Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ninamshkuru sana na Mheshimiwa Gekul kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya maji ni mbaya, jana nilikuwa nasikiliza vyombo vya habari vya Kimataifa, watabiri wanasema Vita ya Tatu ya Dunia itatokana na upungufu wa maji katika dunia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba pale Rombo Mheshimiwa Waziri wa Maji na Naibu Waziri wa Maji mmekuwa maarufu sana kwa Warombo, sababu ni tamko lenu la kuifuta Kili water. Baada ya kutoa tamko la kuifuta Kili water iliyowanyanyasa Warombo kwa ajili ya maji kwa miaka mingi sana, walikuwa wana matumaini makubwa sana sasa kuna jambo litafanyika tuweze kuwa na mamlaka yetu ili tuweze kuratibu matumizi ya maji kidogo tuliyonayo pale Rombo. Mheshimiwa Waziri nawaombeni sana hili jambo liweze kufanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli ni kwamba shida ni kubwa kuliko miaka mingine yote. Hivi ninavyozungumza ukame umeleta athari kubwa sana, vyanzo vidogo vya maji ambavyo tulikuwa navyo sasa vinatoa maji asilimia ndogo kabisa. Mheshimiwa Waziri bahati mbaya sana visima ambavyo tulivipata kutokana na mradi ule wa visima kumi vya World Bank mpaka sasa hivi miundombinu yake bado haijakamilika kutokana na ukosefu wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kisima kwa mfano cha Shimbi Mashariki, visima kwa mfano vya Leto na vinginevyo maji yamepatikana lakini usambazaji umekuwa shida kwa sababu fedha hazijapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna imani na nyinyi kama nilivyowaambia baada ya kuifinya Kili water tumejenga imani kubwa sana na ninyi tusaidieni, kwa sababu hata huu utaratibu wa Halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia maji, own source ndogo haiwezi kufanya Halmashauri ikapata fedha ya kutenga kwa ajili ya kusaidia miradi ya maji. Kwa hiyo, ni matumaini yangu Mheshimiwa Waziri hilo utalichukulia kwa uzito mkubwa na pale Rombo pana Ziwa Chala ambalo lina maji, maji yale yanatumika na wenzetu Kenya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliuliza swali hapa nikajibiwa wakati huo Waziri Maghembe akiwa Waziri wa Maji kwamba maji ya Ziwa Chala ni maji ya Kimataifa, kwa hiyo, kuna mikataba ambayo lazima iangaliwe. Tunachoshangaa watu wa Rombo maji ya Ziwa Chala yanatumika Kenya, kwa nini yasitumike Rombo? Ninaomba sana Mheshimiwa Waziri muangalie uwezekano haya maziwa yaweze kutumika pia kusaidia watu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ambalo ningependa kulizungumza ni kwa Waziri wa Mifugo na bahati nzuri amekaa jirani na Waziri wa Viwanda.
Nimesikia sana huku Bungeni kwamba wafugaji wapunguze mifugo na kadhalika, waipunguzie wapi? Kwa sababu hakuna viwanda vya nyama hapa nchini, ng’ombe jinsi alivyo nyama ni pesa, ngozi ni pesa, kwato ni pesa na mifupa ni pesa. Kwa nini tusianzie hapo? Mheshimiwa Waziri teta na mwenzako upo jirani naye hapo alete viwanda kwa ajili ya mazao ya mifugo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mwijage kama alivyotueleza jana pale yuko sharp, ng’ombe zikiwa na afya huwa zinavuka Ngorongoro zinaenda kiwanda cha nyama Thika Kenya, huu ni ukweli kabisa, lakini sisi tumekaa hapa tunapiga hadithi tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tulivyounda ile Kamati ya Migogoro ya Wakulima na Wafugaji tulipita vijijini, wafugaji wanatuambia kuna shamba darasa la kilimo mbona hatujawahi kuona shamba darasa la mifugo? Kwa hiyo, mimi pamoja na kwamba siyo mfugaji kwa ile maana ya ufugaji tunayoijua, lakini naona migogoro mingine ya wafugaji na wakulima inatokana na kutofanya maamuzi ya kusaidia haya makundi ili yakafanya mambo kitaalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni rai yangu juzi nilikuwa natoka kumzika Kaka yake na Mheshimiwa Cecilia Pareso. Pori hilo kutoka Minjingu mpaka Makuyuni ni harufu ya uvundo ng’ombe wamekufa, Simanjiro yote ni harufu ya mizoga ya ng’ombe. Kwa hiyo ni vizuri…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Selasini.