Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mpango wa Maendeleo ni wa muhimu katika maandalizi ya kutayarisha bajeti ya Taifa, nampongeza sana Waziri wa Fedha, Naibu Waziri pamoja na Wizara ya Fedha kwa kazi nzuri ya kuandaa Mapendekezo ya Mpango wa Taifa kwa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ushauri; katika ukusanyaji wa Mapato Serikali iongeze juhudi ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara ili kuelewa kuwa kulipa kodi si adhabu ni wajibu wa kila mfanyabiashara. Ili kufikia lengo la kukusanya mapato ya Shilingi trilioni 32.946, Serikali inatakiwa kuhakikisha mikakati ya ukusanyaji kodi kutoka vyanzo mbalimbali kuwa wazi kwa kila mtu na kujua Serikali ina malengo makubwa ya kuboresha huduma za jamiii kama vile kuboresha miundombinu ya maji, barabara, afya, nishati na elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika matumizi ya bajeti kwa mwaka 2017/2018 lazima pawepo na uwazi wa matumizi ya bajeti kwa wananchi wetu ili kuepuka malalamiko yasiyo ya lazima.
Mheshimiwa Naibu Spika, TRA watoe elimu kwa Watanzania juu ya utaratibu unaotumika katika ukusanyaji wa kodi, pia kujua aina ya kodi ambazo mfanyabiashara anatakiwa kulipa. Fedha ya maendeleo katika Halmashauri zetu zipelekwe kwa wakati bila kuchelewa ili kukamilisha miradi ambayo imepangwa. Pia Serikali iwe makini sana na miradi ambayo ipo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambazo ni ahadi za Mheshimiwa Rais wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunategemea mwaka 2017/2018 Miradi ya maji, barabara, afya, itaendelea kutekelezwa kwa kufuata Bajeti ya Taifa na miradi ya kipaumbele ni ile ya ahadi ya Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.