Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze mambo mawili tu kwa kuwa mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji nataka nichangie kwenye maeneo mawili muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la Mfuko wa Maji, nashukuru Waziri wa Fedha yupo, fedha pekee ambazo Wizara hii inapata ni fedha za Mfuko wa Maji peke yake. Ukiacha fedha za Mfuko wa Maji, Wizara ya Maji haipati fedha za maendeleo ya miradi ya maji kutoka Serikalini. Kwa hiyo, tunaomba ufafanuzi na tunaomba suala hili Waziri wa Fedha alieleze Bunge hili kwa nini fedha za maendeleo ambazo tulizipitisha kwenye Bunge hili la Bajeti haziendi kwenye Wizara ya Maji ukiacha na fedha za Mfuko wa Maji ambazo ni shilingi 50, tunachangia huko tunaponunua mafuta.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili; suala la Bandari ya Uvuvi. Tangu Bunge la Kumi, Wabunge hapa walikuwa wanapiga kelele suala la Bandari ya Uvuvi, tunapoteza fedha nyingi sana katika nchi hii kwa kukosa Bandari ya Uvuvi, nimesikitika sana. Nimestaajabu kuona Wajapani wametoa fedha kujenga Bandari ya Uvuvi eti inakwenda kujengwa Chato!
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Uvuvi ikajengwe Chato wakati tuna maeneo kwenye Bahari Kuu tunapoteza fedha nyingi wavuvi wanakuja kuvua wanashindwa kutua Tanzania kwa sababu hatuna Bandari ya Uvuvi. Kwa nini Bandari ya Uvuvi msifikirie kuipeleka Mtwara, kwa nini msifikirie kuipeleka Tanga, kwa nini msifikirie Bagamoyo, Bandari ya Uvuvi ukaweke Chato kwa samaki gani walioko Chato ili tukajenge bandari kubwa ya uvuvi na kwa kiwango gani cha fedha ambazo tunapoteza kwenye Ziwa Victoria? Kwa nini tusifikirie kujenga Bandari ya Uvuvi kwenye Bahari ya Hindi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu hili suala kwa kweli linatia doa Serikali yenu. Bandari ya Uvuvi imekuwa ikidaiwa sana humu ndani na tunapoteza fedha nyingi kwenye Bahari Kuu, kwa sababu ya kukosa Bandari ya Uvuvi, leo Bandari ya Uvuvi inaenda kujengwa Chato, fedha waliyotoa Wajapani ni jambo la hatari na ni jambo ambalo kwa kweli linafedhehesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ambalo nataka nizungumzie ni suala la migogoro ya wakulima na wafugaji. Mheshimiwa Mchengerwa amezungumza hapa na mimi ni Mjumbe wa Kamati. Kwa kweli mwenyewe pia sikufurahishwa sana na taarifa tuliyoiandika kuileta hapa juu ya migogoro ya wakulima na wafugaji. Migogoro hii haipungui, inaongezeka. Mheshimiwa Waziri, tunahitaji migogoro ya wakulima na wafugaji ipungue, badala ya kila siku inaongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ina makakati gani wa kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji ili suala hili liwe historia? Vifo vinaongezeka, migogoro inaongezeka, hata maeneo yale ambayo kulikuwa hakuna migogoro ya wakulima na wafugaji kama Lindi hivi sasa na kwenyewe kumeshaanza kuwa plotted ni maeneo ya migogoro. Tunaomba Wizara iwe serious, mnapoamua kumaliza changamoto za wakulima na wafugaji...
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Bobali.