Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa. Nami nitumie nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuleta sote pamoja katika Bunge la mwaka huu tukiwa salama na afya njema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia katika maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza ni eneo la utumishi. Tumeona commitment ya Serikali juu ya kufanya jitihada kubwa ya kurudisha nidhamu ya Watumishi wa Umma, lakini nataka niiombe Serikali kuna two approach, kuna carrot na stick. Nimeona matumizi ya stick yamekuwa makubwa zaidi kuliko carrot mahali ambapo imefikia watumishi wetu wamekuwa waoga sana katika maeneo mbalimbali. Watu wamekuwa hawafanyi maamuzi, watu wameingiwa na hofu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeomba Wizara ya Utumishi, commitment ya Serikali kurudisha nidhamu iende na incentive package kwa watu wanaofanya vizuri na wanaofanya maamuzi katika sekta mbalimbali katika utumishi wa umma ili jambo hili liweze kuwatia moyo wale waadilifu. Hatusemi wanaofanya vibaya wasiadhibiwe. Hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili katika Utumishi ni suala la ku-develop Institutional capacity. Dhamira ya Serikali ya Rais, mimi nakubaliana sana na approach ya Rais Magufuli. When you are in crisis tumia hiyo mechanism ya crisis ku-sort out problem, wakati una develop Institution zako.
Kwa hiyo, ningeomba mwaka huu mmoja tumetumia fire approach sasa Serikali ifanye kazi kubwa ya ku-develop institutional capacity ili Mheshimiwa Rais atakapomaliza kipindi chake cha miaka kumi taasisi ziendelee. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini ni lazima tujenge capacity za Taasisi? Tunapotegemea sana uwepo wa mtu, anapokuwa hayupo tunarudi kule tulikotoka, tutakuwa hatuisaidii nchi kule tunakotaka kwenda. Kwa hiyo hili ni jambo muhimu sana la kufanya ili tuweze kutatua tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni Wizara ya TAMISEMI, nampongeza Waziri wa TAMISEMI na Naibu wake wanajitahidi, lakini wameondoa vyanzo vya mapato hasa katika Miji na Manispaa. Wajitahidi basi hata fedha za OC ziende. Kinachotokea sasa hivi fedha za OC haziendi ambazo ziko budgeted kabisa na zimepitishwa na Bunge, haziendi kwa wakati, hazifiki matokeo yake fedha za mapato ya ndani sasa zinatumika kuendesha ofisi za Hamashauri, matokeo yake zinaathiri development activity katika maeneo yetu. Kwa hiyo, hili ni jambo muhimu sana Serikali ikaangalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mtazame uwezekano wa kurudisha hivi vyanzo vya mapato ambavyo vimeondolewa kwenye Halmashauri. Kwa sababu tunapopunguzia capacity ya Halmashauri ya kifedha maana yake na tumeamua kwenda na approach ya D by D shughuli za maendeleo na hali ya uchumi kwa wananchi wetu ni ngumu. Ni muhimu sana tuone namna gani tunazipa uwezo Halmashauri zetu kutatua changamoto zinazokabiliana nazo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI kama wenzangu wamesema, TAMISEMI ni kama jalala, lakini sitaki kutumia neno jalala imeamuliwa kwamba kwa approach ya utawala tuliyochagua ni kwamba ndiyo coordination center. Leo tumeunda Tume ya Utumishi ya Walimu (Teachers Commission) imeenda TAMISEMI, ingawa mimi kwa mtazamo wangu naiona haina meno, lakini la pili kuna madai ya Walimu ambayo ni makubwa mno. Lazima tuje na mechanism ambayo itajenga hope kwa Walimu wetu kwamba madai yao haya within this span of period yatakuwa yamelipwa. I don‟t believe mpaka leo bado tunafanya uhakiki, tunahakiki mpaka lini? Hili ni jambo ambalo ni lazima tujiulize. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira imekuwa changamoto, wewe ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati yetu unaona Wizara ya Afya ikija, Wizara ya Elimu ikija, suala la ajira linavyokuwa ni mjadala mkubwa na upungufu wa watumishi hasa wa kada ya afya katika Halmashauri zetu. Mheshimiwa Simbachawene na Dada yetu Mheshimiwa Angellah Kairuki, uhakiki wameshafanya for almost one year, hebu wafungulie hizi ajira ili tuondoe watoto wetu wanao graduate mitaani tuweze kuwa-absorb katika ajira, pia tuweze kuondoa kero! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi leo by June katika Mji wa Nzega tutakuwa na zahanati 15 mpya, tutakuwa na vituo vya afya vitatu vipya, hakuna manpower! Leo Nzega tuliamua kuachana na approach ya kushusha vyeo Walimu ambao hawa-perform vizuri na kuwaadhibu, no! Tuliamua kuangalia changamoto zao. Mwaka jana matokeo ya darasa la saba Halmashauri ya Nzega ilikuwa ya mwisho Kimkoa, mwaka huu imekuwa ya pili kwa sababu tulienda ku-tackle matatizo ya Walimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana Mji wa Nzega haukuwa na division one na division two almost lakini performance ya mwaka huu kidogo ime-grow, Halmashauri ya Mji wa Nzega imekuwa ya 73. It‟s very important tukaangalia hizi crisis katika Local Government na Brother Simbachawene you have a lot of mzigo. Kwa hiyo, ni vizuri kupitia Bunge hili na nimshauri kwenye Bajeti inayokuja matatizo ya Walimu tuje na clear plan kwamba madai ya Walimu ni kiwango hiki, tutayalipa ndani ya kipindi hiki ili Walimu wetu wawe na matumaini kule walipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, TASAF. TASAF imesaidia sana watu wetu lakini umefika wakati wa approach ya TASAF kubadilika iwe ni developmental approach, kwamba fedha zinazopelekwa kwenye kaya maskini ziwe ni fedha ambazo zina wa-commit wale watu maskini kuja na miradi ya maendeleo ambayo hawa wataalam wa TASAF mwaka kesho kabla hawajakupa fedha wanaangalia performance ya mwaka jana, fedha tuliyokupa na mradi ulioanzisha. Ni muhimu Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Local Government ikafanya kazi very close na wataalam wa TASAF na Watendaji wetu wa Vijiji ili kusaidia kaya hizi maskini badala ya kupewa fedha kwenda kula ziwe fedha za investment ili tuweze kuondokana na umaskini katika Local Government. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesikia hoja ya asilimia 10 nataka Serikali itafakari. Tuna asilimia 10 katika Halmashauri, tuliahidi kwenye Ilani shilingi 50 million ya kila kijiji. Tuna fedha za Mfuko wa Uwezeshaji, hizi fedha ziko scattered katika maeneo mengi. Umewadia wakati kama Serikali itazame hizi fedha ambazo zina target kwenda kukopesha vijana na akinamama tuziwekee proper framework kisheria ili ziweze kufikia watu kwa wakati. Ukichukua milioni 50 ya kila one basket halafu tukachukua fedha za uwezeshaji zinazowekwa Wizara ya Mheshimiwa Jenista, fedha hizi tukazitengenezea sheria zitatusaidia sana kuondokana na changamoto za financing kwa watu wetu maskini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja.