwaka 2014/2015 kwenye Serikali za Mitaa ndiyo kunatisha, hati zenye mashaka 113, hati zisizoridhisha tatu na hati chafu moja, hii maana yake nini? Maana yake hali siyo nzuri katika taasisi zetu katika kusimamia fedha za umma na hapo lazima Serikali ichukue hatua stahiki kuhakikisha kwamba tunazuia hii hali ambayo ipo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hati yenye mashaka maana yake ni kwamba vitabu na hesabu zilizopo hazioneshi sura halisi ya taasisi. Sasa kama hivyo ndivyo ilivyo tusipochukua hatua hali itaendelea kuwa mbaya katika taasisi zetu. Naishauri Serikali yangu tuendelee kuchukua hatua stahiki ili tuhakikishe mambo yanakuwa mazuri katika miaka inayokuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu ambalo nataka nilizungumzie ni kuhusu taasisi chache ambazo zinafanya kazi kama TRA. Zipo taasisi ambazo zenyewe zinazalisha, zinafanya biashara, zinanunua raw material, zina-process goods halafu zinaenda kuzalisha zinauza kama TANESCO na zinginezo. Hata hivyo, zipo taasisi zinazofanya kazi kama TRA kwa mfano EWURA na TCRA hawana gharama zingine za uzalishaji zaidi ya tozo, zile tozo ni mali ya Serikali, lazima Serikali iweke mkono wake kuhakikisha kwamba zinaingia katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Hiyo ndio itakayoongeza mapato. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la nne, kwa sababu ya muda nakwenda haraka haraka lakini nizungumzie matatizo ambayo yamejitokeza. Labda niweke taarifa vizuri, nimesikia watu wameliongelea suala la Lugumi labda pengine niweke taarifa vizuri. Kwanza niseme mimi ndiyo nilikuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Lugumi iliyokuwa inashughulikia huo mkataba. Katika mkataba ule hadidu za rejea ilikuwa ni moja kwenda kuangalia kama ile mitambo ilinunuliwa na kufungwa, ndiyo ilikuwa kazi yetu. Hatukuwa na kazi nyingine zaidi ya hiyo na tulizunguka nchi nzima, Mikoa yote, Wilaya zote tukathibitishe kama zilinunuliwa na kufungwa. Naomba niweke rekodi sawa kwamba tulikuta kwa asilimia karibu 99 vilinunuliwa na kufungwa. Kilichokuwepo kwenye taarifa ya CAG alisema katika vituo vyote vile ni vituo 14 tu ndiyo mitambo ilikuwa inafanya kazi zake sawasawa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilithibitishie Bunge lako hili hata Kamati Ndogo ilipoenda ilikuta ni vituo 15 ndiyo vilikuwa vinafanya kazi yake sawasawa. Hiyo ndiyo iliyokuwepo kwenye ripoti ya Kamati yetu. Kama vituo 15 vinafanya kazi yake sawasawa kulikuwa na tatizo gani? Ile mitambo ina kazi tatu, kazi ya kwanza ilikuwa ni kuchukua picha na maelezo ya wahalifu; kazi ya pili ilikuwa ni kuhifadhi kumbukumbu zile kwenye njia ya electronic na kazi ya tatu ilikuwa ni kutuma sasa zile taarifa kwenye mitandao ili kuweza ku-share na vituo vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nataka niliambie Bunge lako vizuri kwamba katika kazi ya kwanza na ya pili ilikuwa haihitaji kabisa mtandao wa internet. Hapa ndipo Kamati ilikuwa inauliza kama vifaa vyote hivi vilinunuliwa ni kwa nini sasa vilikuwa havitumiki kufanya kazi ya kwanza na ya pili, ndiyo swali lililokuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nilichotaka kusema ni kwamba mitambo yote ilinunuliwa, imewekwa lakini ilikuwa haijaanza kutumika. Hiyo ndiyo hoja ambayo tunayo kwenye Kamati na naomba ieleweke hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa muda huu.