Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mimi nilitaka niseme
kwanza niipongeze Kamati kwa taarifa walizoleta, lakini jambo moja nilitaka niseme.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nchi tumekuwa tukijadili suala la kuwa na viwanda.
Mambo mawili ni muhimu sana, sekta ya miundombinu na sekta ya umeme. Nilitaka niishauri
Serikali, imefika wakati wa ku-embrace private sector (PPP), energy sector mawazo ya kufikiri
kwamba tutatumia fedha zetu za ndani kununua majenereta, kuzalisha umeme sisi, TANESCO
izalishe umeme, ifanye nini, hatutopiga hatua ya kuwa na hizo megawati 10,000 tunazotaka.
(Makofi)
Kwa hiyo, mimi ningeshauri, wizara mnafanya kazi kubwa sana kwenye rural energy,
mnafanya jitihada kubwa sana lakini mfungue fursa kwa ajili ya uwekezaji wa sekta binafsi
kwenye umeme, ili watu waweze ku-compete na kupatikana umeme wa bei rahisi ili Mwijage
atuletee viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini umeme hauwezi kuja bila kuwa na proper incentive
scheme kwenye sekta. Ningewashauri Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Fedha, na Wizara
ya Viwanda na Biashara, kaeni chini m-develop incentive scheme kwa ajili ya uwekezaji wa
private sector mziweke wazi ili wawekezaji wajue tukienda Tanzania kuwekeza mtaji wetu, these
are the benefits na Wizara ya Fedha iache mindset ya kuweka kodi kwenye inputs. Tarajieni
kuvuna kwenye matokeo hilo ni jambo muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka niiombe Wizara ya Miundombinu, mmeanza jitihada
kubwa sana ya kujenga reli ya kati, kupanua bandari, ni jambo jema. Lakini kule kwetu Nzega,
kama Mkoa wa Tabora kuna barabara; mwaka 2014/2015 mlituwekea fedha kwa ajili ya visibility
study hazikutosha, kwa hiyo ule mpango wa barabara ya kutoka Tabora kupita Mambali
kwenda Bukene, kwenda Itobo, kwenda Kahama mpaka leo imesimama. Ni ahadi ya Rais
Kikwete, ni ahadi ya Rais Magufuli, kwa hiyo, nakuomba kaka yangu Mheshimiwa Waziri wa
Miundombinu, tukumbuke barabara hiyo ni muhimu sana kwa uchumi wa eneo lile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, kuna Daraja la Nhobola pale Nzega, Mheshimiwa
Waziri unafahamu, tumegonga sana mlango ofisini kwako kuomba haka kadaraja. Sasa hivi
wananchi wa jimbo la Nzega upande wa Nhobola hawavuki kwenda kupata mahitaji katika Mji
wa Nzega, inabidi wazunguke kwenda Tinde kwenda kupata mahitaji Mkoa wa Shinyanga
ambako ni mbali zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye uwekezaji wa reli, Mheshimiwa Waziri hakuna
clause muhimu ambayo mnatakiwa muiweke kama Serikali; mambo mawili, commitment ya
nchi ya mapato yetu ya ndani ambayo tunatoa shilingi kulipa mkandarasi yatumike kama
sehemu ya kulipa contract za ndani. Tukitumia zile fedha kumlipa mkandarasi wa nje maana
yake tuta-transfer dola kupeleka nje, zitatuumiza.