Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa na mimi
niweze kuchangia katika hoja iliyo mbele yetu, ya Kamati ya Miundombinu. Kwanza niipongeze
kamati kwa jinsi ambavyo wameleta taarifa ambayo iko vizuri na ipo very detailed pamoja na
Mwenyekiti wa Kamati hii. Nina mambo machache ya kuweza kuchangia.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni suala la viwanja vya ndege, nikisoma ukurasa wa
17 inaonesha kabisa viwanja vya ndege vingi katika nchi yetu vinaendelea kujengwa. Lakini
kuna viwanja ambavyo vilikuwa vilikuwa vinaendela kwa muda mrefu hadi sasa hivi
wanapoleta hii ripoti havijapelekewa pesa hata senti.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza na kiwanja cha ndege cha Songwe. Kiwanja cha
ndege cha Songwe mwaka 2015/2016, kilitengewa shilingi bilioni tano lakini hawakuletewa
fedha hizo, mwaka 2016/2017, tumetengewa bilioni saba hadi wanaandika ripoti hii
hawajaletewa hata senti tano, maana yake nini?
Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanja hiki, ni mfano mzuri kwa mikoa ya Nyanda za Juu
Kusini, Mkoa wa Mbeya, Rukwa, Katavi, Njombe, Iringa mpaka Songea. Kwa maana nyingine
kwa wale wote ambao wanatumia ndege zinazokwenda Mbeya ni hivi karibuni ni majuzi tu
fastjet imerudi kwa sababu ya kutoweza kutua katika kiwanja kile. Imerudi kwa sababu ukungu
ambao unatanda eneo lile, hakuna taa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nchi na kama Taifa tunataka tuwekeze zaidi katika
masuala ya viwanda, na wawekezaji wengi wanataka watumie usafiri huu wa njia ya ndege
kwa ajili ya kuja kuwekeza viwanda vyao hapa nchini. Kwa hiyo, naiomba Serikali kwamba, kwa
bajeti ambazo zimetengwa katika viwanja ndege mbalimbali kati nchi hii; ukizingatia
Mheshimiwa Rais, nampongeza kwa sababu ameshanunua ndege nyingi katika nchi hii, na
bado tunaendelea kununua kama Serikali. Kwa hiyo, viwanja hivi viweze kupelekewa fedha zao
kwa wakati na viweze kutengenezwa kwa wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine muhimu zaidi ni suala la barabara kwa za
kuunganisha kwa kiwango cha lami. Nizipongeze Serikali ya Awamu ya Nne na ya Tano zote
zinaendelea kuthubutu kuunganisha maeneo mbalimbali katika nchi yetu kwa ajili ya
kuunganisha wananchi, lakini pia kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumi. Nimuombe pia
Mheshimiwa Waziri, kwamba kuna barabara ambayo imeahidiwa mara nyingi, na nimeisema
hapa Bungeni kwa miaka mingi; barabara ya Katumba - Lwangwa - Mbwambwa - Tukuyu,
kilomita 83, na wewe Mheshimiwa Naibu Waziri uliona jinsi ambavyo wananchi tulipokea kwa
furaha na tupo tayari hata kutoa maeneo yetu kwa ajili barabara iweze kujengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni suala la mawasiliano. Mawasiliano katika nchi
yetu yamekuwa kwa haraka sana, lakini jambo ambalo linasikitisha kidogo kwa wenzetu hawa
wa TCRA kumekuwa na utapeli mkubwa sana kupitia mawasiliano ya simu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilikuwa naomba Wizara, lakini pia na wataalam,
kuna wataalam wazuri katika nchi hii ambao wanaweza wakaishauri Serikali ni mechanism gani
zitumike kwa ajili ya kuwabana wale wote ambao ni matapeli kwa njia ya mawasiliamo na
ninaamini kwa kuwa na mimi pia niko kwenye fani hiyo tunaweza tukasaidiana na watu wengi
kuiwezesha Serikali ili wananchi wake wasitapeliwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni suala la umeme/nishati. Nakupongeza sana
Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo pamoja na Naibu wako kwa kazi nzuri mnazozifanya.
Suala la REA III na REA II imekuwa ni changamoto katika baadhi ya maeneo.
Mheshimiw Naibu Spika, mara nyingi Mheshimiwa Waziri umekuwa ukisistiza kwamba
wakandarasi wanapokuja katika maeneo yetu lazima wawasiliane na viongozi ambao ama ni
Waheshimiwa Wabunge ama Madiwani. Lakini kwa bahati mbaya sana wakandarasi
wanakwenda eneo…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja.