Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili
na mimi niweze kuchangia katika hotuba ya Kamati ya Wizara ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuunga mkono hoja ya Kamati inayozungumzia
habari ya wananchi kupewa maeneo ya uchimbaji, hasa katika eneo la STAMICO. STAMICO
kulingana na maelezo, Serikali imeliteua Shirika la STAMICO kwa ajili ya kusimamia shughuli za
madini kwa ujumla wake pamoja na kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo nchini kwa
ujumla. Lakini kwa hali iliyopo sasa tunaona jinsi ambavyo STAMICO imeshindwa kufanya kazi
yake vizuri. Kwa hiyo, mimi naishauri Serikali iweze kuangalia namna bora ya kuweza kuiwezesha
hii STAMICO ili iweze kutekeleza majukumu yake vizuri kwa ajili ya manufaa ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiangalia eneo moja la STAMICO ambapo imechukua
baadhi ya migodi; katika Mkoa wa Geita kuna mgodi ambao unaitwa Bacliff. Ni muda, tangu
mwaka 2011 mgodi huu umechukuliwa, wameingia ubia na kampuni nyingine ya kutoka nje
inaitwa royalty lakini tangu wamechukua 2011 mpaka sasa hatuoni ufanisi wowote, hatuoni kazi
yoyote inayoendelea ingawaje kwa hali ya kawaida kabisa tunaona wananchi wa kawaida
wanaona shughuli mbalimbali zinaendelea, uchimbaji ukiendelea. Kwa hiyo hatuelewi kitu
chochote hatuoni faida yoyote ambayo kwa mkataba huu imeweza kulinufaisha taifa na
wananchi kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na kwasababu hiyo basi nilikuwa naomba Serikali kupitia
STAMICO, iangalie namna ya kuiboresha hii taasisi ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi kwani
kwa sasa hivi tunaona inafanya kazi zake tofauti yaani hatuoni tija katika shirika hili ambalo
Serikali imewekeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi nyingine ya STAMICO ni kuangalia namna ya
kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi. Lakini
katika suala hili ninaona jinsi ambavyo STAMICO bado inahitaji kujipanga zaidi kwani wapo
wachimbaji wadogo wadogo wengi sana ambao hawafanyi kazi kwa ufanisi zaidi kutokana na kwamba STAMICO bado haijaingia zaidi katika kuwawezesha. Kwa sababu hiyo sasa naiunga
mkono hoja ya Kamati kwa kuona kwamba STAMICO inabidi ijipange vizuri ili ione namna bora
ya kuweza kuwasaidia wachimbaji wadogo ili waweze kuchangia katika Pato la Taifa…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.