Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia taarifa ya Kamati ya Bajeti.
Mheshimwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kuishukuru Kamati ya Bajeti kwa kutuletea taarifa nzuri ambayo imefanya uchambuzi mzuri juu ya hali ya utekelezaji wa bajeti ya Serikali.
Mheshimwa Mwenyekiti, naomba kwanza kuipongeza Serikali kwa malengo mazuri ya mwaka huu wa fedha wa 2016/2017 Serikali ilitenga asilimia 40 ya bajeti iweze kwenda kwenye miradi ya maendeleo. Mipango hii ni mizuri na imelenga kuwasaidia Watanzania waweze kupata maendeleo ambayo tuliwaahidi katika utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, zipo changamoto na ndiyo maana nimeishukuru Kamati ya Bajeti kwamba wamejitahidi sana kutathmini changamoto hizi na sisi tuna wajibu wa kuzijadili na kuishauri Serikali, bahati nzuri tupo kwenye midterm review ya bajeti. Kwa hiyo, nina imani kwamba Serikali ni sikivu na mapendekezo haya ambayo Kamati imetoa na Waheshimiwa Wabunge watatoa yatafanyiwa kazi ili tunavyokwenda kwenye second half ya utekelezaji wa bajeti ya Serikali hizi changamoto zifanyiwe kazi na baadhi ya changamoto ziwe carried over kwenye bajeti inayofuata.
Mheshimwa Mwenyekiti, naomba nianze na Deni la Taifa, nianze kwenye ukurasa wa tatu wa taarifa ya Kamati ya Bajeti, ninukuu kuhusu mwenendo wa miradi ya maendeleo hasa hasa michango ya washirika wa maendeleo. Kwenye ukurasa wa tatu mwisho kabisa; “mwenendo wa utoaji wa fedha za washirika wa maendeleo unaonesha ni upungufu kwa asilimia 26 ya fedha yote iliyotarajiwa kutolewa. Kamati haikupata majibu ya kuridhisha kuhusu sababu za washirika wa maendeleo kutotimiza ahadi zao kwa asilimia mia moja.”
Mheshimwa Mwenyekiti, kusema ukweli na mimi nipo concerned sana; tumeweka malengo mazuri, tume-target asilimia 40 ya bajeti iende kwenye fedha za maendeleo na hivi sasa tumefika kwenye nusu ya mwaka wa bajeti kwa asilimia kubwa fedha za maendeleo tulitegemea hao wahisani watakapotoa fedha ndizo tutumie kwenye kufadhili miradi ya maendeleo. Ukiangalia ukusanyaji wa TRA, ukichukua ile trilioni takribani 1.2 kila mwezi ya TRA inayokusanya ukalipa mishahara ya watumishi (wage bill), ukalipa madeni ya Taifa, chenji inayobaki ni kidogo mno. Tulitegemea wahisani wakitoa fedha za maendeleo ule mchango wao tutaunganisha na ile chenji inayobaki kwenda kufanya kazi za maendeleo. Wahisani kwa vile hawatoi hizi fedha kwa kweli mimi naona tupo kwenye state of emergency, its very alarming kwamba tupo kwenye midterm review lakini hatujapata fedha ambayo tulitarajia wahisani watupatie ili tuweze kutekeleza miradi ya maendeleo.
Mheshimwa Mwenyekiti, nini kifanyike? Ukiangalia madeni ya Taifa hayaepukiki ni lazima yalipwe. Ukilipa Deni la Taifa kwa sababu asilimia kubwa tunalipa nje hii fedha tunayolipa inaenda kusaidia ku-stimulate uchumi wa kule. Kwa hiyo, ukienda mtaani ndiyo maana unakuta wananchi wanasema hali ya uchumi ni ngumu ni kwa sababu fedha nyingi tunazokusanya zinaenda kulipa madeni ya nje na ina-stimulate uchumi wa kule na siyo uchumi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, hii ni changamoto kubwa, nipende kushauri Wizara ya Fedha labda sijui tufanye road show kwenda kuongea na taasisi za fedha za Kimataifa. Tuangalie ni namna gani tunaweza tukapata fedha za maendeleo kwa sababu local revenue collection ya TRA tayari ina commitment ya wage bill na madeni ya Taifa, sasa tunafanyaje ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa.
Mheshimwa Mwenyekiti, siyo mbaya Wizara ya Fedha ikakaa ikaangalia realistically kulingana na picha iliyopo hivi sasa na bajeti ambayo tulipitisha tunafanyaje ku-adjust ili utekelezaji wa hii bajeti uwe realistic na hali ilivyo ukizingatia wahisani wamekuwa wagumu katika kuchangia asilimia zao ambazo tunatakiwa kupata.
Mheshimwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya hitimisho tungependa kujua kwa upande wa Wizara ya Fedha tupate maelezo wanafanya nini ili kukabiliana na hii hali.
Mheshimwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la makadirio ya Pato la Taifa. Ukiangalia drivers za mapato na changamoto za maafa ambazo zimetupata, kwa mfano, kwa Halmashauri ambazo zilitegemea kukusanya mapato kwenye kilimo, hivi sasa kwa sababu ya ukame mapato yatapungua. Kwahiyo, hii pia inaendelea kuweka presha kwenye ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo tulikadiria kwamba yakipatikana ndiyo yasaidie katika kutekeleza bajeti. Kwa hiyo, unaona kwamba issue inazidi kuwa serious, yale mapato ya ndani kuna changamoto zake na mapato ambayo tulitegemea kutoka nje wahisani hawatoi, kwa hiyo hii changamoto is a serious case.(Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, niende kwenye sekta ya kilimo; wote tunakubaliana kwamba sekta ya kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi wetu hasa hasa kwa upande wa Watanzania wengi wanajishughulisha kwenye hii sekta. Kwenye mpango wa maendeleo wa miaka mitano tulichangia, Waheshimiwa Wabunge tukatoa mapendekezo yetu, lakini ikija kwenye utekelezaji bado naona kuna changamoto. Kwa sababu ukiangalia hata fedha ambazo zimeenda kwenye bajeti ya sekta ya kilimo ni kidogo. Ukiangalia ukuaji wa sekta ya kilimo mwaka wa fedha wa 2014/2015 sekta ya kilimo ilikua kwa asilimia 3.4; mwaka 2015/2016 asilimia tatu.
Sasa hivi changamoto ambazo tumezipata za ukame na mabadiliko ya tabianchi sitashangaa tukipata takwimu za mwaka wa fedha 2016/2017 sekta ya kilimo itakuwa imeshuka zaidi. Sasa kwa sababu tuna malengo ya kuwapeleka watanzania kwenye middle income country status, kuna kila haja katika midterm review ya bajeti hivi sasa kuangalia ni namna gani tunakwenda mbele. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, asilimia 70 ya Watanzania wanategemea sekta ya kilimo; nilitegemea kwenye mpango wa Serikali tuangalie ni namna gani tunamsaidia mkulima. Kwenye upande wa pembejeo; pembejeo ambazo tumezipata katika Wilaya zetu ni kidogo mno. Ukiangalia maafisa ugani tuna shortage kubwa kwa kila kijiji, kila Wilaya Maafisa Ugani wa Kilimo ni wachache mno na Maafisa Ugani wa Mifugo ni wachache mno. Hizo ndiyo indicators ambazo tuki-focus nazo na tukazifanyia kazi sekta ya kilimo ikakua tutakuwa tumesaidia kuwainua asilimia kubwa ya Watanzania kwenda kwenye uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, kwenye upande wa masoko; lazima ile value chain ya kilimo tuisaidie. Tumepata tatizo la ukame, nilitegemea kuona mipango ya Serikali ya ujengaji wa warehousing, kila Wilaya iwe na maghala ya kuhifadhi vyakula, wakati wa harvest vile vyakula ambavyo vinakuwa ni surplus tunakuwa tuna maghala vinahifadhiwa vizuri, demand na supply vinakuwa-balanced kulingana na serving za mazao kwa kila Wilaya.
Mheshimwa Mwenyekiti, bila hizi warehousing kila Wilaya unakuta wananchi wanalazimika kutumia kile wanachokipata kabla hakijaharibika kwa sababu preservation method za warehousing hatunazo katika Wilaya zetu. Sekta ya kilimo ni nyeti sana na nipende kuishauri Serikali hii midterm review tunayoifanya wajikite sana kwa kuangalia tunawasaidiaje Watanzania kuboresha sekta ya kilimo ambayo inaajiri asilimia kubwa ya Watanzania. Nakushukuru!