Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.
Kwanza nianze kwa kusema kuna mengine yalikuwa ni ya utawala, mengine ni ya
kibinafsi, mimi sitagusia mambo ya utawala kwa sababu tuna mihimili mitatu, siwezi kuja kujadili
mambo ya utawala Bungeni, nadhani si utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, cha pili. Labda ifahamike vizuri sana hii ya bei, mimi
ninawasiliana na Waziri, ninawasiliana na Mwenyekiti wa Bodi. Kwa hiyo, aliye na barua kutoka
kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji au Mwenyekiti wa Bodi ya EWURA hiyo ndio anapaswa
kuileta hapa Bungeni, ndio mimi nawasiliana nao hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ninafanya vikao vingi sana na wafadhili, vingi sana. Ni
vizuri ukiwa na barua moja uje na barua 20 maana vikao vyangu na wao ni vingi mno.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tuje kwa mambo ya msingi. Kuhusu magwangala, niseme
vilevile kwa kifupi, nina ripoti nimetoa ushauri kwenye kila tani kumi ya magwangala ndio natoa
gramu nne! Kwenye kila tani kumi natoa gramu nne! Na yale magwangala katika kuchambua
dhahabu, mgodini wametumia siodine na huyu anakuja kutumia mercury! Waheshimiwa
Wabunge ninaacha mfanye tafsiri wenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeulizwa swali la capital gain kati ya BG na Shell. Ukweli ni
kwamba Shell hawajalipa capital gain, hata mchana huu nilimuita Vice President wa Shell
ametoka London, kujadiliana nao. Msimamo wa Serikali ni kwamba lazima capital gain ilipwe
kwa sababu iko kisheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, uwazi wa mikataba. Tulishasema mara mia hapa kwamba
yeyote anayehitaji mkataba wowote ataupata, tutauleta kwa Spika na pale atapata sehemu
atasoma, atarudisha. Na niombe, labda kwa kuwa kwa Spika labda ni usumbufu sana,
Mheshimiwa yule Mbunge Jumatatu, saa 2.00 asubuhi nimewaambia TPDC waweke mikataba
yote wampe asome. Ndio uwazi huo, hakuna cha kuficha. Aende asomee pale TPDC. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ya kusema uzoefu wa nchi zingine kwamba mikataba
inawekwa wazi, Waheshimiwa Wabunge na ninyi ni wazoefu, hakuna nchi ambayo unakuta
mkataba umeandikwa kwenye gazeti. Na kama kweli mkataba unaandikwa kwenye gazeti,
basi tuanze na mikataba yetu sisi wenyewe tuliyonayo tuchapishe kwenye magazeti. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sheria na kanuni. Ni kwei tunachelewa kutengeneza kanuni,
sasa hivi kanuni mpya nzuri kabisa ni kwamba mgodi wowote unaoanzishwa mara moja
unaenda kwenye Soko la Hisa. Sasa malalamiko kwamba hatufaidi yamekwisha, na ile iliyoanza
zamani imepewa miezi sita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndugu zangu wa Kahama, Tarime, nendeni soko la
hisa sasa hakuna kisingizio kwamba, hatufaidiki. Narudia, Kanuni inasema lazima asilimia 60
zikamatwe na Watanzania, twendeni soko la hisa. Unajua huku sasa twende kwa vitendo
Waheshimiwa Wabunge, kwa vitendo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ruzuku kwa wachimbaji wadogo. Ruzuku zipo, iko kwenye Ilani
ya CCM na hizi ni fedha za mkopo wa World Bank. Wengine walisema ooh, nilijadiliana na World
Bank kuhusu bei ya umeme! Nina mijadala mingi, mbona hii ya wachimbaji hawasemi? Fedha
zipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu TANESCO deni lake. TANESCO wanadaiwa, kama
alivyosema Mwenyekiti, zimeshavuka shilingi bilioni 820. Na mimi bado msisitizo wangu sikubali TANESCO ipandishe bei hata kama wengine wakizunguka na barua, msimamo wangu huo
unafahamika, kwa sababu hili deni la shilingi bilioni 320 hatujalichambua, hatuwezi kuangalia tu
wanasema uzalishaji wa umeme ni wa bei kubwa lakini hatujachambua. Mtu hajaniambia kwa
nini bwana fedha wa kituo kimoja ana hoteli 4 wa TANESCO, huyo nae tumchangie, tupandishe
bei, haiwezekani, haiwezekani! Au mtu ananunua lita 20 anaandika amenunua lita 50!
Zimewekwa gari zote za TANESCO tracking system, hata maruti, hata zilizo kwenye mawe, eti
tupandishe bei umeme! Narudia, haiwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kila mwisho wa mwaka wanapeana bonus milioni 50,
utapandishaje bei kwa ajili ya bonus zao? Haiwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, umeme haupandi hata mtu azunguke, kwanza wote
wanafahamu, World Bank, African Development Bank, European Union kitu ambacho nilikuwa
napambana nao, sikubali umeme upande. Lakini ukiangalia ile action plan wanasema tarrif review, nayo ni kiingereza. Review
maana yake sio hacking, you can review and go down. Hizi document ukizunguka nazo ni tafsiri vilevile.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatu. Tuongee cha maana
zaidi. Ni kwamba, tukitaka Taifa letu liendelee ni lazima FDI (Foreign Direct Investiment) za
kutoka nje tuzivutie kutoka za sasa hivi 2.5 mpaka zaidi ya 15 ifikapo mwaka 2025. Na kufanya
hivyo kati ya mwaka huu na mwaka 2020 tunahitaji investment kwenye umeme; tunahitaji dola
bilioni 12. Alichosema Bashe ni muhimu 12 billion ikifika mwaka 2020 wakati tutakuwa na
megawati zaidi ya 5000. Na ndiyo maana tunaibadilisha TANESCO iwe ya kisasa na itaumiza
wenye biashara huko wanachukia lakini lazima ibadilike, iendane na haya matakwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kusema mengine ya muhimu sana kwamba
hatujafaidika na gesi, umeme tunaoutumia hapa mwingi ni wa gesi na kitakachotupeleka nchi
ya kipato cha kati ni uchumi wa gesi. Tuna mradi mkubwa wa LNG, tunaujadili, utachukua
muda utakuja hapa Bungeni. Tuna bomba la Tanga litakuja hapa Bungeni, kote tupo kwenye
matayarisho. Investment ya bomba la Uganda ni bilioni 3.5; lazima mtayarishe kabla hamjaanza
ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, investment ya Liquefied Natural Gas (LNG) ya Lindi ni 30 billion
US Dollars; wapo kwenye matayarisho. Juzi nimetoka Zambia tumeleta tena mradi mwingine
mkubwa, bomba lingine tena; hii ndio maana inaitwa nchi ya mabomba mzee ambao
utakuwa karibu wa dola bilioni mbili. Sasa hii unaweza usione kitu kinafanyika, hii ni lazima ninyi Waheshimiwa Wabunge mje hapa, miradi hii inataka sheria, watu wamejifungia huko sasa hivi
hatulali mchana na usiku. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda cha mbolea Mheshimiwa aliesema tunajenga
viwanda viwili, kimoja Kilwa na kingine Lindi. Cha Kilwa investment yake ni bilioni 1.9...
(Hapa kengele ya pili ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru Kamati na Waheshimiwa Wabunge, naunga
mkono hoja.