Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, mapato, kutokana na ongezeko la mapato shilingi trilioni tatu nukta nne kuna haja ya Serikali kuangalia maeneo mengi zaidi ili kuongeza mapato kama ifuatavyo:-
(i) Kupitia upya tozo mbalimbali zisizo za kodi katika Serikali na Taasisi zake ambazo hazijapandishwa kwa muda mrefu.
(ii) Kushawisha Kampuni nyingi kuandaa mahesabu badala ya kuwa katika mlipa kodi asiyeandaa hesabu.
(iii) Kufuatilia aina zote za kodi kuwa zinatumika ipasavyo. Mfano stamp duty on contracts. Kodi hii kampuni nyingi hazilipi.
(iv) Ripoti ya kuboresha mapato “CHENGE ONE AND TWO” itumike ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo; Serikali itoe kipaumbele zaidi katika kilimo kwani mchango wake ni mdogo wa asilimia 2.9 wakati lengo ni asilimia sita hivyo suala la pembejeo lipewe kipaumbele hususani ruzuku ili kilimo cha jembe la mkono kiondoke kama ilivyoahidi Serikali. Tumbaku bado tuna tozo nyingi na mkulima ananyonywa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tozo katika mafuta sh. 50, tunaomba Serikali iweke sh. 50 kwa lita ili kukidhi mahitaji ya wananchi juu ya maji vijijini na zahanati kwa kuwa uwezo wa halmashauri nyingi ni mdogo hivyo bajeti ya 2017/2018 Serikali ikubali ombi hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti ya Bunge, kutokana na changamoto za utendaji 2016/2017 tunahitaji Waziri ahakikishe kuwa bajeti ya shughuli za Bunge iongezwe kwa kiasi kikubwa kukidhi shughuli za Bunge kwa mujibu wa katiba angalau 130 bilioni.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi inayoendelea, Serikali ihakikishe miradi hii inakamilika ili kupunguza gharama. Tunaomba barabara ya Sumbawanga-Mpanda, Manyoni-Itigi-Tabora na Sitalime-Mpanda zikamilike 2017/2018. Pia Shirika la Reli lipewe pesa kuboresha mabehewa na ofisi ili usafiri utumike mwaka mzima hata masika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikataba ya msamaha; tunaunga mkono hoja ya kupitia upya mikataba hii ya msamaha wa kodi na kuwezesha Serikali kuongeza mapato pia kusaidia zaidi wakulima kufanya kilimo cha kisasa.
Mheshimiwa Mweyekiti, ubia katika uwekezaji; zoezi la uwekezaji katika ubia lipewe muda maalum ili kuharakisha maendeleo kwa wananchi hususani wawekezaji wa ndani wenye uwezo wapewe kipaumbele.