Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa maendeleo uweke kipaumbele suala la maji na miundombinu katika Mkoa wa Lindi. Mkoa wa Lindi unakabiliwa na tatizo kubwa la uhaba wa maji safi, takribani asilimia 85 ya wananchi wa Mkoa wa Lindi hawapati maji safi kupelekea kunywa na kutumia maji ya mito na mabwawa pamoja na wanyama. Kitu cha kusikitisha zaidi hospitali ya Mkoa wa Lindi nayo ina tatizo la uhaba wa maji safi kupelekea wagonjwa kuletewa maji ya vidumu kutoka majumbani.
Hii ni hali mbaya inayopelekea wagonjwa kuwa hatarini kupata magonjwa ya mlipuko, nilitegemea mpango wa maendeleo ungekuwa na mipango ya miradi mbalimbali ya maji katika Mkoa wa Lindi na maeneo yote nchini ambako kunakabiliwa na tatizo la maji.
Miundombinu ilipaswa ionekane kwa mapana katika mpango wa maendeleo kati ya mwaka 2012 - 2015 shilingi bilioni 6.4 zilitengwa kwa ajili ya ukarabati wa barabara yenye urefu wa kilomita 230 inayotoka Nangurukuru kuelekea Liwale. Hali ni hiyo hiyo katika barabara ya Nachingwea – Liwale. Serikali iweke mpango wa kuzijenga hizi barabara katika kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu elimu; Serikali haijaainisha ina mpango gani juu ya wanafunzi waliofaulu kwenda Vyuo Vikuu, mpaka dakika hii hakuna kinachoeleweka juu ya wengi na hawa wanafunzi waliofaulu vizuri na kukosa mikopo. Serikali itambue kwamba elimu inaelekea kuanguka kama haitoandaa mpango wa kueleweka juu ya mikopo ya elimu ya juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu afya; nchi nzima inakabiliwa na tatizo kubwa la uhaba wa dawa katika hospitali, vifaa tiba na chanjo. Hii imejikita katika Wilaya zote za Mkoa wa Lindi na maeneo mbalimbali nchini. Huu mpango ulipaswa uoneshe maboresho katika sekta ya afya, akinamama na watoto wanaendelea kupoteza maisha yao wakati wa kujifungua kwa kukosa vifaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kilimo; mpango wa maendeleo umekosa shirikisho la soko la mazao kwa wakulima wa mazao mbalimbali kama ufuta, mbaazi na kadhalika. Ni vema Serikali ingepanua wigo kwa wakulima kwa kuwatafutia masoko.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mawasiliano; mpango wa maendeleo uzingatie suala la kuhakikisha hata maeneo yote nchini yanapata mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la uchumi; uchumi unaendelea kuanguka na matumizi kuongezeka hata baada ya wafanyakazi hewa kutambulika. Watumishi wengi wamesimamishwa kupeleka kila mwezi wanaendelea kupokea mishahara. Halmashauri zifikishiwe pesa kwa wakati kwa kutekeleza maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliahidi elimu bure kwa wanafunzi, lakini hii haijaainishwa katika mpango wa maendeleo, kwani elimu bure haina maana yoyote kama wazazi bado wanaendelea kutoa michango. Pia kumekuwa na ucheleweshaji wa pembejeo, mpango huu ungeainisha ni kwa kiwango gani Serikali itahakikisha wakulima wanafikishiwa pembejeo kwa wakati.