Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimshukuru jirani yangu Mwita Gatere, Mbunge wa Bunda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na suala la tembo. Tembo ni tatizo Mkoa wa Mara. Tembo ni tatizo Serengeti ni tatizo Bunda, ni tatizo Tarime. Nichukue nafasi hii kutangaza janga la tembo Serengeti, Tarime na Bunda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imefika sehemu tembo anaenda kutafuta chakula kwenye ghala, anabomoa ghala, juzi hapa, ameenda kwenye Kijiji cha Nyichoka, wakabomoa ghala wakala chakula isitoshe wananchi wakahamishia chakula ndani ya nyumba akaenda akabomoa nyumba akala chakula chote, wananchi wamebaki hawana chakula. Bahati nzuri amekuja Naibu Waziri, tumempeleka mpaka maeneo hayo amekuta nyumba zimebomolewa.(Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tembo anauwa wananchi kwa wingi sana sasa hivi, tembo amekuwa ni hatari sana kwenye ukanda wetu huo. Kama Serikali isipochukua hatua ni hatari kubwa mtasikia huko. Sasa hivi majambazi wanauwa tembo hawaendi kuwatafuta hifadhini wanakuja kuwavizia kwenye vijiji vya Serengeti nje kabisa. Juzi hapa nilimwambia Mheshimiwa Waziri wamekuja wakaua tembo sita katika kijiji cha Merenga, wakawapiga wakaua wakang’oa meno wakaenda. Kwa hiyo, sasa hivi majambazi hawasumbuki kwenda kutafuta tembo hifadhini maana tembo wanakuja huku kusambua wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie Wizara ya Maliasili na Utalii chukua hatua ya ku-protect wananchi wa Serengeti, Bunda na Tarime dhidi ya tembo. Kama hamtafanya hivyo tembo wanaenda kuisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni WMA.WMA ni chombo cha wananchi, wananchi wameji-organize wakatoa maeneo ya wakaunda WMA. Leo Wizara ndiyo inakusanya mapato yanayotokana na WMA kwa nini? Kwa mfano, tumeenda Babati kwenye ile WMA ya Burunge Wizara inakusanya mapato, imekusanya shilingi bilioni sita inawapelekea milioni 800 for what? Unakusanya bilioni sita unarudisha milioni 800 itafanya nini? Kwa hiyo, mimi niiombe Serikali, suala la WMA ukusanyaji wa mapato, uendeshaji wa WMA waachie WMA wenyewe, waendeshe wenyewe, wakusanye mapato yao, wajiletee maendeleo wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine linalotesa WMA ni single entry. Tunaomba Serikali ifanye utaratibu wa kurekebisha bila kurekebisha issue ya single entry WMA zitakufa. Kule kwangu Serengeti WMA ya Ikona sasa hivi mahoteli yaliyokuwa ndani ya hifadhi wawekezaji wameanza kuondoka, kwa sababu hakuna wageni. Serikali naomba mrekebishe hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni mauaji, kwangu Serengeti wameuwawa watu 50 na askari wa wanyamapori, ninayo taarifa ambayo nimeandikiwa na Serikali za Vijiji, Watendaji wa Vijiji ambavyo viko kandokando mwa hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba orodha hii nitakuletea uone askari wa wanyamapori wanauwa Watanzania wenzao kisa amekanyaga ndani ya hifadhi anapigwa risasi anauawa. Mimi binafsi Ryoba nimeshuhudia wameuwa, hivi huu ndiyo utaratibu au ndiyo maana Magufuli ameweka Katibu Mkuu mwanajeshi, Mwenyekiti wa Bodi Waitara mwanajeshi ili kuwaua Watanzania wanaoingia hifadhini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu wameuwawa vijana 50, huu ndiyo utaratibu wa Tanzania kuua vijana wake? Ndiyo utaratibu wa Serikali ya CCM? Hebu ninaomba Serikali chukua hatua, kama hamtachukua hatua nitawashughulikia mwenyewe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine…
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Ryoba dakika zako zimeisha.