Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. PROF. NORMAN A. SIGALLA KING – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE
YA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kipekee kabisa kwanza
kupongeza wachangiaji wote 15 ambao wamechangia kwa maandishi na 22 wamechangia
hapa Bungeni. Mambo machache tu niangalize.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema shukrani hizo, Waheshimiwa Wabunge
nichukue nafasi hii kipekee kabisa kumpongeza Waziri mwenye dhamana na wasaidizi wake
wote kwa sababu kwa muda wote ambao Kamati imekuwa ikifanya kazi zake wamekuwa
wakitupa ushirikiano mkubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mambo machache ambayo mmesisitiza ni pamoja na ujenzi
wa reli ya kati, barabara mbalimbali, bandari zote kwa maana ya Dar es Salaam ,Mtwara,
Tanga na Bagamoyo; lakini pia mmesisitiza upande wa ATCL. Pia Waheshimiwa Wabunge
wamesisitiza sana juu ya ajira pale bandarini na kwamba wako watu walioajiriwa ambao
wamefukuzwa kama hivi; sisi kama Kamati tumepokea taarifa hiyo na Wizara imesikia na sisi
wajibu wetu tutafuatilia kuona kwamba Serikali inafanya inavyopasa kama lililofanyika
halikupaswa kufanyika hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge nitumie nafasi hii kusema mambo
machache tu, na hasa juu ya mradi huu wa reli ya kati. Ninaipongeza sana Serikali kwa sababu
dhamira yake na haya maneno niliyasema Dar es Salaam wakati wa kusaini mkataba juzi wa kutoka Dar es Salam kwenda Morogoro. Nikasema kwa sababu mipango yetu ya kwanza ya reli
yetu haikuwa kilometa 160 kwa saa, kuchelewa huku ndiko kumetupelekea kwenye kilometa
160 kwa saa. Nikasema kama kuchelewa ni huku basi ni kuchelewa kuzuri, maana sasa
tumeenda kwenye spidi kubwa zaidi yenye manufaa zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini muhimu kabisa ambalo Wizara ni vizuri ifahamu ni
kwamba kukamilika kwa reli ya kati ni jambo moja, muda wa kukamilika reli ya kati ndio muhimu
zaidi. Kwa sababu zilezile kwamba mzigo tunaotegemea ili uweze kurudisha mkopo wao wote
wa reli ya kati ni ule ule ambao Kenya, Uganda, Rwanda, DRC na Zambia wanautegemea.
Ndio maana nasisitiza tena na Kamati inasisitiza tena kwamba vyovyote itakavyokuwa tumieni
mkandarasi yoyote mnayemjua kwa vipimo mnavyovijua, muhimu reli hii ikamilike haraka kabla
wenzetu hawajakamilisha, hilo ni muhimu kwetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, na nisisitize tu kusema pia kwamba naunga mkono vizuri sana,
Mheshimiwa Waziri amesema amegawa vipande vingi vingi kwa maana ya ujenzi wa reli ya kati
na sisi Kamati hatuna tatizo na hilo lakini bado tunasisitiza kwamba standard ya reli na
upatikanaji wa funding ndio unaotengeneza hot cake ya project yoyote. Narudia, project
yoyote haiwi viable kama funding haipo; kwa hiyo ni funding inapokuwa available ndio
inafanya mradi kila mkandarasi aone ni hot cake. Unayejua umuhimu wa kuchukua mizigo
Kigoma au kuchukua Kalemi kule Mpanda ama Mwanza ni wewe Mtanzania; mjenzi
anachoangalia ni funding. Ndiyo maana Serikali mjipange ili kufasili kwa usahihi kwamba
funding iko vipi na kwahiyo tunaelekea wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nichukue nafasi hii tena kuomba sasa
kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu lilidhie taarifa ya Kamati ya Miundombinu iwe maelekezo
rasmi kwa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.