Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabisa, napenda kutoa pongezi kwa Kamati ambayo imewasilisha muda siyo mrefu, kwa sababu kuna mambo ya msingi wameweza kuyaweka bayana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukianza na suala la Serikali kuchelewa kupeleka fedha za miradi katika maeneo husika, hasa katika eneo la umeme; mimi ni miongoni mwa wahanga katika tatizo hili. Umeme wa upepo Singida, kwa muda mrefu, toka miaka ya 1990 mpaka
Bunge lililopita, Serikali imekuwa ikipiga danadana kuhusiana na suala hili. Majibu ni yale yale! Kila siku Mheshimiwa Waziri husika anapokuja kuzungumzia suala hili, analeta majibu yale yale ambayo anayazungumza toka Bunge lililopita na bahati nzuri ni Waziri yule yule kutoka Bunge
lililopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishauri Serikali, kama wameshindwa kupata fedha kutoka nje ambazo wanazitegemea, basi ni heri atumie fedha za ndani kutekeleza mradi huu, kwa sababu ni muda mrefu sana. Tumepewa majibu haya haya kila siku, wananchi wa Mkoa
wa Singida wamechoka na Wabunge wa Singida naamini hapa wataniunga mkono katika hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba katika suala hili la umeme wa upepo wa Singida, Serikali, kama kuna uwezekano wa kuchukua fedha kutoka ndani, ichukue na itekeleze mradi ule kwa sababu kiukweli tumechoka. Upepo wenyewe labda tungekuwa tumepewa na mtu;
tumepewa na Mwenyezi Mungu, ilikuwa ni suala la Serikali kutekeleza mradi huu na kuweza kutimiza ahadi ambazo wanazitoa kwa wananchi wa Mkoa wa Singida.
Mheshimiwa Naibu Spika, Singida ninyi Chama cha Mapinduzi mnajua ni champion wa kutoa kura kwa Chama cha Mapinduzi mfululizo miaka yote, lakini ni miongoni mwa watu ambao kwenye miradi mmewasahau. Naomba suala la umeme wa upepo wa Singida, Serikali ilichukulie kwa uzito wa kipekee, kwa sababu ni ahadi za muda mrefu sana ambazo zimekuwa hazitekelezeki.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuachana na hayo, naomba pia nizungumzie suala ambalo limekuwa likizungumzwa miaka nenda miaka rudi karibu Mabunge yote; ni suala la mikataba kuwekwa wazi. Namaanisha mikataba ya gesi pamoja na mikataba ya madini specific. Suala hili la mikataba kuwekwa wazi limeshazungumzwa kwa muda mrefu sana. Wamezungumza Awamu ya Nne, wamezungumza Awamu ya Tatu na Awamu ya Tano tena tunalizungumza suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Serikali yoyote ambayo inajipambanua kwamba yenyewe ni ya uwajibikaji, uwazi na ya kutumbua majipu, suala la mikataba kuwekwa wazi lilikuwa siyo suala la kuanza kuihoji, lilikuwa ni suala ambalo lilipaswa kutekelezeka tu. Miongoni mwa vitu ambavyo tulipaswa tuvizingatie ni pamoja na sisi kuwa Wajumbe kwenye organizations ambazo zinazungumzia masuala ya mikataba kuwa wazi. Mfano, sisi ni member kwenye OGP (Open Governance Partnership), lakini toka mwaka 2011 tumekuwa member katika organization hii,
bado vitu vyetu tunafanya kwa mazingira ya usiku usiku; Bunge usiku, mikataba usiku.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado sisi toka mwaka 2009 ni member kwenye Shirika la EITI (Extractive Industry Transparency Initiative). Hii ni aibu. Ukiachana na sisi kuwa member katika hizi taasisi, lakini bado Awamu ya Nne Bunge hili lilipitisha sheria ya kutaka mikataba kuwa wazi na
Mheshimiwa Rais, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akasaini, lakini danadana zikaanza kupigwa baada ya kufika kwa Waziri husika kwa maana ya kutunga kanuni ambazo zinaweza zikasababisha sheria hiyo kutekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, labda tu ni kutofahamu, linapokuja suala la sheria ambazo zina maslahi kwa umma, kwa mfano, mwaka 2016 tulipitisha sheria ambazo zinafunga vyombo vya habari, zinafunga demokrasia, zimepitishwa Rais akasaini immediately na Waziri husika
akatunga kanuni na zikaanza kutekelezwa, lakini zinapokuja sheria kama hizi ambazo zina maslahi kwa umma, kwamba mikataba iwe wazi, sheria hizi zinakaa muda mrefu sana. Mfano, toka Awamu ya Nne mpaka sasa, bado Mheshimiwa Waziri hajatunga kanuni na mpaka dakika
hii hajasema sababu ni nini. Labda ni kutofahamu, au ni kufahamu lakini ni kiburi tu kwamba mikataba ikiwa wazi kuna faida gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, mikataba inapokuwa wazi, kwanza wananchi wanakuwa na confidence na Serikali yao. Pia mikataba inapokuwa wazi, wale wawekezaji katika eneo husika wanakuwa na mahusiano mazuri na watu wa eneo lilo ambalo linawazunguka kwa kuamini
kwamba wanayoyafanya ni mambo ambayo wanayajua kwa maana yako wazi. Lingine, mikataba kuwa wazi inasaidia sana zile organisations na NGOs ambazo zinafanya tafiti mbalimbali kuwa na correct details, figures ambazo ni sahihi kuhusiana na mkataba husika au investment husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna nchi mbalimbali ambazo unaweza ukafikiri labda ni Tanzania tu tutakuwa wa ajabu sana, lakini zipo nchi nyingi sana ambazo zimeweka mikataba wazi; na kwa sababu ya muda nashindwa kuzitaja lakini nitazitaja chache, ninazo hapa zote.
Nchi ya Liberia, Ghana, Congo, USA, Colombia, Canada; nchi karibu zote zimeweka mikataba wazi. Kwa nini Tanzania tunaendelea kuweka mikataba hii katika hali ya usiku? Naomba kama Bunge, ikiwezekana tutunge sheria ambayo itambana Waziri, kwamba ndani ya miezi sita
atunge kanuni ambazo sheria itaanza kutekelezeka, lakini siyo afanye anavyotaka yeye.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna jambo lingine ambalo limenishtua kidogo na napenda kushare na Wabunge wenzangu humu ndani. Naomba Waziri atakapokuja kuhitimisha alielezee kwa ufasaha kabisa, kwa sababu siyo vyema kuliona linaandikwa kwenye majadala ya Kimataifa halafu kama Wabunge humu ndani hatuna information sahihi. Kuna kampuni inaitwa BG Group ya Uingereza ambayo inamiliki vitalu vya gesi Tanzania. Ilifanya transfer share kwenda Kampuni ya Shell ambayo ni kampuni kutoka Uholanzi. Kisheria na kiutaratibu wakati kampuni inafanya transfer shares, ni lazima kama Serikali tupate kitu kinaitwa Capital Gain Tax, lakini ni aibu kwa Serikali hii, transfer share imefanyika lakini Serikali haijapewa kodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri anapokuja kuhitimisha hapa aseme kama kodi hii imelipwa au kama suala hili lina ukweli kiasi gani? Siyo vyema kuona linazungumzwa na kama Wabunge hatulifahamu lakini pia kama Serikali haiji kutoa maelezo
yoyote kwa maana ya Wizara. FCC hawana majibu, nimewauliza na wakasema watatoa kwa maandishi, mpaka leo hawajanipa; TRA hawana majibu, lakini pia Wizara tunaomba majibu leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala lingine la uwekezaji katika gesi asilia.
Unapozungumzia…
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.