Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaamini kwamba mtengamano wa kisiasa ni nguzo moja muhimu katika kujenga nchi yenye maendeleo makubwa na ya uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mtengamano wa kisiasa unajumuisha siasa safi za kiustaarabu na zenye kuheshimu mawazo ya kila mmoja ili kukidhi katika kufikia demokrasia ya ukweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi washirika, ambayo ni wadau wakuu wa kusukuma maendeleo katika nchi yetu tayari wameanza kurudi nyuma kwa kukosekana sifa nilizozielezea hapa juu hasa baada ya Serikali ya CCM kuendeleza ubabe wake kwa kutoheshimu maamuzi ya Wazanzibari waliyoyafanya kwenye uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba, 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa miujiza gani Mheshimiwa Waziri wa Fedha anaweza kufanikisha mipango yake ya kuimarisha uchumi wa nchi hasa baada ya kukosekana mtangamano wa kisiasa hapa nchini kwetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya maamuzi ya kuhamishia Makao Makuu ya Serikali katika Mkoa wa Dodoma, kwa kile kinachoaminika kama ni katikati ya nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Dodoma ni katikati kwa Tanzania Bara na sio kwa Tanzania nzima. Kwa kupunguza usumbufu kwa Wazanzibari wa kufuatilia matatizo yao Dodoma, naishauri Serikali kwamba Wizara zote za Muungano zibakie kule kule Dar es Salaam na zile zisizo za Muungano ndizo zihamishiwe Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2015/2016, Serikali imetoa mafunzo katika fani za mafuta na gesi kwa ngazi tofauti ndani na nje ya nchi kwa wanafunzi 159. Naomba Mheshimiwa Waziri afafanue kati ya wanafunzi hao, wamo wanafunzi Wazanzibar wangapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa wanafunzi 35 wanaogharamiwa na washirika wa maendeleo ni wangapi wanatoka Zanzibar?