Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nianze kumshukuru Mungu wote tupo salama mpaka siku ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niipongeze Serikali kwa namna ya pekee ambavyo wameweza kunyanyua kiwango cha ukusanyaji wa mapato yanayotokana na kodi na yale ambayo hayatokani na kodi, tunapongeza sana. Tukiangalia miezi hii sita ya mwanzo TRA wameweza kukusanya 7.2 trillion ukilinganisha na miezi sita kama mwaka wa fedha uliopita 6.4. Kwa hiyo, ni hatua nzuri na Mheshimiwa Rais aendelee na juhudi hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini upande wa Halmashauri zetu zimefanya vibaya kidogo. Wamekusanya shilingi bilioni 117 ambayo ni sawa na asilimia kama 70, sababu ni zipi? Bado tuna vyanzo vichache vya mapato au kuondolewa kwa property tax na kukusanywa kwa upande wa TRA? Kwa hiyo, tungeomba Serikali waweze kuangalia suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tatizo lililopo pia ni haya mapato ya Halmashauri jinsi gani yanapelekwa kwenye miradi ya maendeleo. Halmashauri nyingi kutokana na uhaba wa OC wanatumia fedha zote na kwenye miradi ya maendeleo haziendi. Kwa hiyo, Serikali ifanye tathmini ya hii miezi sita, mapato ya ndani kila Halmashauri ilikuwa ni ngapi na kulingana na sheria ya asilimia 60 kwenda kwenye miradi ya maendeleo wamepeleka asilimia ngapi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niipongeze Kamati kwa kazi nzuri sana ambayo wameifanya. Wametoa maoni na tunaomba Serikali iyachukue. Kwanza tukianza na pendekezo la kujenga zahanati kwa Serikali kutoa shilingi bilioni 30, ni muhimu sana. Tuna vijiji karibu 12,800 sina takwimu za haraka sidhani kama vijiji zaidi ya asilimia 60 vina zahanati. Halmashauri yangu nina vijiji 59 lakini zahanati zipo kwenye vijiji 17 tu na ukiangalia uwezo wa Halmashauri nyingi kuweza kukamilisha masuala haya ni ngumu. Kwa hiyo, tuombe Serikali hiyo shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati kwenye bajeti ya 2017/2018 waiweke. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Kamati imeiomba Serikali kuongeza tozo kwenye mafuta kwa ajili ya Mfuko wa Maji. Sera ya Maji ya mwaka 2012 inasema kwamba wananchi watapata maji ndani ya mita 400 lakini mfano kwenye Jimbo langu mtu anakwenda kufuata maji mpaka kilometa tatu, ni tofauti na sera. Sasa tukishaitunga sera ni lazima tuweke mipango ya kuweza kuitekeleza. Mipango yenyewe ndiyo hayo maoni ya Kamati tuongeze kwenye mafuta kutoka sh. 50 mpaka sh. 100.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge la bajeti ya 2016/2017 tulihimiza sana hapa ndani, lakini Serikali haikuchukua ikasema tutaangalia bajeti hii, sasa bajeti hii tunaomba msiangalie basi mkubaliane na maoni ya sisi Wabunge ili tukatatue matatizo ya maji vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu asilimia 34 ya wananchi ndiyo wanaopata maji safi na salama. Kwa hiyo, ni jinsi gani tutaweza kutatua hili tatizo la maji, tuongeze hii shilingi 50 na tunaomba sana hiki kilio mkisikie. Kwa kufanya hivyo ndiyo utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwani wananchi wana kilio sana na maji na sisi Wabunge tunasema tukitatua tatizo la maji hata 2020 mtatuona tena humu ndani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi tumeahidi kutoa shilingi milioni 50 na Serikali imekubaliana, wametenga kwenye bajeti shilingi bilioni 59. Hata hivyo mpaka sasa hivi ule mpango mzima wa jinsi gani huu mfuko utaendeshwa ili tuondokane na yale matatizo ya awali yaliyotukumba kwa zile fedha maarufu zikiitwa za JK ambazo watu waliona ni za bure na hata hizi shilingi milioni 50 wananchi kule wanafikiria ni za bure, hapana! Tunaomba tuwaambie wananchi hii itakuwa ni revolving fund, mnakopa kwa riba iliyo ndogo ili na wengine waweze kukopa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iangalie uwezekano wa kwenda angalau kata chache kwa kila Jimbo. Kupeleka shilingi milioni 50 kwenye kila kijiji itahitaji fedha nyingi sana. Sasa hivi tukiangalia makusanyo ya ndani ya Halmashauri, zile asilimia 10 kwa ajili ya vijana na akinamama wanaojitokeza kukopa hawakopi kwa kiasi kingi. Kwa hiyo, hata hii shilingi milioni 50 kwa kuwa itahitajika hela nyingi na makusanyo yetu hayatoshelezi kama bajeti ilivyo, basi tuangalie kata chache ziwe kama za mfano tuguse kila Jimbo angalau hata kata mbili shilingi milioni hamsini hamsini ndiyo tuanze kama mfano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wengi wamezungumzia kuhusu mapato. Naomba nichangie, zile ripoti, Chenge I na II bado Serikali irudi mle ikapekue. Suala la deep sea fishing hatujalisikia na masuala mengine. Kwa hiyo, tunaomba sana kwenye hii bajeti, Waziri wa Fedha na Kamati ya Bajeti mrudi kwenye ile ripoti ya Chenge I na II muangalie maeneo yote ya mapato ambayo yalielezwa ambayo yatasaidia katika bajeti yetu. Mwelekeo wa bajeti ni shilingi trilioni 32, tunatoka kwenye shilingi trilioni 29. Sawa, mmeweka vyanzo vingine pale lakini muangalie jinsi gani tunaweza tukafika hata shilingi trilioni 34 kutokana na vyanzo vingine vipya vya mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wamelalamika kuhusu Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye utalii, basi Serikali ifanye utafiti, je, kweli hii kodi ambayo imewekwa kwenye auxiliary services za watalii imepunguzwa kwa kiasi gani ili watu wapate uelewa? Nafikiri wakati Waziri Mkuu anafunga Bunge, naomba Waziri wa Maliasili na Utalii ampe hiyo taarifa aweze kuisoma hapa tupate uelewa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara imeshazungumzwa upande wa transit goods, tumeweka VAT ambayo imeleta mgogoro sana na mizigo yetu mpaka kupungua. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais jinsi alivyoweza kujenga mahusiano na viongozi wa nchi jirani na sasa biashara imeanza kurudi na tumeona kwenye vyombo vya habari hivi karibuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala ya kilimo kama ndiyo Uti wa Mgongo na asilimia 70 ya ajira. Tunaomba ruzuku iongezwe na pembejeo zije kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna eneo ambalo bado hatujaona ni jinsi gani tunaweza kupata fedha ni upande wa mifugo. Tuweke blocks za ulishaji na watozwe. Kwa hiyo, Serikali iangalie suala hili na tupunguze migogoro hii ya wakulima na wafugaji na tuone ni kwa jinsi gani tunaweza kupata mapato kutoka kwenye mifugo, hili ni eneo ambalo bado hatujaliweka sawa. Tunatoza mifugo tu inapouzwa mnadani lakini kwa kila siku inavyokuwepo na uharibifu wa mazingira kama tunavyoelewa, tuangalie tunawekaje tozo katika mifugo ili tuweze kuongeza mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kamati wameeleza suala la utawala wa Kibunge kwamba Bunge sasa litakuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Wabunge na Kamati nyingi hazikuweza kwenda kukagua miradi ikiwa ni sehemu ya kuisimamia Serikali kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 63 kwamba Bunge tuna wajibu wa kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Sasa tunavyoenda kama Kamati kukagua miradi ya Serikali ndipo tunapoisimamia. Kamati nyingi hazijafanya safari na maslahi ya kiujumla kwa mfano, je, Mbunge anatakiwa akakae hoteli ya nyota ngapi? Kwa hiyo, tuangalie maslahi ya Wabunge na gharama kiujumla katika kufanya kazi zao za kuweza kuisimamia Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunavyokagua miradi ndiyo tunatia chachu kwa watumishi wetu kule, wakisikia Kamati inakuja ndipo utaona mambo mengi yanakwenda mbiombio wanakimbizana. Tunapotoa maagizo inasaidia sana katika kutekeleza miradi na ndipo tunaleta tija kwa wananchi ili waweze kujua kwamba Serikali yao sasa imewaletea miradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho naomba niseme kwamba, tunaenda nchi ya viwanda lakini tunaomba Serikali iangalie uwiano. Siku za nyuma Hayati Mwalimu Nyerere alijaribu kuangalia uwiano wa Kikanda kuweka viwanda ili kuweka usawa katika ajira. Kwa mfano, Mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora, Chunya wanalima tumbaku. Je, hatuna haja Serikali ikashawishi NSSF au PPF, hii Mifuko ya Jamii wakaingia ubia na Vyama vyetu vya Msingi kutoa mchango wao kwa kujenga kiwanda Tabora ili …
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.