Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti napenda nikushukuru sana kwa nafasi hii, mapema kabisa niseme kwamba naunga mkono hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia juu ya utalii na namna ambavyo tunaweza kuuboresha utalii wetu. Nianze tu kwa kusema kwamba utalii wetu unachangia asilimia 17.5 ya mapato yetu yote ya mwaka ya Taifa na asilimia 25 ya fedha zote za kigeni tunazozipata. Aidha, inatoa ajira kwa watu laki tano, ajira za moja kwa moja na Watanzania milioni moja wamejiajiri wao wenyewe katika utalii na potential ya kuongezeka ni kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sekta ya utalii ikiwa na mchango wake mkubwa huu na ukizingatia kwamba hata mtu anayenunua sukari, unga, misumari kwenye duka la mtaani analipa VAT. Hutegemei kwamba sekta ambayo inachangia karibu moja ya tano ya pato lote la Taifa nchini ifanye biashara hiyo bila kulipa au kuchangia mapato ya kodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utakumbuka wakati ulipokuwa Mwenyekiti wa Kamati hii ya Bajeti mwezi Juni mwaka 2015 mliwaita wadau wengi sana kuzungumza nao na kuangalia namna ya kupanua wigo wa kodi hapa nchini. Mwezi Juni mwaka 2015 mlikutana na wadau wa utalii na kuwapa taarifa kwamba mmeona kwamba huduma za utalii ni moja ya maeneo ambayo mnafikiria kuyaongeza kwenye wigo wa kodi. Wakati ule Wadau wakaomba mwaka mmoja ili waweze kujiandaa na kweli kwa mwaka ule 2015/2016 wakapewa ahueni hiyo na mwaka 2016/2017 ndiyo kodi hii ikaingizwa kama mapendekezo ya Kamati yetu hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa ni-propose hata tabasamu kidogo kwamba Kamati hii imekuwa na mchango mkubwa katika kuiangalia bajeti na kuongeza mapato ya Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, VAT inatumika duniani kote, nchi jirani yetu iliondoa VAT katika kipindi hiki cha mwaka 2016/2017 kwa sababu maalum. Katika mwaka 2013/2014, Watalii walioingia kule walikuwa milioni mbili lakini mwaka 2015/2016 waliteremka wakafika milioni moja nukta tatu. Kwa sababu hiyo wakaona labda wakiondoa VAT watarudisha watalii wafike kiwango kile ambacho kilikuwa nyuma na ninyi mnajua wote kwamba ilitokana na Ugaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa kwanza wa kutoza VAT hatujaona negative impact ya VAT kwenye idadi ya watalii. Napenda pia niseme kwa sababu muda wenyewe ni mfupi sana na niwapongeze Waheshimiwa Wabunge…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.