Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nianze kuipongeza sana Kamati kwa kazi waliyoifanya ingawa taarifa yao ni ya quarter moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka niishauri Serikali. Siyo dhambi kufanya evaluation ya kipindi cha miezi sita na kurudi kwenye drawing table ili kujipanga upya. Ukisoma taarifa ya Kamati, ukisoma Taarifa ya Hali ya Uchumi aliyoiwasilisha Mheshimiwa Waziri kwenye Bunge hili, ukisoma Taarifa ya BOT waliyoitoa Desemba inatuonesha kabisa tuna kila sababu ya Serikali kurudi kukaa chini kujitathmini na kupanga upya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe indication chache ambazo kwa upande mmoja Kamati wamezi-observe upande mwingine taarifa ya BOT waliyoitoa Desemba wamezionesha. Kwenye taarifa ya BOT na Waziri wa Fedha kwenye taarifa yake aliyoisoma juzi ndani ya Bunge hili, ukisoma kwenye taarifa aliyoisoma kwenye Bunge hili, item number (6) na (7) naomba ninukuu. Kwenye item number (6), Mheshimiwa Waziri anasema:-
“Kiashiria kingine cha jumla cha afya ya uchumi wa Taifa ni mfumuko wa bei ambao unapima mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zinazotumiwa na kaya nchini. Mfumuko wa bei ulipungua kutoa 6.5 Januari mpaka 5.5 Juni 2016”.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda item number (7), Mheshimiwa Waziri anasema:-
“Kuna viashiria vinavyoonesha uwezekano wa kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutokana na hali ya ukame uliojitokeza hapa Tanzania na Ukanda wa Afrika Mashariki na uwezekano wa kuongezeka kwa bei za mafuta katika soko la dunia” Mheshimiwa Mwenyekiti, item (6) ni viashiria vya kuporomoka wakati item (7), kuna uwezekano wa kupanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya Benki Kuu inasema, headline inflation ime-grow kutoka 0.1% kwenda 1.1% na contributing factor ni energy na fuel growth. Kwa hiyo, tafsiri yake ni nini? Ni kwamba kuanzia leo Januari mpaka tunapofika Julai hali ya mfumuko wa bei itakwenda juu. Maisha ya Watanzania yatakuwa magumu. Kwa hiyo, ni vizuri sasa Serikali ikachukua hatua ili ku-rescue situation inayotukabili huko mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? Kwa sababu sehemu kubwa ya bajeti yetu tuliyopitisha, fedha za maendeleo tulitarajia kutoka nje ya nchi. Hali inavyoonesha tume-attain less than 30% na kuna uwezekano development partner wasitupatie hizi fedha. Tumekimbilia kwenda kukopa ndani ambako tume-burst, tumekwenda 132%. Tafsiri yake mzunguko wa fedha kwenye soko utashuka maisha yataendelea kuwa magumu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea kushuka kwa shilingi. Mheshimiwa Waziri anatuonesha confidence na mimi nayasema haya kufuata maelekezo yako kwamba tujikite kwenye ripoti ya Kamati, najenga hoja zangu hizi za awali ili ripoti ya Kamati ambayo wamei-submit hapa iweze kutu-guide na Serikali ikubali kuna tatizo. Dola ya Kimarekani wameamua wao wenyewe kuongeza kutoka 0.25% interest kwenda 0.5% na wana project by December itakwenda 0.75%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafsiri yake ni kwamba madeni tuliyokopa kama nchi gharama yake itaongezeka. Serikali inasema deni linahimilika, Mheshimiwa Waziri umefika wakati sasa, ushauri wangu kwenye hili, tuanze kulitathmini deni letu sio kwa GDP tulitathmini deni letu kwa mapato yetu halisi against revenue kwa sababu tunalipa kwa kodi tunayoikusanya kutoka kwa Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nchi, Kamati imesema na Serikali imesema kwamba tumekusanya vizuri kodi kutoka kwa Watanzania, tafsiri yake ni nini? Tumetoa fedha kwenye mifuko ya Watanzania, tumeipeleka Serikalini. Njia pekee ya kutatua hii changamoto ni fedha hizi zirudi kwa shughuli za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niipongeze Serikali kusaini mkataba wa ujenzi wa reli ya kati na Waturuki wa kilometa 200. Naipongeza sana na nikitazama kwa bajeti ya 2016/2017 achievement zitaonekana kwenye item ambazo hazigusi maisha ya Watanzania moja kwa moja, ndege tuta-attain na hilo ni jambo jema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaelewa sana Wizara ya Fedha wanafanya jitihada ya kutuondoa kwenye consumption based economy kwenda kwenye investment based economy lakini hatutakiwi ku-destroy fundamental pillars tulizozijenga, uchumi wetu muda mrefu umekuwa based on consumption.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niishauri Serikali, tuna dhamira ya kwenda kwenye viwanda, angalieni takwimu zifuatazo. Ukisoma taarifa ya Waziri na taarifa ya Kamati tunasema kwamba tumepunguza importation lakini importation zipi tulizopunguza? Capital goods imports zimeshuka kwa 33%, building and construction zimeshuka kwa 29%, machinery zimeshuka kwa 36%, fertilizers zimeshuka kwa 24%, transport equipment zimeshuka kwa 32%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii tafsiri yake ni nini? Ni kwamba uwekezaji kwenye viwanda haupo! Hakuna mtu anaenda kuwekeza! Kwa hiyo, Serikali sasa hivi inachotakiwa kukifanya na mkubali kwamba bajeti ya mwaka jana tuliyopitisha haikuwa realistic! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri la kwanza na tulisema kwenye bajeti wakati tunachangia mwaka jana kwamba wakati umefika tuwe na realistic budget na vipaumbele ambavyo tunaweza ku-attain kwa muda mfupi. La pili, financial institution, Waziri amesema Benki zetu ziko imara, moja ya benki iliyopata hasara quarter ya pili ni Tanzania Investment Bank, ndiyo ime-lead! Imepata hasara ya 20 billion shillings lakini hoja tunayoisikia sana kutoka Wizara ya Fedha ni kwamba provision zinazowekwa na benki za non-performing loans ni nyingi ndiyo maana wanapata hasara. Kunapokuwa na NPL nyingi sio rocket science ni kwa sababu wakopaji waliokopa wameshindwa kulipa! Kwa hiyo, wanacho-provide ni kwamba hazitakusanyika huko na kwa kuwa hazitakusanyika maana yake mabenki yatapata hasara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tazama Benki yetu ya Kilimo ilikuwa ina 56 billion shillings, wamekopesha only 3.6 maana yake hakuna mikopo inaenda kwenye sekta ya kilimo. Sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa kutuletea fedha zetu za nje pamoja na tourism lakini hali ya nchi inavyoonekana, sekta ya kilimo imeshuka kwa 0.5. Kitakachotokea mavuno ya 2016/2017 itashuka zaidi kwa sababu hatukutenga fedha kwa ajili ya pembejeo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa perception ya Serikali sasa hivi kwamba uwekezaji kwenye pembejeo na researchers wamefanya uchunguzi duniani kwamba msipo-provide fedha nyingi kwenye kilimo kwa kuwekeza kwenye pembejeo ukuaji wa sekta ya kilimo utakuwa ni historia, hatuwezi! Kwa hiyo, ningeiomba Serikali, Wizara ya Kilimo uwekezaji kwa ajili ya pembejeo kwenye bajeti ijayo ufanyike…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naunga mkono ripoti ya Kamati.