Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote niunge
mkono hoja, pia niungane na waliotoa pole kwa wenzetu wana-CCM ambao walipata
majeruhi huko Moshi, tuwaombee ndugu, jamaa na wengine wapate kupumzika salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitajielekeza kwenye mambo ya msingi na niwapongeze
sana Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia, kwenye hoja za maandishi pamoja na zile za
maneno. Kwa ujumla tuna hoja 30 za maneno na za maandishi nane, kwa hiyo, zilikuwa ni hoja
nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge nianze tu na
kuzungumza kidogo, kuhusiana na masuala ya kazi ya kusambaza umeme, hasa kwa Shirika letu
la TANESCO. Nikubaliane na Waheshimiwa Wabunge speed kulingana na uharaka wa
utandazaji umeme kwa kweli haulingani na uwezo wa TANESCO kwa sasa, lakini tunachofanya
ili kuendana na changamoto hizo sasa Serikali imeweka mikakati ya kufuata ili kuhakikisha
kwamba wananchi wanapata umeme kwa haraka kutoka katika shirika letu la TANESCO.
La kwanza kabisa, tunawashukuru Bunge lililopita lilitupitishia bajeti ya kuanzisha ofisi 47
kwa ngazi za Wilaya, sasa tunaanza utaratibu wa kuimarisha ofisi na kujenga ofisi nyingine mpya
katika maeneo ambako hakuna ofisi. Hii ni hatua madhubuti sana kuharakisha upatikanaji wa
umeme katika maeneo yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo kwa sababu wakati mwingine ni
ufinyu wa bajeti, ili kupambana na hatua hiyo, TANESCO sasa imeanza utaratibu ufuatao:-
Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, kwanza kabisa tulishaagiza
transfoma zote pamoja na nguzo yataanza sasa kununuliwa hapa nchini. Hii itarahisisha sana
usambaziji wa umeme kwa kasi kubwa. Kwa hiyo, tuna imani kwamba kwa hatua hii
itaharakisha sana usambazaji wa umeme mijini na vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya pili, wakati tunajipanga kujenga ofisi, tumeanza sasa
kuanzisha madawati ya huduma kwa wateja mahala ambako kuna wateja wengi, badala ya
kusubiri kujenga ofisi mpya. Hii ni hatua madhubuti itaturahisishia sana kusambaza umeme kwa
wananchi wengi na kwa muda mfupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua nyingine tumeagiza shirika letu, kuanzia Januari mwaka
huu, litaanza sasa kufata wateje walipo badala ya lenyewe kufuatwa na wateja. Hii itasidia
sana, kwa sababu maeneo mengine kwa wananchi hawawezi kufikia ofisi zetu na hata wakifika
inakuwa kwa gharama kubwa na wakati mwingine wanakata tamaa. Kwa hiyo, sasa
wataalamu wa TANESCO wa shirika letu wataanza kufuata wateja walipo ili kuharakisha
huduma hizi mahsusi. Kwa hiyo, tunaamini kwamba utaratibu huu utachangia sana kuharakisha
uzambazaji wa umeme ili kulingana na kasi ya ukuaji wa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika sambamba na hilo nizungumzie kidogo kukatikakatika kwa
umeme. Ni kweli, hasa maeneo ya Lindi na Mtwara hata kule Geita kwa Mheshimiwa Kanyasu
na maeneo ya Dar es Salaam. Kazi inayofanyika sasa hivi ni pamoja na ukarabati wa
miundombinu ambayo kwa kiasi kikubwa mingi imekuwa ya muda mrefu. Sasa katika kipindi hiki
kifupi, maeneo mengi yataendelea kupata shida kidogo, lakini ni tatizo la muda mfupi, jitihada
madhubuti zinafanyika ili kurekebisha hali hii. Ni matarajio yetu ndani ya miezi hii miwilii ukarabati
wa maeneo mengi utakuwa umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala la Lindi na Mtwara nielezee kidogo. Lindi na Mtwara
wananchi wa Lindi wanatumia megawati 18. Kwa sasa mashine moja imeharibika, inafanyiwa
ukarabati hasa kuhakikisha kwamba ile mashine iliyoharibika inafanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo ujenzi wa kusafirisha umeme sasa
kutoka Mtwara kwenda Lindi ambako kituo cha kupoza umeme pale Mnazi Mmoja kinajengwa
na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miezi miwili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa wananchi wa Mtwara baada ya kituo kile
kukamilika, hasa kile kituo cha substation kutoka kilovolti 33 kwenda kilovolti 130 zitakapokamilika
matatizo ya kukatika umeme kwa wananchi wa Lindi na Mtwara yatatatulika kwa mara moja.
Kwa hiyo ni vizuri tuwaeleze wananchi wa Mtwara, ni kero hata kwetu sisi tunaliona lakini ni
jambo ambalo linafanyiwa kazi kwa kina sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo lilizungumzwa, ni suala la sera ya mafuta
kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili. Ni kweli kabisa suala la kutafsiri lugha za kigeni sasa ni muhimu
sana kwa sababu watumiaji wengi ni Watanzania ambao ndio kwa kiasi kikubwa wanatumia
lugha ya Kiswahili. Mkatati umeshaanza, timu ya wataalam imeshaundwa inayojumuisha wizara
yetu pamoja na taasisi zinazojumuisha Wizara yetu; lakini kazi hii itafanyika kwa kushirikiana na
TUKI ambao ni wataalam wa kutafsiri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ili kuepika kufanya kazi na TUKI peke yake, na kuna
masuala mengine ya kiteknolojia na ya kitaalam zaidi, lazima timu mbili zifanye kazi kwa
pamoja. Kwa hiyo, utaratibu unaofuata sasa ni kukaa pamoja ili kuanza kazi hiyo mara moja. Ni
matarajio yetu ndani ya miezi miwili/mitatu timu hiyo itakuwa imeshaanza kazi, pamoja na TUKI.
Kwa hiyo, suala la kutafsiri linafanyika na utaratibu tumeshauanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kulinda Tanzanite. Kwanza niseme kwamba ni kweli kabisa
madini ya Tanzanite hapa ulimwenguni yanapatikana Tanzania peke yake, hakuna sehemu
nyingine, kwa maana ya yanakochimbwa. Lakini nikiri kwamba, yako matatizo na changamoto
ambazo zimesababisha pia control yake kuwa kidogo. Hata hivyo hatua za Kiserikali ambazo
zimefanyika, ni vizuri kuwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba hili neneo kuanzia mwaka
2001 lilianza kutengwa kama eneo tengefu ili kuhakikisha kwamba rasilimali ya Tanzanite
haitoroshwi nje bila kuzingatia utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni changamoto kidogo, ilikuwa ngumu na ujenzi wa fence
ulifanyika mwaka 2005, lakini kwa bahati mbaya sana wananchi wanaozunguka maeneo yale
waling‟oa fence pamoja na vyuma. Kwa hiyo, mkakati unaofanyika sasa ni kujenga fence ya
mawe pamoja na tofali, tunatafuta fedha kwa ajili ya kujenga fence hiyo. Kwa hiyo, nikushukuru
Mheshimiwa Ndassa yeye alikuwa Mwenyekiti wa Nishati na Madini huko nyuma huko nyuma
kwa kuliona hili, lakini jitihada zinafanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati mingi sana imefanyika katika eneo hili. Pamoja na
kuanzisha Police Post, kimejengwa Kituo mahususi cha polisi pale Mererani ili kuhakikisha
kwamba udhibiti unakuwa imara na ambao kwa kweli ni shirikishi. Tunaamini kwamba hatua hizi
zimechangia kwa kiasi kikubwa kusaidia madini yetu yasiende nje sana. Lakini pia, kuna joint
committee iliyoundwa ikishirikisha taasisi mbalimbali ikiwemo Uhamiaji, TRA na nyingine ili
kudhibiti utoroshaji huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hayo ili kupunguza utoroshaji wa madini
ya Tanzanite, mwaka 2010 Sheria ya Madini Mpya ilivyotungwa ilipunguza kiasi cha mrabaha
kutoka asilimia tano kwa madini yaliyokatwa kurudi asilimia moja ili kuvutia Watanzania wengi
kukata madini ya Tanzanite hapa nchini. Kwa hiyo, hizo ni hatua ambazo Serikali imechukua,
ambazo ni vizuri sana kuwaeleza wananchi, lakini pia, changamoto tunazichukua bado
tutaendelea kuimarisha ulinzi zaidi katika eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu REA III nikubaliane na Waheshimiwa Wabunge wengi,
REA II iliyokamilika hivi sasa kwanza niseme imekamilika kwa asilimia 95.8 na asilimia 4.2 iliyobaki
ni kwa ajili ya kuwaunganishia umeme wateja. Sasa kazi ya kuunganisha umeme inategemea
mambo mawili, la kwanza utayari wa mwenye nyumba, mtaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, basi nijielekeze la
mwisho, nizungumzie kuhusiana na mikakati ya REA III. REA III imeshaanza maeneo ya mikoa sita
kama nilivyotaja juzi, Mkoa wa Pwani, Mara, Arusha, Iringa, Njombe, Mbeya pamoja na
Songwe, kwa hiyo, tumeshaanza na utaratibu utakwenda hivyo kwa nchi nzima, na mpaka
kufikia tarehe 31 Machi nchi nzima sasa wakandarasi watakuwa wameingia kwenye mikoa yote
kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa REA III.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zitakazofanyika, nisaidie kunipa dakika moja kwenye hili, ni
pamoja na kufikisha umeme kwenye vijiji vyote vilivyosalia ambavyo ni 7,873 pamoja na
vitongoji vyake. Lakini kazi ya pili ni kupeleka umeme kwenye taasisi zote za umma, hapa nina
maana ya hospitali, zahanati, magereza, polisi, shule, masoko pamoja na pampu za maji. Kwa
hiyo, huu ni mradi mkubwa, tunatarajia wananchi wote watapata umeme kwa kupitia mradi
huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia utapeleka umeme kwenye maeneo ambayo yako nje na
gridi, hasa visiwani pamoja na yale ambayo yanapitiwa na Hifadhi za Taifa. Ni mradi wa miaka
minne hadi mitano, kwa hiyo, mwaka wa 2020/2021 tuna matarajio kwamba vijiji vingi vitakuwa
vimepata umeme kupitia mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kusema jambo hili ambalo nadhani ni tamu sana
kwa Waheshimiwa Wabunge. Hatua tunayofanya kwa sasa ni utandazaji wa umeme shirikishi.
Kabla mkandarasi hajaingia kwenye site yoyote ile ataanza kwanza kupiga hodi kwa Mbunge husika. Hii itasaidia sana kupeleka umeme maeneo ambako wananchi mnajua vipaumbele,
lakini pia ataenda hata kwa Mheshimiwa DC na Mkuu wa Mkoa ili kusaidia katika usimamizi
wake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo kwa sababu muda ni mfupi,
ningependa niseme mengi sana kuhusu hili, nashukuru sana. Naunga mkono hoja.