Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru kwa kunipa nafasi nichangie taarifa yetu ya Kamati ya Bajeti. Kwanza nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kuongeza bajeti ya Serikali kwa upande wa miradi ya maendeleo hadi kufikia asilimia 40. Tunachoomba tu kwamba pesa ziendele kwenda kwa wakati ili miradi itekelezwe kama ambavyo tumepanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia niipongeze Serikali kwa hatua ya kusaini mkataba kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati. Reli ya kati ni kama mishipa ya fahamu ya mwili wa binadamu kwa uchumi ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuendelea kwa kutegemea bidhaa na malighafi zetu kubebwa na Lori moja moja kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma, Mwanza na kwenda nchi za jirani na hilo hilo lirudi lije lichukue kwa kweli hili haliwezi kutufikisha mbali lakini kwa hatua hii ya Serikali kusaini Mkataba wa kujenga reli tena kwa standard gauge kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kama hatua ya kwanza naipongeza sana na tunaomba vipande vilivyobaki basi vifanyiwe haraka ili mradi huo uweze kukamilika kwa wakati ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ningependa Serikali kulisisitizia ni eneno la EPZA. Kamati ilitembelea eneo la Mheshimiwa Benjamin Mkapa pale Mabibo, kwa kweli kule ndani kuna kazi nzuri sana inayofanyika na kuna ajira nyingi sana zinazotolewa kwa vijana wetu. Bidhaa zinazozalishwa pale ni za ubora wa hali ya juu na za mauzo ya nje ambazo zinatuingizia pesa za Kigeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kitu kama kile tulitegemea Dar es Salaam pale tuwe na EPZA kama mbili na ikiwezekana angalau kila mkoa tuwe na eneo la EPZA kwa sababu ni eneo ambalo linakuza ajira, linaingiza mitaji, linatuongezea teknolojia kutoka nje. Eneo la Kurasini tayari Serikali ilishalipia fidia kwa hiyo, tunaomba wawezeshwe EPZA kuweza kujenga miundombinu na hivyo kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza katika eneno la EPZA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la tatu, kwa sababu umenipa dakika tano, ningependa kusisitiza suala la utekelezaji wa mradi wa Mchuchuma na Liganga. Mradi huu umezungumzwa kwa muda mrefu sana na ni mradi ambao kwa kweli utaleta viwanda mama, viwanda vya vyuma, viwanda ambavyo vitaleta viwanda vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua iliyofikiwa si mbaya kwa maana kwa upande wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia makaa ya mawe sawa, lakini upande wa chuma. Makaa ya Mawe yale na chuma tunategemea kwa kiasi kikubwa yasafirishwe kupitia Bandari ya Mtwara na reli ambayo tayari feasibility study ilishakamilika, upembuzi yakinifu ulishakamilika sasa hii tathmini ya fidia ilishakamilika, kwa hiyo, tunaomba fidia ile iweze kulipwa na ile reli kutoka Mtwara kwenda Mchuchuma na Liganga na matawi yake kwenda Mbamba Bay upewe umuhimu wa hali ya juu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu chuma kile bila reli ile na makaa ya mawe yale bila reli ile kwa kweli hatuna barabara za kuweza mzigo mzito kama ule sana sana barabara zetu zitakuwa ni za kujenga baada ya miaka miwili zimeharibika halafu tunawalaumu waliojenga au waliosimamia kuzijenga lakini ni kutokana na mzigo mzito kwa hiyo nisisitize mradi wa Liganga na Mchuchuma na pia reli ya kutoka Mtwara, Liganga na Mchuchuma vitekelezwe kwa wakati muafaka ili kukuza uchumi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana ulinipa dakika tano nisingependa unigongee kengele, naunga mkono hoja.