Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii na naomba nianze kwa kusema naunga mkono hoja iliyowekwa mezani na Kamati yetu ya Bunge ya Bajeti. Nimpongeze Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati hii, Mheshimiwa dada yangu Hawa Ghasia pamoja na Makamu wake na Wajumbe wote wa Kamati yetu ya Kudumu ya Bajeti kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya kwa kutushauri sisi Serikali na kutusimamia. Kwa kweli mnafanya kazi nzuri sana. Hongereni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme machache kwa sababu muda ni mfupi ambao nimepatiwa, naomba nianze na hili ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi wameonesha concern yao kwamba Serikali ipunguze kukopa ndani, tunapunguza mzunguko wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge na Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali yetu inakopa katika soko la ndani kwa kuzingatia uwezo wa soko lenyewe na kuhakikisha kuwa haipunguzi uwezo wa Taasisi hizi kukopesha Sekta Binafsi na watu binafsi. Hili naomba lifahamike kuna miongozo, kuna vigezo na lazima tufahamu hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wameihusisha pia na kukopa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, lakini naomba pia ifahamike kwamba Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ina taratibu na miongozo ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na kupanga kiwango au kiasi cha fedha wanazoweza kuweka katika hati fungani na dhamana za Serikali. Kwa hiyo, kama Serikali tuko makini, hatuwezi kabisa kukopa katika Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii mpaka ikafikia kiwango cha kushindwa kulipa wastaafu wetu. Tuko vizuri, tuko imara na mifuko yetu inafuata miongozo kila kitu na wala hamna shida katika hili. Niombe tu kuwajulisha kwamba mikopo ya ndani pia ni njia mojawapo ya kuimarisha Sekta Binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inapokopesha ina uwezo wa kufanya hivyo. Kwa hiyo, tukizuia na kusema kwamba hapana kwa Serikali tutakuwa tunaiua Sekta yetu Binafsi, tutaua Taasisi zetu ambazo zinaweza kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo pia Waheshimiwa Wabunge wameongelea kwamba Mabenki kufanya vibaya kwa sababu hiyo tunakopa, kama nilivyosema mwanzo hapana. Mabenki yetu sasa yanajitathmini yenyewe. Tukumbuke tuliwahi kusema hapa ndani ya Bunge hili kama Serikali yetu kwamba ilifika sehemu mabenki haya yakawa yanatumia pesa ambazo sio za kwake na yakasahau jukumu lao kubwa. Kwanza anapokuja mtu kukopa pale benki anatakiwa afanye tathmini - ilikuwa haifanyiki. Niko Wizara ya Fedha nawasiliana na nafanya vikao na ma-CEO wa mabenki haya, wanaeleza kabisa kwamba sasa mtu aki-apply mkopo wanakwenda kwenye vigezo. Ilifika sehemu wanakopesha bila vigezo na ndiyo maana ya kuongezeka kwa mikopo chechefu. Lazima tuweke uimara katika usimamizi wa sekta yetu ya fedha ili tuweze kutoka vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa kulitolea ufafanuzi au kuchangia hoja hii ni kuhusu kodi ya majengo kukusanywa na TRA. Katika hotuba hii iliyowasilishwa na Kamati yetu ya Bajeti na data tunazoziona ni kwa quarter ya kwanza na katika quarter ya kwanza, Januari mpaka Septemba, TRA hawakukusanya kodi ya majengo na Halmashauri zilipewa maelekezo waendelee kukusanya kodi hii ya majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, performance tunayoiona ni ya Halmashauri zetu kukusanya kodi ya majengo na ndiyo maana Serikali imeona sasa kama Halmashauri zetu zinakusanya katika level hii inaonesha kabisa haziwezi na sasa TRA ichukue kodi hii ili iweze kukusanya. Itakapoletwa taarifa ya nusu mwaka iki-include na quarter ya pili tutaona utofauti mkubwa wa kodi ya majengo ambapo TRA wameanza kukusanya kuanzia mwezi wa Kumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tuelewe nia ya Serikali na lengo la Serikali yetu ni jema. Halmashauri zetu zilishindwa kufanya vizuri ndiyo maana kama Serikali tumechukua ukusanyaji huu na mtaona tutakapoleta tathmini yetu ya nusu mwaka, kuna utofauti mkubwa katika hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mengi naomba nimalizie kwa kusema katika hili la kufunga biashara nimeona pia Wabunge wengi wameshangilia. Ndugu zangu naomba mfahamu sasa hivi tunarasimisha biashara zetu. Tunaona TRA wanatoa TIN mpya, biashara zilizofungwa ni 4,183, naomba tufahamu katika hili. Biashara mpya zilizofunguliwa ni 1,039,554. Kwa hiyo, naomba niseme katika hili, tutaleta taarifa katika Bunge lako, tunamalizia kufanya tathmini ya ukubwa wa biashara zilizofungwa na ukubwa wa biashara zinazofunguliwa. Kwa hiyo, lazima tuongee tukiwa na data ndugu zangu ili tuweze kuitendea haki Serikali yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.