Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya maskini – Mpango ueleze namna ambavyo wilaya maskini zitasaidiwa kutoka kwenye lindi la umaskini kama ilivyotangazwa kwenye Bunge la Bajeti 2016. Wilaya ya kwanza ni Kakonko ikifuatiwa na Biharamulo. Wilaya hizi zisaidiwe kwenye kilimo (pembejeo za bei nafuu kwa wananchi wote), ufugaji, mabwawa ya samaki, viwanda, vidogo vidogo vya kuchakata mihogo, ujasiriliamali na elimu yake. Wilaya hizi zisipopata boost ya kiuchumi zitaendelea kurudisha nyuma uchumi wa nchi (overall).
Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara; zipo barabara za Kidahwe hadi Nyakanazi zitengewe fedha za kutosha. Aidha, ikumbukwe Manyovu-Kasulu hadi Nyakanazi, pia barabara ya Sumbawanga-Mpanda-Nyakanazi, kwa nini zisitajwe hivi:-
(i) Manyovu-Kasulu-Kibondo-Kabingo (mpya)
(ii) Sumbawanga-Mpanda-Uvinza-Kasulu (mpya)
Mheshimiwa Naibu Spika, Nyakanazi-Kabingo inaendelea, bajeti iwepo, Kidahwe-Kasulu-Nyakanazi iendelee kutengewa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, Pato la Taifa; hali ya pato la Taifa kukua litafsiriwe kwenye hali nzima ya maisha ya Watanzania. Haiwezekani pato la Taifa limekua, wananchi wanabakia maskini, karibu Watanzania milioni 20 ni maskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tozo na Kodi; kumekuwa na tozo nyingi kwa wajasiriamali na shughuli zao. Mfano tozo za mazao kama korosho, kahawa na kadhalika wajasiriamali wadogo kama bodaboda wametozwa ushuru wa parking; parking fee. Kodi mbalimbali za bandarini zipunguzwe ili zivutie wawekezaji wengi kuja Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wamezuiliwa kukata leseni za biashara za halmashauri na kuamriwa wakalipe mapato TRA jambo ambalo limewafanya washindwe kufanya biashara hivyo kupotea kwa mapato ya halmashauri/Serikali Kuu. Mfano mfanyabiashara mwenye mtaji wa laki mbili anataka kufungua biashara ndogo anaenda TRA anatakiwa alipe kodi ya laki moja nukta tano kitu ambacho hakiwezekani.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushuru juu ya mapato kuongezeka; mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara. Hali ya kisasa iwe nzuri isiyodhibiti demokrasia nchini. Utulivu wa kutosha usioleta shaka/hofu kwa wawekezaji. Mfano, Serikali ya CCM na kuwakataza wapinzani kufanya mikutano ya hadhara na hivyo nguvu kubwa kutumika kudai demokrasia hiyo. Hili linawaweka wawekezaji katika hofu na wasiwasi, kuleta mitaji inaleta mashaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira rafiki kibiashara zipunguzwe zinazoleta urasimu wa kusajili biashara na kufanya biashara. Mfano, Mfanyabiashara haruhusiwi kufanyabiashara kwa muda hata wa miezi mitatu ndipo aanze kulipa kodi/ushuru. Vivutio vizuri vitawezesha wafanyabiashara wengi kuingia na hivyo Serikali kupata mapato makubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, bandari; ni kosa kubwa kuwa na bandari tatu kubwa nchini halafu nchi inakuwa maskini. Bandari ya Dar es Salaam isiwekwe kodi nyingi zisizo na tija kwa wafanyabiashara na zinazosumbua wananchi. Bandari ifanye operations zake electronically ili kupunguza muda wa kutoa mizigo bandarini kama vile malipo all financial transactions na zionekane kila upande TRA- Bandari.
Mheshimiwa Naibu Spika, uvuvi, Sekta iimarishwe ili kuuza samaki wengi ili kuweza kuuzwa nje na ndani ya nchi. Mfano, zinunuliwe meli za uvuvi wa baharini na maziwa kama vile Victoria na Tanganyika, meli zivue samaki wanaoshindikana kuvuliwa kwa sababu ya poor fishing gears.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo; mazao ya biashara na chakula yalimwe kitaalam kwa kutumia mbolea na mbegu bora. Kilimo cha umwagiliaji kisisitizwe ili kuepuka njaa kwa sababu ya ukame. Iteuliwe mikoa/wilaya za umwagiliaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, gesi; nchi yoyote yenye gesi asilia haitakiwi kuwa maskini, tuuze gesi kwa wananchi kwa bei nzuri affordable ili kuokoa misitu yetu itakayotuletea mvua. Tuuze gesi nje ya nchi kupata fedha za kigeni tuuze umeme unaotokana na gesi kwa nchi jirani.