Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Jumanne Kibera Kishimba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KIBERA J. KISHIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri pole sana kwa misukosuko unayopitia. Uchumi ni soko gumu sana hasa uchumi wa dunia ya tatu na nchi maskini kama Tanzania na hasa kuwatoa kwenye maisha waliyozoea kwa miaka 25 ni kama kumwachisha mtoto ziwa, lazima kuwe na mgogoro mkubwa, vuta subira!
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu, kwanza ni maoni kuhusu Serikali kuruhusu madini yetu na ya nje ambayo yanazalishwa na wachimbaji wadogo yawe asilimia zero wakati wa kuingia, kutoka iwe asilimia moja, itatusaidia sana kama nilivyochangia kwenye mchango wa bajeti mwezi wa Saba ulio kwenye Hansard ya Bunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wa Kariakoo ni wachangiaji wazuri wa uchumi kwenye importation, lakini tatizo lao kubwa liko kwenye vitu viwili: Suala la TBS kwa product ambazo siyo chakula. Mfano, Redio ya sh. 5,000 wanataka iwe na ubora, lakini wananchi wananunua na wanasikiliza habari au muziki; wanawasumbua na ukizingatia mali nyingi inanunuliwa na watu wa Malawi, Mozambique, Zambia, Congo na majirani wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tariff kwa bidhaa kwa mfano, Colgate gram 100 inauzwa sh. 2,000, Colgate herbal 100 inauzwa sh. 8,000. Kwenye tariff zinaitwa (Toothpaste) TRA anavyothamini ni sh. 8,000, muagizaji kaagiza kwa sh. 2,000, hapo ndipo mzozo unazuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kufikiria upya suala la license kwenda kwenye mafuta ili kukusanya fedha kwenye ma- grader, tractor, generator na mashine nyingi, zitapunguza pia rushwa za barabarani.