Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami kwanza nichukue fursa hii kushukuru kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia na nitaanza na TAMISEMI. Kwa mujibu wa taratibu zilizopo Serikali zipo za aina mbili, kuna Central Government na Local Government, lakini sasa kuna kitu au utaratibu ambao umeanzishwa wa kuondoa makusanyo ya property tax ambacho kilikuwa ni chanzo cha mapato katika Halmashauri zetu tumekipeleka katika Serikali Kuu kwa kukusanywa na TRA. Naona hili ni kama kuzizika Serikali za Mitaa, kwa hiyo nakumbusha kwamba Serikali za Mitaa ndizo zinazoziba aibu ya Serikali Kuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na miradi mingi ambayo inatekelezwa na Serikali za Mitaa, kwa mfano uchongaji wa barabara za vijijini, miradi ya maji vijijini, pamoja na kwamba inapelekewa fedha na Serikali Kuu lakini bado wenye mamlaka ya kusimamia ni Serikali za Mitaa. Sasa kuzinyang‟anya Serikali za Mitaa chanzo hiki cha property tax ni kuziua Serikali hizo. Kwa hiyo, nashauri kwamba ikibidi property tax irudishwe katika Serikali za Mitaa kama kweli tunataka miradi ya wananchi inayofika moja kwa moja katika Halmashauri zetu iweze kusimamiwa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna suala zima la mapato, leo ukienda kwenye Halmashauri zote zipo hoi kimapato, baada ya kunyang‟anywa chanzo kile zimekuwa kama zimechanganyikiwa, zimekuwa zikitegemea tu kupata ruzuku kutoka Serikali Kuu ambayo nayo inacheleweshwa, inaletwa katika robo ya mwisho ya Mwaka wa Fedha wa Serikali, matokeo yake sasa inafanywa miradi kwa kukurupuka, miradi mingi inakuwa chini ya viwango na hapohapo pia ndipo watu wanapopiga „dili‟. Nashauri bado tuzitazame sana Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tukumbuke pia Serikali za Mitaa kama alivyotangulia kusema mmoja imekuwa ni kama jalala, mizigo yote imesukumwa kwenye Serikali za Mitaa; elimu ya msingi na sekondari zinasimamiwa na Serikali za Mitaa, miradi ya maji vijijini inasimamiwa na Serikali za Mitaa na miradi mingine ya afya bado inasimamiwa na Serikali za Mitaa. Hata hivyo, tukija kwenye elimu kwa mfano, elimu kwa mujibu wa utaratibu siyo biashara ni huduma, lakini kuna utaratibu ambao umeanzishwa tena wa kukusanya mapato kutoka kwenye hizi English Medium Schools, matokeo yake sasa wamiliki wa shule nao kwa kuwa wanatozwa fedha nyingi, wanaongeza ada matokeo yake wananchi au wazazi wanashindwa kuwapeleka watoto katika hizi shule za English Medium. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Serikali, ikibidi tuondoe hii tozo ya kodi katika hizi shule za English Medium, vilevile pia hata kwenye sekondari. Tunasema hapa elimu bure lakini ukiangalia, kwa mfano katika sekondari kumesamehewa sh. 20,000 tu ya ada, vikorombwezo vyote bado mzazi anatakiwa kulipia, tena baya zaidi kunatakiwa counter books, counter book moja sh. 5,000 mtoto anatakiwa atumie zaidi ya counter books 12, hapohapo tena kuna nguo za michezo, kuna uniform, viatu pair mbili, majembe, tumewasaidia tu kuondoa hilo suala la madawati baada ya fedha iliyobaki katika Bunge kuingiza fedha hiyo kwenye madawati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Halmashauri napo labda nimpongeze tu Mheshimiwa Rais kwa hili suala la kumaliza tatizo la madawati lakini bado elimu bure siyo bure. Katika baadhi ya shule wanashindwa hata kulipa walinzi, wanashindwa hata kulipa maji, wanashindwa hata kulipa umeme! Hebu fikiria watoto wanashinda kutwa nzima lakini maji yamekatwa, yote hii inatokana na kutamka kwamba elimu itakuwa bure lakini siyo bure kwa asilimia mia moja. Nashauri Serikali kama tumeamua elimu iwe bure basi iwe bure kwelikweli kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kingine pia naishauri Serikali, TAMISEMI haina uwezo wa kulipia maji na umeme katika shule zetu za sekondari, sasa ikibidi shule za sekondari, shule za msingi, taasisi za kidini kama makanisa na misikiti, hili naona pia tungeondoa kabisa hilo suala la kuzichaji masuala ya bili ya umeme na maji tusiwe tumependelea, ili taasisi na shule hizi ziwe zinatumia maji pasipo malipo, tutasaidia kupunguza mzigo kwa wazazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ni kawaida kwamba hata inapotokea kukiwa na majanga tunatumia viongozi wetu wa kidini kumwomba Mwenyezi Mungu aisalimishe nchi yetu na majanga na matatizo mengine sasa je, tunasaidiaje taasisi za kidini. Nashauri kupitia shule za msingi na sekondari pamoja na taasisi za kidini hizi tuondoe haya masuala ya malipo ya maji na umeme ili kama tunasema elimu bure iwe elimu bure kweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine katika elimu natoa ushauri hata shule za private za sekondari tumekuwa tunawatoza kodi kubwa sana, matokeo yake na wao wanaongeza school fees ambayo imekuwa sasa ni kilio kwa wananchi. Waheshimiwa Wabunge wenzangu watakuwa ni mashahidi, kila Mbunge hapa ana orodha ya watoto siyo chini ya 20, wote wamefaulu wazazi hawana uwezo unatakiwa Mbunge uchangie, utachangia watu wangapi? Naishauri Serikali elimu iwe bure kama katika baadhi ya nchi za wenzetu, wenzetu wanawezaje sisi tushindwe, upo usemi unaosema wao waweze wana nini, sisi tushindwe tuna nini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala zima la Katiba na Sheria; mimi niliipitia taarifa hii lakini kuna baadhi ya maeneo naomba yafanyiwe marekebisho kidogo, kwa mfano, Waheshimiwa Wabunge wenzangu watakuwa mashahidi, sote katika Wilaya zetu kuna Magereza, ukiwa ni mwenyeji wa kutembelea Magereza utakuta kuna akinamama ambao wana watoto wachanga wananyonyesha. Mama ndiye amefanya kosa labda ameiba, labda amefanya kosa lingine huko ametiwa hatiani, lakini mtoto mchanga anayenyonyeshwa ambaye hawezi kuishi bila mama yake inabidi naye ageuke mfungwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naishauri Serikali, kwa wale akinamama ambao wengine ni wajawazito wanajifungulia kule gerezani, lakini na kwa wale akinamama wote ambao watakuwa wana watoto wachanga, hawa watoto dini zote zinaamini kwamba mtoto mdogo kuanzia miaka 14 kuja chini ni malaika, kwa nini tumtese malaika huyu akae gerezani hali ya kuwa yeye hakufanya kosa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, kama mama ana mtoto mchanga basi ama asamehewe apewe kifungo kile cha kufanya kazi za kijamii kama kusafisha hospitali, ofisi ya Mkuu wa Mkoa au Mahakama, lakini kitendo cha kuwafanya watoto wachanga wawe wafungwa, hawapati haki za watoto za kucheza na watoto wenzao, hawapati muda wa kujinafasi, lakini pia mama zao wanakuwa wanyonge wanaona kwamba mimi nimekosa, mtoto wangu naye anafungwa amekosa nini. Naishauri Serikali tuangalie mtindo mwingine wa kuwafikiria hawa watoto ambao mama zao wamekuwa wafungwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la Sheria na Katiba kuna kipengele hiki tumekipitisha hapa cha kwamba wasaidiwe wale wasiokuwa na uwezo. Mimi naomba hili jambo kwa mujibu wa utaratibu wa kisheria tuliangalie vizuri, kwa sababu ni watu wengi ambao wana kesi hawana uwezo wa kuweka Mawakili, vilevile pia kuna suala zima la ajali. Nchi nyingi zilizotuzunguka inapotokea ajali wahanga wa ajali wanaokufa ama wanaopata vilema vya maisha, utaratibu katika baadhi ya nchi Mawakili wa Kujitegemea wanakwenda hospitalini au wanakutana na familia za wale wahanga wanaweka makubaliano, kwamba kwa sababu mtu wenu amefariki, ameacha wajane na watoto yatima, sisi tutaisimamia kesi ya compensation, kwamba huyu mtu alipwe fidia ili aweze kusomesha watoto wake ambao wamebaki yatima au kama ana mjane au wagane waweze nao kupata haki yao ya malipo yanayotokana na insurance, lakini nchini kwetu…………
MWENYEKITI: Ahsante.