Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Mengi yameshasemwa, lakini napenda ni-concentrate katika mambo mawili au matatu. La kwanza, nilikuwa naangalia ripoti hii ya wenzetu, ni nzuri sana, Kamati inawapa pongezi mmeiweka ripoti vizuri. Nilipokuwa napitia ukurasa wa 42 kuhusu ukuaji wa Sekta ya Kilimo na kwamba asilimia 70 ya nchi yetu wananchi wetu wanategemea kilimo na kwamba sekta hii ndiyo inaweza kuondoa umaskini hasa vijijini na kweli vijijini ndio kwenye hii asilimia kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikaanza kujiuliza, hii slogan ya Kilimo Kwanza tumeisikia muda mrefu sana, slogan hii sikuona ikiwekewa mikakati ya jinsi ambavyo ingeweza kutekelezwa. Nilikuwa nikipitia, nikiangalia jinsi ambavyo Kilimo Kwanza kingetekelezwa wakati kila sekta inafanya bajeti yake, Sekta ya Maji imegeukia kulia, Sekta ya Kilimo imegeukia kushoto na sisi tunaongelea Kilimo Kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama priority ilikuwa katika umwagiliaji, kwa akili ya kawaida ungetegemea hizi sekta mbili ziweze kufanya assessment, ni maeneo gani basi tunakwenda kuyaboresha, je, tunakwenda kwenye Bonde la Rufiji, kulikojaa maji, yale maji tunayatoaje pale? Ili bonde lile liweze kuilisha Tanzania na nchi za jirani, hilo hulioni. Hiyo slogan imekwisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuja slogan ya viwanda nayo naiangalia, hivi priority ya viwanda vyetu ni ipi, tunaangalia vyuma au tunaangalia kilimo ambacho tunajua kwanza ndiyo uti wa mgongo ili tuwe na ile backward and forward linkage tuweze kuoanisha kwamba kama basi tunataka viwanda priority yetu iko kwenye moja, mbili, tatu. Kwa hiyo, wakulima wetu wawezeshwe katika kilimo hiki na pesa nyingi iwekwe hapo, hasa katika umwagiliaji na ninyi muangalie ili tusitegemee mvua, huvioni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najiuliza hivi viwanda navyo vitakuwa kama Kilimo Kwanza, nchi yetu kwenda kwa slogans tu? Kama tunakwenda kwa slogans hivi tunamdanganya nani. Ningetegemea basi hata Wizara hii ya Fedha na Mipango waite hizi sekta Ministries wakae pamoja wawe focused, waangalie kwamba tunaomba pesa nyingi iwekwe katika sekta hizi mbili, tatu, ili tuweze kupata azma tuweze kufikia lengo letu la viwanda, kinyume cha hapo hii slogan nayo itapita kama ilivyopita ya Kilimo Kwanza. I am sure ukiangalia unaona kilimo kimewekwa pembeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa Kamati wametuwekea vizuri sana kwamba hii sekta itategemea umwagiliaji, sasa kama umwagiliaji Wizara ya Maji na Umwagiliaji wameweka mikakati ya kufanya sensa kwamba ni sehemu gani kuna maji mengi yanayoweza kutumika kwa umwagiliaji ili iweze ku-demarcate yale maeneo kwamba yatamwagiliwa na kwa malengo gani, kwamba tuta-produce kiasi gani? Nilishangaa wakati mmoja, nafikiri ilikuwa mwaka jana, Waziri wa Kilimo alivyozungumza, alipokuwa Soko la Kibaigwa kwamba ameshangaa mazao yamekuwa mengi sana na storage hamna, kwa hiyo yapo nje yananyeshewa yanaharibika, Waziri wa Kilimo anashangaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu tunasema tuna upungufu wa chakula, kwa kweli ukiangalia ni utani, ingekuwa hizi Wizara zinaendeshwa na Wapare na Wachaga ningesema hawa ni watani wa jadi, lakini unaona watu tuko serious, tunakaa hapa Waziri anasema ameshangaa mavuno ni mengi hamna pa kuweka, hii inaniambia kwamba hatufanyi kazi kwa kuweka malengo au malengo yetu tunaweka madogo sana, hatuwi realistic, hatutumii wataalam wetu kufanya projections, matokeo yake tunashangaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachonishangaza zaidi, wakulima na wafugaji wote wako chini ya Wizara moja na kila siku kuna vita kati ya wakulima na wafugaji. Hivi hiki Kilimo Kwanza ambacho sasa Kamati hii inatilia mkazo kitakuwaje kama mtu amelima kesho ukiamka wanyama wameingia wamekula mazao yako yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unaangalia Wizara moja mmeshindwa kuja na mikakati ya kuona mifugo yetu itunzweje, kilimo chetu kitunzweje. Bado wafugaji wetu ni wale wa kuswaga, zile artificial insemination centers zimekufa wakati ukiangalia hizi Sekta za Kilimo, Ufugaji na Utalii zingeweza kutoa nchi hii katika umasikini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunaambiwa tuna ng‟ombe wengi, viangalie ving‟ombe vyetu vilivyokondeana, uliza anatoa lita ngapi per day, tunaringa katika Afrika Tanzania ni ya pili ikifuatiwa na Ethiopia, yet miaka yote hii hatuna mikakati. Unamwambia mfugaji punguza mifugo humpi target, huyu anafuga 2,000, huyu 10,000, huyu 500, huyu 200, unamwambia apunguze, apunguze kutoka wapi kwenda wapi, akipunguza anapeleka wapi, kama anamuuzia Mheshimiwa Profesa Maghembe ni palepale si ndiyo, mifugo inatoka hapa inakwenda pale, hatuna viwanda vya nyama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa anapunguza anapeleka wapi, unatoa mzigo kichwani unaweka begani ndiyo kupunguza huko? Kibaya zaidi humpi alternative, unaboreshaje ng‟ombe wako, tuwe na shamba darasa weka ng‟ombe kumi tukuonyeshe jinsi ya kuwaboresha vis-a-vis ng‟ombe wako 1,000, mfugaji ataweza kuelewa. Hufanyi hivyo unamwambia punguza, amuuzie nani, kiwanda kiko wapi?
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Sasa nasema kwa kweli kama nchi yetu inge-concentrate Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa anapunguza anapeleka wapi, unatoa mzigo kichwani unaweka begani ndiyo kupunguza huko? Kibaya zaidi humpi alternative, unaboreshaje ng‟ombe wako, tuwe na shamba darasa weka ng‟ombe kumi tukuonyeshe jinsi ya kuwaboresha vis-a-vis ng‟ombe wako 1,000, mfugaji ataweza kuelewa. Hufanyi hivyo unamwambia punguza, amuuzie nani, kiwanda kiko wapi?
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Sasa nasema kwa kweli kama nchi yetu inge-concentrate na kilimo tungekwenda mbali sana. Ahsante sana.