Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo kimepungua hadi 2.7% wakati malengo yalikuwa kikue kwa 6%. Hii inaleta wasiwasi hasa kwa wanawake ambao ni wengi katika sekta hii. Sekta hii ni muhimu sana kwani wanawake ni wadau wakubwa sana na mpango huu umejikita kwenye viwanda, hivyo kilimo kiwekewe kipaumbele cha 100% ili kiakisi na viwanda na wakati huo kitaleta tija kwa viwanda vyetu. Maskini wengi wako vijijini ambapo wengi ni wanawake.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfumuko wa bei; mwaka 2011 mfumuko wa bei ulikua kwa 19.8%, mwaka 2015 ulishuka kufikia 5.6%, hii ilikuwa sawa lakini kwa sasa imefikia tena 19% na kuleta mkanganyiko kwa jamii maskini. Mfumuko wa bei una madhara mengi kwa jamii hasa wanawake. Nashauri mfumuko ubaki kwenye tarakimu moja kwa kadri inavyowezekana na ikibidi wanawake wakingwe kwa gharama yoyote. Iwepo mipango mahsusi ya kupeleka maendeleo kwa wanawake kwenye vikundi vyao mbalimbali ili kuweza kuzalisha mali kwa maendeleo yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nguvu kazi ya utaalam; kuna upungufu mkubwa wa takwimu zilizochambuliwa kwa mtazamo wa kijinsia. Maeneo ya miradi mikubwa ya kiuchumi kama miradi ya Mchuchuma na Liganga ingepewa watu mahsusi na kuzingatia jinsia kutoa wataalam.